Ugaidi wa Mbowe na Masheikh wa Uamsho

TENGEFU

Senior Member
Jan 25, 2017
138
206
Masheikh wa uamsho waliofanya matendo yenye viashiria vyote vya ugaidi wanaachiwa huru lakini raia mwema ambaye kosa lake ni kutamka tamka “katiba Mpya” anakamatwa na kuuziwa kesi ya Masheikh wa Uamsho. Ugaidi wa Mbowe ni mkubwa kiasi gani ukilinganisha na Masheikh walioachiwa huru.

Mtu anajiuliza kama kweli tuko serious na kupambana na ugaidi, tunawaachiaje masheikh wa Uamsho halafu tunamkamata mbowe ambaye hata hajawahi mmwagia mtu hata maji?

Viongozi wa Tanzania mjue watanzania wanaona na wanajua kuchambua mambo kwa kina na mapana. Kilichozuiwa ni kongamano la Katiba, hivyo tunataka kujua hili lina uhusiano gani na ugaidi?.

Kama kuongelea Katiba mpya tungetegemea pia Jaji Warioba aunganishwe kwenye kesi ya Mbowe; lakini pia kwa muktaza huo walioshiriki Bunge la katiba nao wote ni magaidi.

Lazima ijulikane kuwa watanzania waliomwomba Mungu katika kipindi cha awamu ya Tano bado wako magotini wakimlilia Mungu. Kuna kila dalili kuwa viongozi wetu huingia madarakani na macho na masikio lakini wakianza tu kukalia kiti wanakuwa vipofu na viziwi na mara nyingi hufiisha hisia zao kwa kuhakikisha keki iliyoko mezani haipati hata vumbi.

Ifike mahali viongozi waendelee kujua uongozi ni koti na wasipolivua Mungu atawavua. Na pia viongozi wa Tanzania wajue Mungu hajawaacha Watanzania bali anawajaribu watu mbalimbali kama wanaweza kuwaongoza kwa haki na akiona watu wake wanaumia basi anatumia uungu wake kufanya kazi yake.

Kama kumkamata Mbowe ni amri toka juu basi tumeshaingia chaka hata kabla ya miezi sita ya uongozi wa awamu ya Sita.

Kutaka kuongoza nchi bila challenge ni kujidanganya maana hata wazazi katika familia zao hupata changamoto nyingi toka kwa family Members haswa Watoto lakini husikii wazazi wakiwabambikia Watoto wao kesi. Rais chukulia nchi kama familia ambayo usitegemee smooth leadership.
 
Mimi siyo shabiki wa siasa za mbowe,labda sababu sipendi siasa na Mambo yake, lakini kwa hili la mbowe kusingiziwa ugaidi napinga kwa nguvu Zote.

Mmwache mzee wa watu bwana,watu wenye kesi za ugaidi mmewaachia halafu mnabana huyu

Kuna harufu ya udini hapa
 
Mimi siyo shabiki wa siasa za mbowe,labda sababu sipendi siasa na Mambo yake, lakini kwa hili la mbowe kusingiziwa ugaidi napinga kwa nguvu Zote.

Mmwache mzee wa watu bwana,watu wenye kesi za ugaidi mmewaachia halafu mnabana huyu

Kuna harufu ya udini hapa
kila mtu mwenye uwezo wa kuona mbali anaona kitu fulani hapa
 
Atulie tu gerezani hadi kesi yake iishe, Sabaya atatoka wakati yeye ndio atakuwa anaanza kuzoea jela.
 
No One knows the truth behind, Tutulie then Jamhuri na Serikali yetu Tulivu itatoa tamko, Ukimsiliza kwa makini Msemaji wa Polisi, utagundua kuna kitu kipo nyuma ya Pazia, Tusipende kushanikia vitu tusivyovijua...
 
Hivi dunia hii kuna mtu anaweza kufanya kazi ya hasara? kama sivyo, basi kuna mambo tunaweza tusiyafahamu kuhusu ajenda za siri za CHADEMA
nyuma yao kuna masilahi binafisi na sio kwa Taifa

Ndio maana serikali inawapiga vita sana kuharibu au kuvunja mipango yao.

Pia serikali ikubali kukosolewa tatizo wakosoaji nao wapo kimaasilahi tu
 
Interrogation ?!!!

Hilo neno ni sahihi kulitumia ulivyokusudia?!! Mmh haya mkuu....

#PundaAfeMzigoUfike
#MzigoNiUtulivuWaNchi
#KaziIendelee
Lipo sahihi kabisa labda ulikariri hiyo quotation lakini nimetumia interrogation kwa maana ya majibizano
 
Lisu alikuwa anapewa na nani taarifa za kwamba Magufuli anaumwa na hatapona?

Bila shaka laptop za mbowe zilizokamatwa zimesema mengi kuhusu kundi la kigaidi.
 
Lisu alikuwa anapewa na nani taarifa za kwamba Magufuli anaumwa na hatapona?

Bila shaka laptop za mbowe zilizokamatwa zimesema mengi kuhusu kundi la kigaidi.
Sasa kwani Magufuli alipona??
 
Mimi siyo shabiki wa siasa za mbowe,labda sababu sipendi siasa na Mambo yake, lakini kwa hili la mbowe kusingiziwa ugaidi napinga kwa nguvu Zote.

Mmwache mzee wa watu bwana,watu wenye kesi za ugaidi mmewaachia halafu mnabana huyu

Kuna harufu ya udini hapa
Kwa hiyo unataka kusema ni kutesa kwa zamu! Siamini hivyo
 
Back
Top Bottom