LordJustice1
JF-Expert Member
- Jan 19, 2011
- 2,263
- 530
Nape mimi nashukuru kwa kuja kujibu hoja hapa JF tena kwa jina lako! Tatizo kuu nilionalo kuhusu wewe ni siasa za mipasho za kushambulia "personalities" zaidi kuliko kudeal na maslahi ya nchi! Kwa mfano ulitakiwa kwanza umshukuru Dr W. Slaa kwa kuiwezesha CCM "kujivua gamba" (hata kama mmejivua gamba la kisanii) tangu alipotaja ile orodha maarufu kama "List of Shame!" Badala yake unamwita Dr Slaa "Padre fulani!" Sasa wewe unataka kweli tuamini kwamba una mapenzi mema na nchi yetu kwa kumshambulia mtu aliyekisaidia Chama chenu indirectly? Kwa nini umekalia udini tu na kuwafanya Magamba wenzako waamini kwamba eti Dr Slaa ametumwa na Kanisa kugombea Urais? Kwa kueneza propaganda hizo huoni kwamba wewe pamoja na Rais wako kipenzi unayemfagilia kila siku pamoja na kwamba ameshindwa kazi, mnaigawa nchi yetu kwa misingi ya dini? Kwa kifupi bwana Nape kwa nini unamwangalia Dr Slaa kwa jicho la "upadre" ambao hata hivyo alishauacha? Nape ipo siku vijana watakupiga mawe kama walivyomrushia mawe Rais wako JK! Muda wa kudanganya umekwisha sasa hivi! Wekeni mikakati ya kutekeleza ahadi zenu hewa kuliko kupiga domo tuuuuuu! Tena huyo Rostam Aziz mnatakiwa kumpeleka mahakamani ili akajibu mashtaka, msidai kwamba eti "sisi tumefanya kama chama" huku mkijiita "Serikali ya CCM!" Kisha mfilisi mali zake zote, halafu mumtimue kwenye Chama! Shame on you!Wanaoendelea kudai MIE bado DC pengine Wanasababu zao tusizozijua. NARUDIA NILISHA KABIDHI U DC NINAPOTAKIWA KUKABIDHI NA KWASASA ANAYEKAIMU PALE ANAITWA FATMA ALLY MKUU WA WILAYA YA NANYUMBU. Kuhusu MISHAHARA miwili NADHANI kuna WATU hawajui taratibu ZA utumishi nchini ambazo MIE NI muumini sana. HATA hao wengine wanaotajwa ETI WALIKUA WAKIPATA MISHAHARA MIWILI NI UONGO NA UZUSHI, KATI YA HAO WALIOTAJWA e.i kina MKUCHIKA, HAKUNA ALIYKUWA AKICHUKUA MISHAHARA MIWILI,UKWELI NI KWAMBA UKISHATEULIWA UNATAKIWA KUCHAGUA MSHAHARA MMOJA KAMA UNA KAZI MBILI,SHERIA HAIRUHUSU KULIPWA MISHAHARA MIWILI. KWA MFANO UNAKUWA MBUNGE PENGINE NA RC, UNATAKIWA KUCHAGUA MSHAHARA MMOJA WA U RC AU UBUNGE NA SI YOTE MIWILI.KUNA MANENO HAPA KAMA VILE NIMETUKANA AU NIMETUMIA MANENO MABAYA KWA MTU BINAFSI, NAULIZAX WAPI? HIVI WAPI AMBAPO NIMEMSHAMBULIA MTU BINAFSI? HIVI KUSEMA MTU HALIPI KODI NI DHAMBI KAMA HALIPI?HAPA JF AKISEMA NAPE FLANI ANAKWEPA KODI NI KUONYESHA. KUWA NAPE HANA AKILI KAMA MNAVYONISEMA? TUNAJADILI NCHI YETU, TUKIGUSA MAHALI MSIPOTAKA BAADHI BASI NITAPOROMOSHEWA MATUSI MENGINE AMBAYO MASIKINI WA MUNGU SIDHANI KAMA NINASTAHILI.MIMI KWANGU SIO TATIZO KEJELI ZA BAADHI YA WATU JAMVINI, LAKINI HEBU FIKIRIA ANAYEJIUNGA LEO JAMVINI ASIYEJUA HESHIMA YA HAPA ENZI ZA JAMBO FORUM, ANAJIFUNZA NINI.? Inawezekana NI jitihada ZA makusudu kuvunja moyo WATU wengine tusije HAPA LAKINI NAWAHAKIKISHIA SITAACHA KUJA HAPA KWANI JF LICHA YA KUWA NI SEHEMU NZURI YA KUZUNGUMZA JUU YA NCHI YETU NI MAHALI AMBAPO KWANGU NI SHULE NA KIOO TOSHA,UKIACHILIA MBALI WACHACHE WANAOKIPAKA MATOPE KIOO ILI MTU ASIJIONE VIZURI.MTAKUMBUKA NILITUKANWA SANA HAPA NIKAPEWA KILA JINA NILIPOKUWA NIKISIMAMIA KWA NGUVU WATU KUWAJIBIKA KWA MUJIBU WA MAAMUZI YA NEC, NI HAPA WATU WAKADAI NIMEKURUPUKA, SIO MAAMUZI YA KIKAO, NAKURUPUKA KWASABABU MIE MPUMBAVU, MJINGA, ZEZETA, NEPI nk.LEO TUPO HAPA, NAOMBA MRUDI TENA KUSEMA NILIKUWA NIKISIMAMIA YA KWANGU NA HUKU WATU WANAWAJIBIKA....