Ufisadi wa kutisha wa Bernard Membe

Ufisadi wa kutisha wa Bernard Membe

Mtwara anajenga mahotel ya kitalii kama uyoga kila kukicha katika mitaa mbalimbali, watu wanashangaa pesa hizi anatoa wapi?

Miongoni mwa mahotel hayo limejengwa baharini kabisa, na kulazimika mipango miji Mtwara kuhamisha barabara kuipeleka majini kumsaidia bwana Mkubwa huyu.

Hali ambayo imewanufaisha wengi akiwemo Meya wa mji ambaye naye alibadili eneo la wazi lililokuwa limeachwa wazi kwa ajili ya bahari.
Eneo hilo limebadilishwa na kupima kiwanja cha maakazi eneo ambalo lilielezwa katika ramani mama kuwa halifai kwa ujenzi nyumba za makaazi kutokana na chini kupita mkondo wa maji ya bahari.

Kiwanja hicho nae meya kwa kuona ni bomu amemuuzia mtu mwingine wa CRDB ambaye tayari ameweka msingi looo nchi hii hakuna wizara yenye makucha hata huyu mama haiwezi wizara hii.
 
Sijaelewa yeye ameshiriki kama nani! Muandika uzi unaonekana hujamchimba vzr huyo mheshimiwa, hebu leta isue ambazo anahusika direct( naamini zipo tu) na acha ubabaishaji
 
Wanajamvi kumekuwa na upotoshaji wa makusudi kwenye siasa za Tanzania kumuhusu ndg Benard Membe, waziri wa mambo ya nje na ambaye anatajwa kwenye mbio za kusaka ukuu wa nchi kuwa ni msafi na asiye na doa.

Ukweli ni kwamba huyu hana tofauti na wenzake huko kwenye chama chao,huyu bwana ameitia nchi hii kwenye hasara kubwa kwa makusudi ama kwa malengo anayoyajua yeye.

Akiitumia kampuni ya ujenzi ya shemeji yake Emmanuel Masanche iitwayo MODSPAN bwana huyu alichukua kandarasi ya ujenzi wa gati katika bandari ya Mbamba Bay huko Ruvuma na Kigoma lakini kilichofanyika ni usanii wa hali ya juu kwani gati la Mbamba Bay halikidhi viwango na liliamriwa kubomolewa na kujengwa upya.

Ajabu ni kwamba hasara hii ni ya serikali kwa sababu MODSPAN imelipwa fedha zote na kandarasi imepewa tena kampuni ya kichina kubomoa gati hilo na kulijenga upya huku MODSPAN ikiachwa kwa amani kabisa na haijachukuliwa hatua zozote kisheria kisa kazi ilikuwa ya bwana mkubwa MEMBE.

Hivi huyu anaitakia mema hii nchi kweli ndg zangu.....shime wananchi CCM ni kama ukoo wa panya hakuna aliye msafi huko tuwaondoe

View attachment 149045View attachment 149045

Pichani ni sehemu ya gati hilo la mbamba bay ambalo linavunjwa ili kujengwa upya.

Sifagilii ufisadi. Kama kuna ushahidi achukuliwe hatua.

lakini nahisi hapa kuna mchezo mchafu unafanywa na watu wananunuliwa kuchafua wenzao hasa wale wanaotajwatajwa kwenye mbio za urais 2015 ili kujisafishia njia zao. Unaposifia ufisadi wa Membe, je umejaribu kufuatilia ufisadi wa hao wapinzani wake ndani ya chama chake?

Mimi nazani tungejaribu kuanzisha uzi mpya hapahapa JF wakufichua maovu yote ya hao wanaotaka urais 2015 ili wananchI tuwapime nani wa angalau angalau maana wote NI wachafu ila wanazidiana.
 
Tatizo liko kwetu Watanzania, kuendelea kufikiri kwamba katika CCM huenda bado kuna MSAFI. Baada Nyerere kung'atuka CCM, CCM hakuna msafi hata mmoja. I bet my neck. MFUMO waliouweka CCM after Nyerere NI MFUMO FISADI. Hauruhusu mtu yeyote MSAFI ndani ya CCM to excel na kupata nafasi za juu za UONGOZI. Viongozi wote wa juu wa CCM ni manyang'au. Wale wana-CCM ambao ni wasafi, MFUMO FISADI wa CCM huwatema wakiwa kwenye ngazi za chini za uongozi. Ya Membe is the birds of the same feather flocks together!
 
Nasikia pia alimdanganya Marehemu Gaddafi akakwapua Tshs. 24Bn Fuatilia kwa MO1
 
hii nchi inaliwa na wenye meno jamani, halafu wanakuja baadae kutupa ahadi mi3, kweli sisi watangantika tumekuwa mazombi.
 
NIlitarajia ungeshusha lawama kwa Tender Board, Waziri wa Ujenzi pamoja na Waandisi wa mikoa husika. Waziri wa Mambo ya Nje anahusika vipi na tenda za ndani za ujenzi? Tuseme Membe alitumia nafasi yake ili shemeji yake apate upendeleo; ilikuwaje Mheshimiwa Magufuri na bodi yake ya zabuni ikubali jambo hilo? Membe sio Mhandisi na wala wizara yake haihusiki na masuala ya uandisi...so, ilikuwaje wizara husika itoe tenda kwa kampuni isiyohusika licha ya kwamba ina wataalamu ambao wangeweze ku-asses uwezo wa kampuni husika?

whoops!!! una umri gani dogo? you must be underage...!!!!
 
watunzi wa riwaya wanazidi kuongezeka JF
ngoja tu waimbe rewaya sasa hawana chakutafuna na kusaza kama nyie unategemea wafanyeje?nyie nch ni yakwenu na vizaz vyenu wamekula kushba na kuvimbiwa wazee wenu sasa mpo nyie ndomana wenyenjaa mnatukebeh ila jua kazi 2 kubwa za mdomo.1kula 2kuongea wewe upo namba1 ndo mana tnamshangaa ambaye anaimba riwaya badala yakutafuna nch ya vizaz wenu.
 
Ukiwa mgeni na Tanzania hoja zako zina mashiko. Lakini kwa sisi wenyeji na nchi hii tunajua fika kuwa alichosema mtoa hoja kinawezekana kabisa (ingawa sina hakika kama kweli kimefanywa na Mh Membe a.k.a Joka la Mdimu)
Tumeshuhudia viongozi wakitumia makampuni ya shemeji zao na kutumia madaraka yao kuvuruga mchakato wa tenda mara nyingi, sio kitu kugeni. Kwa Tanzania Membe na Magufuli wanaweza kupigiana simu tu na tenda ikatolewa na BOQ zikawa zinachakachuliwa kupitisha malipo fasta. Haya mambo yanatokea sana Tanzania, haitakuwa ajabu au mara ya kwanza kama ni kweli Membe amefanya ufisadi huo.
Nakubalina na wewe lakini inaonekana mtoa mada ni kama huko kwingine nako ni tatizo lakini tatizo ni Membe. Membe inawezekana kabisa akaomba upendeleo lakini hakuwa na final say. Sasa hapa ndipo tunapotakiwa kufahamu kwamba je, hao wenye final say wali-offer hiyo deal kwa sababu tu Membe ni Waziri au taratibu zilizingatiwa! Suala hili muhimu limeachwa na mleta mada.
 
ngoja tu waimbe rewaya sasa hawana chakutafuna na kusaza kama nyie unategemea wafanyeje?nyie nch ni yakwenu na vizaz vyenu wamekula kushba na kuvimbiwa wazee wenu sasa mpo nyie ndomana wenyenjaa mnatukebeh ila jua kazi 2 kubwa za mdomo.1kula 2kuongea wewe upo namba1 ndo mana tnamshangaa ambaye anaimba riwaya badala yakutafuna nch ya vizaz wenu.
mkuu ungetumia ufahamu huu kuzalisha wala tusingekua hapa kulaumiana
 
Wanajamvi kumekuwa na upotoshaji wa makusudi kwenye siasa za Tanzania kumuhusu ndg Benard Membe, waziri wa mambo ya nje na ambaye anatajwa kwenye mbio za kusaka ukuu wa nchi kuwa ni msafi na asiye na doa.

Ukweli ni kwamba huyu hana tofauti na wenzake huko kwenye chama chao,huyu bwana ameitia nchi hii kwenye hasara kubwa kwa makusudi ama kwa malengo anayoyajua yeye.

Akiitumia kampuni ya ujenzi ya shemeji yake Emmanuel Masanche iitwayo MODSPAN bwana huyu alichukua kandarasi ya ujenzi wa gati katika bandari ya Mbamba Bay huko Ruvuma na Kigoma lakini kilichofanyika ni usanii wa hali ya juu kwani gati la Mbamba Bay halikidhi viwango na liliamriwa kubomolewa na kujengwa upya.

Ajabu ni kwamba hasara hii ni ya serikali kwa sababu MODSPAN imelipwa fedha zote na kandarasi imepewa tena kampuni ya kichina kubomoa gati hilo na kulijenga upya huku MODSPAN ikiachwa kwa amani kabisa na haijachukuliwa hatua zozote kisheria kisa kazi ilikuwa ya bwana mkubwa MEMBE.

Hivi huyu anaitakia mema hii nchi kweli ndg zangu.....shime wananchi CCM ni kama ukoo wa panya hakuna aliye msafi huko tuwaondoe

View attachment 149045View attachment 149045

Pichani ni sehemu ya gati hilo la mbamba bay ambalo linavunjwa ili kujengwa upya.
Basi kama ni kweli wasimguse Lowassa kabisa, nitazaa na mtu atakayemsema Lowassa vibaya bila kutaja hao wengine kama hili jmbazi jipya Membe. Tumeaminishwa Lowassa ni Fisadi namba moja kumbe Membe naye yumo? ndiyo maana naongea akibana pua

 
Maadui 11 na wote watakimbilia Kenya.teh,teh yani CCM bana,kama wehu
 
Ngoja Benard Membe aje humu jamvini atupe majibu ya tuhuma hizi, Lakn tujiulize kama watu makini, taratibu na sheria za manunuzi hazikuzingatiwa? Na kama hazikuzingatiwa nani alaumiwe...
 
Back
Top Bottom