Dakika 45 tayarNaam dakika 45 kutoka sasa naandika tena, ni mkasa muhimu kuutoa kwa jamii una mafunzo ndani yake.
Yani kirahisi tu mkubali kuwa mmeiba mzigo ili mkapumzishwe miezi 6 ndani.Salaam
Leo nimekumbuka kisa cha ndugu yetu mwizi (kaka yangu mtoto wa mama mdogo) ambae alikuwa ameiva kwenye wizi hasa wa kutumia uchawi na mbinu kali za kitapeli.
Nyakati hizo nilikuwa naishi karibu kabisa na nyumba ya familia ya Babu mzaa mama, na mama yangu pamoja na ndugu zake walikuwa wanaishi hapo kwa baba yao.
Huyu kaka yangu alikuwa hajulikani anapoishi ila akiharibu anakuja hapo kwa mama zake kujificha mpaka mambo yatulie, ni mara nyingi amefungwa na kuachiwa, kupigwa na kuja hoi pale nyumbani na wahuni wenzake ambao walimuuguza kwa mitishamba na kumchua kwa majani ya mnyono mpaka atakapopona kwani waliogopa kwenda hospital.
Kuna siku nilifika pale nyumbani nikawakuta na wenzake kama sita hivi juu ya meza wamewasha mshumaa wanatumia madawa ya kulevya, baada ya salamu wakasema dah! Tuna majonzi sana, tumekwenda kuchukua mali mahali ila msala jamaa zetu watatu wale ambao tuliwahi kuja nao hapa...imekuwa bahati mbaya wamechomwa moto!
Jamaa wakisema hivyo huku wanapata vitu vyao kama hakujatokea kitu na wakipumzika siku mbili ujue wanaingia kazini tena.
Mimi binafsi nilishamkuta kwenye pikipiki yangu kubwa akiikata waya ili aiibe, na pia kuna siku niliingia nyumbani kwangu ile kuangalia Tv nikapitiwa na usingizi ilikuwa kama tano usiku, kushtuka nakuta jamaa kabeba deki na mwenzake king'amuzi! Hapo wakaanza kuzuga na kuniambia "hapa una connect vipi mdogo wangu tucheck movie?" Mpango wao ukafa.
Huyu jamaa hakuna aliyempenda wala kumtaka aje pale nyumbani ila hakuna wa kumfukuza maana pale panamuhusu ni kwa babu yake pia na mama yake mzazi yupo pale na babu ameshafariki.
Mimi ki upande wangu ilikuwa ni mdogo kwake na amenizidi sana umri, aliniheshimu na niliheshimika pia kulingana na kazi yangu kwenye jamii, hivyo niliposikia au kumuona amekuja pale nilikuwa siendi haswa baada ya kushamiri matendo yake ya ajabu.
Muda wote ana panga kiunoni au sime, ni jitu limepanda na genge lake lote katika wezi wa mji walimuita master maana hata wakiishiwa mipango, jamaa akiingia yeye basi ujue hela ndefu inapatikana muda mfupi kiasi cha kuzunguka tu na kumwambia mtu una matatizo na akitema mate ni nywele, na kuchukua vitu vyake vyote kwa hiyari kabisa.
Siku moja nilikwenda kwa mama pale na ndugu zangu tumekaa tunasubiria tuuone mwaka mpya na kipindi hicho jamaa hajaonekana zaidi ya miezi sita na tukajua yuko jela, kwani alikuwa akishikwa hamwambii mtu, kesi anafuatilia peke yake mpaka anafungwa na akitoka halaumu mtu wala hana nongwa na ndugu.
Basi ile tumekaa nje kama saa sita kasoro ghafla jamaa akaletwa na Defender na Askari kama nane wakiwa na bunduki, mabomu na marungu na kuambiwa aingie ndani aonyeshe mzigo alioiba jana yake katika duka walilovunja! Ghafla pale pale kuna jamaa mwenye kitambi nilikuja kugundua ndiye mwenye duka, akaropoka "hawa wawili pia walikuwepo tena walikuwa wananirushia mawe!"
Hapo akimaanisha mimi na ndugu yangu wa kiume ambae alikuja likizo!
"Simama juu" ilikuwa ni amri ya Afande mmoja wapo na tukachukuliwa moja kwa moja mpaka kituoni saba usiku.
Nikamtonya Askari mmoja wapo kuwa sisi hatuhusiki na mimi ni mtu na shughuli zangu za maana na dogo ni mwanafunzi, akasema ile ni oda hivyo ameikamilisha nisubiri wakuu niwaeleze asubuhi.
Mle ndani hewa ilikuwa nzito, chumba kidogo na kidirisha kipo juu sana na kidogo mno, nilijawa na mawazo na kufikiria najitoaje pale katika jambo zito kama hilo, na muda huo huo naisikia Radio Call toka kwa Afande inasema, ile kesi ya ujambazi wa kuvunja duka, tumekamata majambazi watatu bado wanne ovaaa!!!
Muda wote Bro kalala chini kwenye sakafu yenye mikojo bila wasi wasi wowote, akisema, mkiulizwa acheni kubisha bisha mambo yatachelewa, semeni tumechukua mzigo ili tukapumzike miezi sita tutarudi uraiani.
Inafika saa nani usiku akaletwa jamaa ambae kamtorosha binti wa Traffic, jamaa alipigwa sana mpaka akatupaka damu mle ndani na kutuaga kuwa anakufa...



Ndo nusu nusuTayari pia.
ndo imeishaInaendelea....
Bro alisema tumemuuza maana tumefufua mambo mazito sana hivyo tutashika adabu mule ndani, hakika giza likatanda tena katika akili yangu maana njia niliyodhani itakuwa msaada haikusaidia na badala yake imeleta matatizo zaidi...wakati nikiwaza na kuwazua na huku jamaa akilia pale chini huku kashikilia ubavu mara ghafla akaingia Afande na kutupeleka ubaoni mimi na mdogo wangu.
Tulipofika hapo tukakutana na baba mdogo pamoja na jamaa aliyeibiwa, kumbe aliyeibiwa anatujua vizuri tu tuliishi mtaa mmoja miaka ya nyuma na kupoteana katika harakati za maisha, hivyo akatuomba msamaha kuwa tumsamehe hakujua kama ni sisi, na kwamba anatufahamu tangu ni wadogo hatuna mambo ya ajabu.
Hapo tukapewa nguo zetu na vitu vyetu kama vile mikanda ya suruali na pochi na tuaachiwa kwa maagizo kwamba tukihitajika muda wowote tutaitwa.
Wakati tukivaa vaa vitu vyetu pale nje tulishuhudia karandinga likiingia na kuzungushwa kwa mbwembwe nyingi na kisha likabeba watuhumiwa akiwemo Brother na likaondoka kwa speed kuelekea mahakamani.
Mpaka muda huo tukamshukuru Mungu na kurudi nyumbani japokuwa tulitaniwa kuwa tumekonda kwa usiku mmoja tu, lakini kwetu cha muhimu ni kutoka kule maana ni balaa unapohusishwa katika jambo zito usilolijua mwanzo wala mwisho.
Muda ulipita na jamaa hakupewa dhamana hivyo alikaa mahabusu na hatimae akafungwa ingawa hatukujua alihukumiwa miaka mingapi, ila tu hakutaja wenzake hata mmoja.
Miaka ikakatika kwa amani kabisa ila jioni moja tukashangaa jamaa akaja pale kwa kina mama nyumbani, alikuja akiwa na wenzake kama saba akiwemo mwanamke mmoja ambae pia alionyesha ni hao hao tu, aliniulizia akaambiwa yupo kwake hivyo akachukua genge lake na kuja moja kwa moja kwangu!
Nilipomuona nikajua ohoo yale ya polisi yamekuja kulipiwa kisasi, ila cha ajabu tulisalimiana vizuri kabisa na akasema "mdogo wangu vitu vidogo vile unambwela na kuanza kutiririka mafaili kwa wajinga wajinga, mambo ya kawaida tu ya kwa mwanaume" kisha wenzake wakaunga mkono kuwa kule ni sehemu ya kupangia mipango na ku refresh akili tu hivyo nimeharibu kwa master.
Wakaondoka na kuelekea kule kwenye nyumba ya familia tena, na hapo wakaanza kufungua mabegi waliyokuja nayo na kuanza kugawana mali za wizi bila shaka, na ni wazi kwamba jamaa huenda alitoka muda kidogo na alikuwa akifanya mambo yake na jamaa zake kama kawaida.
Waligawana pesa vibunda, simu na jamaa akampa yule demu cheni nzito ya dhahabu avae, kumbe ni mpenzi wake.
Mama mdogo mwenye mtoto huyo ambae ni mwizi ndiye anaeulea ubovu wote hataki mwanawe asemwe, anasema aachwe kila mtu na majaliwa yake.
Hivyo safari hii jamaa akamuacha demu wake akae pale na mama mkwe na jamaa na genge lake wakasepa maana hakai pale na anapokaa hapajulikani anafanya kuja tu kama mvua.
Bi. Mdogo alikatiwa kibunda hivyo akampokea mkwe na kuona maisha ndiyo haya.
Baada ya siku tatu tu jamaa akaibuka na kumwambia yule demu wake ampe ile cheni akauze kwani hana hata mia, demu akakataa na kusema juzi tu ulikuwa na laki tisa zimekwenda wapi?
Ugomvi ukawa mkubwa jamaa akatoa panga na mke akakimbilia shoka ili zipigwe, ila kwa bahati nzuri wahuni wenzake nao wakaingia na kuongea na shemeji yao vizuri wakapewa cheni na kuondoka.
Katika kipindi ambacho jamaa yupo jela, nilianzisha mfugo wa mbuzi watano na niliwajengea banda pale pale kwa mama na walinawiri na wawili walikuwa na mimba.
Sasa baada ya kupita mkasa wa cheni kama wiki hivi usiku nimelala kwangu nikaota mbuzi wanaibiwa na watu wawili ambao nawajua ni huyo Bro na rafiki ya mwizi mwizi vidole baadhi pia vimekatwa.
Nikashtuka nikataka nitoke niende kule nikaangalie mbuzi ila nikaona ni ndoto tu nikalala, nikakurupuka ni saa kumi na mbili kasoro nikatoka haraka kwenda kuangalia mbuzi, ajabu kufika banda lipo wazi hakuna mbuzi zaidi ya mistari tu ya miburuzo ya kamba, nikaona leo yamenifika.
Nikachukua pikipiki na kwenda sehemu kadhaa za machinjio bila mafanikio ila sehemu ya mwisho nilikuta wamesha chinjwa nimejua hilo kwa sababu ngozi zao zina michoro maana niliwanunua kwa Wamasai na nimezikuta hapo.
Sikutaka kufanya vurugu wala kumshitaki mtu hivyo nilirudi nyumbani maana nilipanga kumshitakia Mungu anipe majibu kwa maadui zangu wa jambo hilo.
Niliomba Mungu nijuavyo mimi (sio uchawi ni kufunga na kumlilia Mungu) na baada ya wiki moja asubuhi, yule rafiki yake bro aliiba simu kwa dada mmoja na kumuwekea kisu shingoni, raia wakamuona na kumpiga mpaka wakamuua.
Siku tatu mbele Bro aliingia kwenye maduka ya wachaga mchana wa saa nane na kuiba fuko moja la ile mifuko myeusi ya nylon iliyopigwa marufuku siku hizi, jamaa kala vitu vyake jicho nyanya akaona haonekani kumbe wenzake wamemuona wanamlia tyming tu, ile kuzama dukani kutoka jamaa wakamzunguka na hapo ukumbuke ni mjini kwenye lami hakuna mawe, hivyo wenye maduka walikuja na mapanga na kumkata kata huku akilia kwa uchungu na kusema hataiba tena, lakini wapi alikuwa amechelewa!
Polisi waliwahi lakini walipoona ni yeye walichoka nae hivyo waliondoka na kuomba wananchi wamalize kazi na ikawa hivyo, akaaga dunia jamaa.
Kizaaa zaa ni siku ya mazishi, ndugu hatukubeba jeneza lake kwani lilibebwa na wahuni kutoka kila pande na walifurika sana, huyu ana sikio moja, huyu jicho moja huku yule ana mguu mmoja basi ilikuwa ni balaa.
Kufika kaburini baada ya kuzika ikabidi Sheikh atoe mawaidha "ndugu zangu maisha ni mafupi hivyo tuishi kwa wema, ona ndugu yetu huyu amekufa katika mazingira magumu ya dhambi..." ghafla Sheikh akapigwa ngumi moja tu ya kichwa na jamaa mmojawapo na akasema "wewe mbwa una msimanga master!!?" Hakuna aliyetarajia jambo hili...
Hatari sana." ghafla Sheikh akapigwa ngumi moja tu ya kichwa na jamaa mmojawapo na akasema "wewe mbwa una msimanga master!!?" Hakuna aliyetarajia jambo hili...
Muda wote Bro kalala chini kwenye sakafu yenye mikojo bila wasi wasi wowote, akisema, mkiulizwa acheni kubisha bisha mambo yatachelewa, semeni tumechukua mzigo ili tukapumzike miezi sita tutarudi uraiani.Salaam
Leo nimekumbuka kisa cha ndugu yetu mwizi (kaka yangu mtoto wa mama mdogo) ambae alikuwa ameiva kwenye wizi hasa wa kutumia uchawi na mbinu kali za kitapeli.
Nyakati hizo nilikuwa naishi karibu kabisa na nyumba ya familia ya Babu mzaa mama, na mama yangu pamoja na ndugu zake walikuwa wanaishi hapo kwa baba yao.
Huyu kaka yangu alikuwa hajulikani anapoishi ila akiharibu anakuja hapo kwa mama zake kujificha mpaka mambo yatulie, ni mara nyingi amefungwa na kuachiwa, kupigwa na kuja hoi pale nyumbani na wahuni wenzake ambao walimuuguza kwa mitishamba na kumchua kwa majani ya mnyono mpaka atakapopona kwani waliogopa kwenda hospital.
Kuna siku nilifika pale nyumbani nikawakuta na wenzake kama sita hivi juu ya meza wamewasha mshumaa wanatumia madawa ya kulevya, baada ya salamu wakasema dah! Tuna majonzi sana, tumekwenda kuchukua mali mahali ila msala jamaa zetu watatu wale ambao tuliwahi kuja nao hapa...imekuwa bahati mbaya wamechomwa moto!
Jamaa wakisema hivyo huku wanapata vitu vyao kama hakujatokea kitu na wakipumzika siku mbili ujue wanaingia kazini tena.
Mimi binafsi nilishamkuta kwenye pikipiki yangu kubwa akiikata waya ili aiibe, na pia kuna siku niliingia nyumbani kwangu ile kuangalia Tv nikapitiwa na usingizi ilikuwa kama tano usiku, kushtuka nakuta jamaa kabeba deki na mwenzake king'amuzi! Hapo wakaanza kuzuga na kuniambia "hapa una connect vipi mdogo wangu tucheck movie?" Mpango wao ukafa.
Huyu jamaa hakuna aliyempenda wala kumtaka aje pale nyumbani ila hakuna wa kumfukuza maana pale panamuhusu ni kwa babu yake pia na mama yake mzazi yupo pale na babu ameshafariki.
Mimi ki upande wangu ilikuwa ni mdogo kwake na amenizidi sana umri, aliniheshimu na niliheshimika pia kulingana na kazi yangu kwenye jamii, hivyo niliposikia au kumuona amekuja pale nilikuwa siendi haswa baada ya kushamiri matendo yake ya ajabu.
Muda wote ana panga kiunoni au sime, ni jitu limepanda na genge lake lote katika wezi wa mji walimuita master maana hata wakiishiwa mipango, jamaa akiingia yeye basi ujue hela ndefu inapatikana muda mfupi kiasi cha kuzunguka tu na kumwambia mtu una matatizo na akitema mate ni nywele, na kuchukua vitu vyake vyote kwa hiyari kabisa.
Siku moja nilikwenda kwa mama pale na ndugu zangu tumekaa tunasubiria tuuone mwaka mpya na kipindi hicho jamaa hajaonekana zaidi ya miezi sita na tukajua yuko jela, kwani alikuwa akishikwa hamwambii mtu, kesi anafuatilia peke yake mpaka anafungwa na akitoka halaumu mtu wala hana nongwa na ndugu.
Basi ile tumekaa nje kama saa sita kasoro ghafla jamaa akaletwa na Defender na Askari kama nane wakiwa na bunduki, mabomu na marungu na kuambiwa aingie ndani aonyeshe mzigo alioiba jana yake katika duka walilovunja! Ghafla pale pale kuna jamaa mwenye kitambi nilikuja kugundua ndiye mwenye duka, akaropoka "hawa wawili pia walikuwepo tena walikuwa wananirushia mawe!"
Hapo akimaanisha mimi na ndugu yangu wa kiume ambae alikuja likizo!
"Simama juu" ilikuwa ni amri ya Afande mmoja wapo na tukachukuliwa moja kwa moja mpaka kituoni saba usiku.
Nikamtonya Askari mmoja wapo kuwa sisi hatuhusiki na mimi ni mtu na shughuli zangu za maana na dogo ni mwanafunzi, akasema ile ni oda hivyo ameikamilisha nisubiri wakuu niwaeleze asubuhi.
Mle ndani hewa ilikuwa nzito, chumba kidogo na kidirisha kipo juu sana na kidogo mno, nilijawa na mawazo na kufikiria najitoaje pale katika jambo zito kama hilo, na muda huo huo naisikia Radio Call toka kwa Afande inasema, ile kesi ya ujambazi wa kuvunja duka, tumekamata majambazi watatu bado wanne ovaaa!!!
Muda wote Bro kalala chini kwenye sakafu yenye mikojo bila wasi wasi wowote, akisema, mkiulizwa acheni kubisha bisha mambo yatachelewa, semeni tumechukua mzigo ili tukapumzike miezi sita tutarudi uraiani.
Inafika saa nani usiku akaletwa jamaa ambae kamtorosha binti wa Traffic, jamaa alipigwa sana mpaka akatupaka damu mle ndani na kutuaga kuwa anakufa...

Kizaaa zaa ni siku ya mazishi, ndugu hatukubeba jeneza lake kwani lilibebwa na wahuni kutoka kila pande na walifurika sana, huyu ana sikio moja, huyu jicho moja huku yule ana mguu mmoja basi ilikuwa ni balaa.Inaendelea....
Bro alisema tumemuuza maana tumefufua mambo mazito sana hivyo tutashika adabu mule ndani, hakika giza likatanda tena katika akili yangu maana njia niliyodhani itakuwa msaada haikusaidia na badala yake imeleta matatizo zaidi...wakati nikiwaza na kuwazua na huku jamaa akilia pale chini huku kashikilia ubavu mara ghafla akaingia Afande na kutupeleka ubaoni mimi na mdogo wangu.
Tulipofika hapo tukakutana na baba mdogo pamoja na jamaa aliyeibiwa, kumbe aliyeibiwa anatujua vizuri tu tuliishi mtaa mmoja miaka ya nyuma na kupoteana katika harakati za maisha, hivyo akatuomba msamaha kuwa tumsamehe hakujua kama ni sisi, na kwamba anatufahamu tangu ni wadogo hatuna mambo ya ajabu.
Hapo tukapewa nguo zetu na vitu vyetu kama vile mikanda ya suruali na pochi na tuaachiwa kwa maagizo kwamba tukihitajika muda wowote tutaitwa.
Wakati tukivaa vaa vitu vyetu pale nje tulishuhudia karandinga likiingia na kuzungushwa kwa mbwembwe nyingi na kisha likabeba watuhumiwa akiwemo Brother na likaondoka kwa speed kuelekea mahakamani.
Mpaka muda huo tukamshukuru Mungu na kurudi nyumbani japokuwa tulitaniwa kuwa tumekonda kwa usiku mmoja tu, lakini kwetu cha muhimu ni kutoka kule maana ni balaa unapohusishwa katika jambo zito usilolijua mwanzo wala mwisho.
Muda ulipita na jamaa hakupewa dhamana hivyo alikaa mahabusu na hatimae akafungwa ingawa hatukujua alihukumiwa miaka mingapi, ila tu hakutaja wenzake hata mmoja.
Miaka ikakatika kwa amani kabisa ila jioni moja tukashangaa jamaa akaja pale kwa kina mama nyumbani, alikuja akiwa na wenzake kama saba akiwemo mwanamke mmoja ambae pia alionyesha ni hao hao tu, aliniulizia akaambiwa yupo kwake hivyo akachukua genge lake na kuja moja kwa moja kwangu!
Nilipomuona nikajua ohoo yale ya polisi yamekuja kulipiwa kisasi, ila cha ajabu tulisalimiana vizuri kabisa na akasema "mdogo wangu vitu vidogo vile unambwela na kuanza kutiririka mafaili kwa wajinga wajinga, mambo ya kawaida tu ya kwa mwanaume" kisha wenzake wakaunga mkono kuwa kule ni sehemu ya kupangia mipango na ku refresh akili tu hivyo nimeharibu kwa master.
Wakaondoka na kuelekea kule kwenye nyumba ya familia tena, na hapo wakaanza kufungua mabegi waliyokuja nayo na kuanza kugawana mali za wizi bila shaka, na ni wazi kwamba jamaa huenda alitoka muda kidogo na alikuwa akifanya mambo yake na jamaa zake kama kawaida.
Waligawana pesa vibunda, simu na jamaa akampa yule demu cheni nzito ya dhahabu avae, kumbe ni mpenzi wake.
Mama mdogo mwenye mtoto huyo ambae ni mwizi ndiye anaeulea ubovu wote hataki mwanawe asemwe, anasema aachwe kila mtu na majaliwa yake.
Hivyo safari hii jamaa akamuacha demu wake akae pale na mama mkwe na jamaa na genge lake wakasepa maana hakai pale na anapokaa hapajulikani anafanya kuja tu kama mvua.
Bi. Mdogo alikatiwa kibunda hivyo akampokea mkwe na kuona maisha ndiyo haya.
Baada ya siku tatu tu jamaa akaibuka na kumwambia yule demu wake ampe ile cheni akauze kwani hana hata mia, demu akakataa na kusema juzi tu ulikuwa na laki tisa zimekwenda wapi?
Ugomvi ukawa mkubwa jamaa akatoa panga na mke akakimbilia shoka ili zipigwe, ila kwa bahati nzuri wahuni wenzake nao wakaingia na kuongea na shemeji yao vizuri wakapewa cheni na kuondoka.
Katika kipindi ambacho jamaa yupo jela, nilianzisha mfugo wa mbuzi watano na niliwajengea banda pale pale kwa mama na walinawiri na wawili walikuwa na mimba.
Sasa baada ya kupita mkasa wa cheni kama wiki hivi usiku nimelala kwangu nikaota mbuzi wanaibiwa na watu wawili ambao nawajua ni huyo Bro na rafiki ya mwizi mwizi vidole baadhi pia vimekatwa.
Nikashtuka nikataka nitoke niende kule nikaangalie mbuzi ila nikaona ni ndoto tu nikalala, nikakurupuka ni saa kumi na mbili kasoro nikatoka haraka kwenda kuangalia mbuzi, ajabu kufika banda lipo wazi hakuna mbuzi zaidi ya mistari tu ya miburuzo ya kamba, nikaona leo yamenifika.
Nikachukua pikipiki na kwenda sehemu kadhaa za machinjio bila mafanikio ila sehemu ya mwisho nilikuta wamesha chinjwa nimejua hilo kwa sababu ngozi zao zina michoro maana niliwanunua kwa Wamasai na nimezikuta hapo.
Sikutaka kufanya vurugu wala kumshitaki mtu hivyo nilirudi nyumbani maana nilipanga kumshitakia Mungu anipe majibu kwa maadui zangu wa jambo hilo.
Niliomba Mungu nijuavyo mimi (sio uchawi ni kufunga na kumlilia Mungu) na baada ya wiki moja asubuhi, yule rafiki yake bro aliiba simu kwa dada mmoja na kumuwekea kisu shingoni, raia wakamuona na kumpiga mpaka wakamuua.
Siku tatu mbele Bro aliingia kwenye maduka ya wachaga mchana wa saa nane na kuiba fuko moja la ile mifuko myeusi ya nylon iliyopigwa marufuku siku hizi, jamaa kala vitu vyake jicho nyanya akaona haonekani kumbe wenzake wamemuona wanamlia tyming tu, ile kuzama dukani kutoka jamaa wakamzunguka na hapo ukumbuke ni mjini kwenye lami hakuna mawe, hivyo wenye maduka walikuja na mapanga na kumkata kata huku akilia kwa uchungu na kusema hataiba tena, lakini wapi alikuwa amechelewa!
Polisi waliwahi lakini walipoona ni yeye walichoka nae hivyo waliondoka na kuomba wananchi wamalize kazi na ikawa hivyo, akaaga dunia jamaa.
Kizaaa zaa ni siku ya mazishi, ndugu hatukubeba jeneza lake kwani lilibebwa na wahuni kutoka kila pande na walifurika sana, huyu ana sikio moja, huyu jicho moja huku yule ana mguu mmoja basi ilikuwa ni balaa.
Kufika kaburini baada ya kuzika ikabidi Sheikh atoe mawaidha "ndugu zangu maisha ni mafupi hivyo tuishi kwa wema, ona ndugu yetu huyu amekufa katika mazingira magumu ya dhambi..." ghafla Sheikh akapigwa ngumi moja tu ya kichwa na jamaa mmojawapo na akasema "wewe mbwa una msimanga master!!?" Hakuna aliyetarajia jambo hili...

Maombi ni silaha tosha funzo kubwa.Inaendelea....
Bro alisema tumemuuza maana tumefufua mambo mazito sana hivyo tutashika adabu mule ndani, hakika giza likatanda tena katika akili yangu maana njia niliyodhani itakuwa msaada haikusaidia na badala yake imeleta matatizo zaidi...wakati nikiwaza na kuwazua na huku jamaa akilia pale chini huku kashikilia ubavu mara ghafla akaingia Afande na kutupeleka ubaoni mimi na mdogo wangu.
Tulipofika hapo tukakutana na baba mdogo pamoja na jamaa aliyeibiwa, kumbe aliyeibiwa anatujua vizuri tu tuliishi mtaa mmoja miaka ya nyuma na kupoteana katika harakati za maisha, hivyo akatuomba msamaha kuwa tumsamehe hakujua kama ni sisi, na kwamba anatufahamu tangu ni wadogo hatuna mambo ya ajabu.
Hapo tukapewa nguo zetu na vitu vyetu kama vile mikanda ya suruali na pochi na tuaachiwa kwa maagizo kwamba tukihitajika muda wowote tutaitwa.
Wakati tukivaa vaa vitu vyetu pale nje tulishuhudia karandinga likiingia na kuzungushwa kwa mbwembwe nyingi na kisha likabeba watuhumiwa akiwemo Brother na likaondoka kwa speed kuelekea mahakamani.
Mpaka muda huo tukamshukuru Mungu na kurudi nyumbani japokuwa tulitaniwa kuwa tumekonda kwa usiku mmoja tu, lakini kwetu cha muhimu ni kutoka kule maana ni balaa unapohusishwa katika jambo zito usilolijua mwanzo wala mwisho.
Muda ulipita na jamaa hakupewa dhamana hivyo alikaa mahabusu na hatimae akafungwa ingawa hatukujua alihukumiwa miaka mingapi, ila tu hakutaja wenzake hata mmoja.
Miaka ikakatika kwa amani kabisa ila jioni moja tukashangaa jamaa akaja pale kwa kina mama nyumbani, alikuja akiwa na wenzake kama saba akiwemo mwanamke mmoja ambae pia alionyesha ni hao hao tu, aliniulizia akaambiwa yupo kwake hivyo akachukua genge lake na kuja moja kwa moja kwangu!
Nilipomuona nikajua ohoo yale ya polisi yamekuja kulipiwa kisasi, ila cha ajabu tulisalimiana vizuri kabisa na akasema "mdogo wangu vitu vidogo vile unambwela na kuanza kutiririka mafaili kwa wajinga wajinga, mambo ya kawaida tu ya kwa mwanaume" kisha wenzake wakaunga mkono kuwa kule ni sehemu ya kupangia mipango na ku refresh akili tu hivyo nimeharibu kwa master.
Wakaondoka na kuelekea kule kwenye nyumba ya familia tena, na hapo wakaanza kufungua mabegi waliyokuja nayo na kuanza kugawana mali za wizi bila shaka, na ni wazi kwamba jamaa huenda alitoka muda kidogo na alikuwa akifanya mambo yake na jamaa zake kama kawaida.
Waligawana pesa vibunda, simu na jamaa akampa yule demu cheni nzito ya dhahabu avae, kumbe ni mpenzi wake.
Mama mdogo mwenye mtoto huyo ambae ni mwizi ndiye anaeulea ubovu wote hataki mwanawe asemwe, anasema aachwe kila mtu na majaliwa yake.
Hivyo safari hii jamaa akamuacha demu wake akae pale na mama mkwe na jamaa na genge lake wakasepa maana hakai pale na anapokaa hapajulikani anafanya kuja tu kama mvua.
Bi. Mdogo alikatiwa kibunda hivyo akampokea mkwe na kuona maisha ndiyo haya.
Baada ya siku tatu tu jamaa akaibuka na kumwambia yule demu wake ampe ile cheni akauze kwani hana hata mia, demu akakataa na kusema juzi tu ulikuwa na laki tisa zimekwenda wapi?
Ugomvi ukawa mkubwa jamaa akatoa panga na mke akakimbilia shoka ili zipigwe, ila kwa bahati nzuri wahuni wenzake nao wakaingia na kuongea na shemeji yao vizuri wakapewa cheni na kuondoka.
Katika kipindi ambacho jamaa yupo jela, nilianzisha mfugo wa mbuzi watano na niliwajengea banda pale pale kwa mama na walinawiri na wawili walikuwa na mimba.
Sasa baada ya kupita mkasa wa cheni kama wiki hivi usiku nimelala kwangu nikaota mbuzi wanaibiwa na watu wawili ambao nawajua ni huyo Bro na rafiki ya mwizi mwizi vidole baadhi pia vimekatwa.
Nikashtuka nikataka nitoke niende kule nikaangalie mbuzi ila nikaona ni ndoto tu nikalala, nikakurupuka ni saa kumi na mbili kasoro nikatoka haraka kwenda kuangalia mbuzi, ajabu kufika banda lipo wazi hakuna mbuzi zaidi ya mistari tu ya miburuzo ya kamba, nikaona leo yamenifika.
Nikachukua pikipiki na kwenda sehemu kadhaa za machinjio bila mafanikio ila sehemu ya mwisho nilikuta wamesha chinjwa nimejua hilo kwa sababu ngozi zao zina michoro maana niliwanunua kwa Wamasai na nimezikuta hapo.
Sikutaka kufanya vurugu wala kumshitaki mtu hivyo nilirudi nyumbani maana nilipanga kumshitakia Mungu anipe majibu kwa maadui zangu wa jambo hilo.
Niliomba Mungu nijuavyo mimi (sio uchawi ni kufunga na kumlilia Mungu) na baada ya wiki moja asubuhi, yule rafiki yake bro aliiba simu kwa dada mmoja na kumuwekea kisu shingoni, raia wakamuona na kumpiga mpaka wakamuua.
Siku tatu mbele Bro aliingia kwenye maduka ya wachaga mchana wa saa nane na kuiba fuko moja la ile mifuko myeusi ya nylon iliyopigwa marufuku siku hizi, jamaa kala vitu vyake jicho nyanya akaona haonekani kumbe wenzake wamemuona wanamlia tyming tu, ile kuzama dukani kutoka jamaa wakamzunguka na hapo ukumbuke ni mjini kwenye lami hakuna mawe, hivyo wenye maduka walikuja na mapanga na kumkata kata huku akilia kwa uchungu na kusema hataiba tena, lakini wapi alikuwa amechelewa!
Polisi waliwahi lakini walipoona ni yeye walichoka nae hivyo waliondoka na kuomba wananchi wamalize kazi na ikawa hivyo, akaaga dunia jamaa.
Kizaaa zaa ni siku ya mazishi, ndugu hatukubeba jeneza lake kwani lilibebwa na wahuni kutoka kila pande na walifurika sana, huyu ana sikio moja, huyu jicho moja huku yule ana mguu mmoja basi ilikuwa ni balaa.
Kufika kaburini baada ya kuzika ikabidi Sheikh atoe mawaidha "ndugu zangu maisha ni mafupi hivyo tuishi kwa wema, ona ndugu yetu huyu amekufa katika mazingira magumu ya dhambi..." ghafla Sheikh akapigwa ngumi moja tu ya kichwa na jamaa mmojawapo na akasema "wewe mbwa una msimanga master!!?" Hakuna aliyetarajia jambo hili...