Bado kuwaachia mashehe wa Kiislamu tu, sasa tunaona CCM wanajitahidi kuweka na kuziba au kutia viraka sehemu zao,mara walimu, mara pembejeo, mara afya, mara 'ishuwarensi'. Yaani wanahangaika na kurusha madaluga vibaya sana. Walikuwa wapi tokea tupate Uhuru, walikuwa wapi miaka mitano iliyopita?
Hivi ni nani kawakurupusha, je ni wapinzani? Hapana ni wananchi; wananchi wameamka na wanatamka waziwazi sio kuwa hawampendi Magufuli, hapana wanampenda sana ila mahali alipo wananchi hawapo. Wananchi hawaitaki CCM hata kuiona, wameteseka wanaendelea kuteseka na haitokaa sawa milele hata mashehe na mapadire wanapokuwepo CCM huwa na roho mbaya sana ni hatari.
CCM imepoteza muelekeo, hili halitaki tochi kuliona. Sasa sasa ni wakati muafaka CCM inaondoka mdomo wazi.
Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali
Kavimba yote mapaja na kutetemeka mwili
Kwaheli CCM, ni kweli umetoka mbali
Hivi ni nani kawakurupusha, je ni wapinzani? Hapana ni wananchi; wananchi wameamka na wanatamka waziwazi sio kuwa hawampendi Magufuli, hapana wanampenda sana ila mahali alipo wananchi hawapo. Wananchi hawaitaki CCM hata kuiona, wameteseka wanaendelea kuteseka na haitokaa sawa milele hata mashehe na mapadire wanapokuwepo CCM huwa na roho mbaya sana ni hatari.
CCM imepoteza muelekeo, hili halitaki tochi kuliona. Sasa sasa ni wakati muafaka CCM inaondoka mdomo wazi.
Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali
Kavimba yote mapaja na kutetemeka mwili
Kwaheli CCM, ni kweli umetoka mbali