Nini tofauti ya msomi na asiye msomi?

Nini tofauti ya msomi na asiye msomi?

ShesRise_1

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2025
Posts
17,456
Reaction score
41,378
Kuna jambo huwa linanichanganya sanašŸ¤”

Je, elimu imekuongezea akili au imekuondolea upumbavu?

Kwa sababu nimeona watu wenye elimu za juu sana, vyeti vingi na majina marefu, lakini baadhi ya maamuzi yao yanakufanya ujiulize kama kweli elimu peke yake inatosha kumfanya mtu awe na akili

Unakuta mtu ni kiongozi ameshika nyadhifa mbali mbali ila ukitazama maamuzi yake unabaki na alama ya mshangao heh huyu si ni msomi?

Unajiuliza huyu elimu haikua na msaada kwake ?

Mbona anaamua,anaongea kama mjinga?


Wakati huo huo unakutana na mtu ambaye hakusoma sana au hakupata nafasi ya kusoma kabisa, lakini ana uwezo mkubwa wa kufikiri, kutatua matatizo na kuona mambo kwa upeo mpana kuliko hata baadhi ya wasomi

Hapo ndipo nikajiuliza, ni nini hasa kinachomfanya mtu aitwe genius na ni nini kinachomfanya aonekane mpumbavu?

Je, ni kiwango cha elimu?
Je, ni uwezo wa kufikiri?
Je, ni maamuzi anayofanya kila siku?
Au ni namna anavyojifunza kutokana na makosa yake?

Kwa mtazamo wangu, elimu inaweza kuongeza maarifa, lakini si lazima iondoe upumbavu

Maana kuna wasomi wapumbavu(hapa nisamehewe)

Na kutosoma sana si lazima kumfanye mtu akose akili

Wewe unaonaje?
Tofauti ya mtu mwenye akili nyingi na mpumbavu unaiona wapi?
Na elimu imekusaidia nini hasa kwenye hilo?

Chombezo( ni kua hata wapumbavu huzeeka)

ShesRise_1 🤚

It's Furahi deiiiiiišŸ’ƒ
 
Shida ni kwamba neno "genius" halina maana moja. Linaweza kumaanisha ubunifu, uvumbuzi au hata kuwa na kipaji maalum.

Inapendeza zaidi ukibainisha, labda genius wa muziki, genius wa hisabati nk.

Tambua kwamba hakuna mtu aliye bora kwenye kila kitu. Lazima kuna mahali utapelea. Huu ni ubinadamu, uwe ni genius ama sio.
 
Kwa hiyo msomi anaweza kua mjinga pamoja na kua ni msomi?
Kwa sababu
Mjinga akishaambiwa inakwisha
Ujinga ni kutojua (inamaana gani?)
Maana haujui lilifanyika nini?
Sasa ukielezwa ujinga wako unakwisha
Now you know!

Ujinga ni Ignorance mmh
Hujui maana yake ni nini au nini kilifanyika au inafanyika vipi au inakuajekuaje? Ukishajua wewe sio mjinga tena

Upumbavu ni Foolishness
Foolishness ni kitu cha kipuuzi ni kitu kisichokua na maana yoyote ni upuuzi upuuzi tu

Ukiambiwa unafanya upumbavu au wewe ni pumbavu maana yake unafanya upuuzi au unafanya vitu ambavyo havina maana yoyote kwa watu wanaokuzunguka
 
Shida ni kwamba neno "genius" halina maana moja. Linaweza kumaanisha ubunifu, uvumbuzi au hata kuwa na kipaji maalum.

Inapendeza zaidi ukibainisha, labda genius wa muziki, genius wa hisabati nk.

Tambua kwamba hakuna mtu aliye bora kwenye kila kitu. Lazima kuna mahali utapelea. Huu ni ubinadamu, uwe ni genius ama sio.
Labda nimekosea kuwasilisha ila maana yangu ni kwamba mara nyingi tunaambiwa nenda shule uondoe upumbavu kicwani au uondoe ujinga

Sasa ndio maana nikauliza mbona baado kuna wasomi wengi tena elimu za juu lakini bado wanaonekana maamuzi yao ni kama ile elimu waliyoipata haikuondoa huo ujinga au upumbavu?
 
Kuna jambo huwa linanichanganya sanašŸ¤”

Je, elimu imekuongezea akili au imekuondolea upumbavu?

Kwa sababu nimeona watu wenye elimu za juu sana, vyeti vingi na majina marefu, lakini baadhi ya maamuzi yao yanakufanya ujiulize kama kweli elimu peke yake inatosha kumfanya mtu awe na akili

Unakuta mtu ni kiongozi ameshika nyadhifa mbali mbali ila ukitazama maamuzi yake unabaki na alama ya mshangao heh huyu si ni msomi?

Unajiuliza huyu elimu haikua na msaada kwake ?

Mbona anaamua,anaongea kama mjinga?


Wakati huo huo unakutana na mtu ambaye hakusoma sana au hakupata nafasi ya kusoma kabisa, lakini ana uwezo mkubwa wa kufikiri, kutatua matatizo na kuona mambo kwa upeo mpana kuliko hata baadhi ya wasomi

Hapo ndipo nikajiuliza, ni nini hasa kinachomfanya mtu aitwe genius na ni nini kinachomfanya aonekane mpumbavu?

Je, ni kiwango cha elimu?
Je, ni uwezo wa kufikiri?
Je, ni maamuzi anayofanya kila siku?
Au ni namna anavyojifunza kutokana na makosa yake?

Kwa mtazamo wangu, elimu inaweza kuongeza maarifa, lakini si lazima iondoe upumbavu

Maana kuna wasomi wapumbavu(hapa nisamehewe)

Na kutosoma sana si lazima kumfanye mtu akose akili

Wewe unaonaje?
Tofauti ya mtu mwenye akili nyingi na mpumbavu unaiona wapi?
Na elimu imekusaidia nini hasa kwenye hilo?

Chombezo( ni kua hata wapumbavu huzeeka)

ShesRise_1 🤚

It's Furahi deiiiiiišŸ’ƒ
You can be a professor but still "an adiot "
 
Werevu ni wa kuzaliwa nao kama ilivyo upumbavu.

Mwerevu hata asipoenda shule hubaki kuwa mwerevu, mpumbavu hata akiwa na vyeti vingi na majina marefu kama ulivyoanisha bado ataendelea kuwa mpumbavu hata akivaa suti na tai.

Msukuma, Kishimba, Mnyika huenda wanazo za kuzaliwa kuliko wale wapumbavu uliowatunzia heshima kwa kuficha majina yao.
 
Kwa sababu
Mjinga akishaambiwa inakwisha
Ujinga ni kutojua (inamaana gani?)
Maana haujui lilifanyika nini?
Sasa ukielezwa ujinga wako unakwisha
Now you know!

Ujinga ni Ignorance mmh
Hujui maana yake ni nini au nini kilifanyika au inafanyika vipi au inakuajekuaje? Ukishajua wewe sio mjinga tena
Ujinga ni kutokojua jambo Fulani ukishajua ujinga umeishašŸ‘
Upumbavu ni Foolishness
Foolishness ni kitu cha kipuuzi ni kitu kisichokua na maana yoyote ni upuuzi upuuzi tu

Ukiambiwa unafanya upumbavu au wewe ni pumbavu maana yake unafanya upuuzi au unafanya vitu ambavyo havina maana yoyote kwa watu wanaokuzunguka
šŸ‘šŸ‘šŸ‘
 
Katika hotuba na mafundisho Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alisisitiza kuwa tofauti ya msingi kati ya mjinga na mpumbavu inatokana na uwezo wa mtu kupokea na kuelewa mambo
  • Mjinga: Ni yule anayekosa maarifa au asiyejua jambo fulani, lakini anafundishika. Akielezwa ukweli au kupewa elimu anaelewa na kubadilika.
  • Mpumbavu: Ni yule asiyefundishika (kichwa ngumu). Hata ukimweleza na kumuelimisha vipi, haambiliki, hataki kubadilika, na anaendelea na msimamo wake wa makosa.
 
Kuna tofauti kati ya elimu na kuelimika,unaweza ukawa na elimu ila ukawa hujaelimika,elimu yako inakua haijakukomboa kifikra,

Pia tambua kua kuna formal education na informal education,elimu ya darasani na elimu ya mtaani,

Akili ni kile kinachobaki baada ya kuondoa kile ulichofundishwa darasani,

Usichanganye kati ya elimu na inteligence,ni vitu viwili tofauti kabisa,

Education is the structured acquisition of knowledge and credentials.
Intelligence is the innate or developed capacity to think critically, adapt, and apply knowledge in real-world scenarios
 
Labda nimekosea kuwasilisha ila maana yangu ni kwamba mara nyingi tunaambiwa nenda shule uondoe upumbavu kicwani au uondoe ujinga

Sasa ndio maana nikauliza mbona baado kuna wasomi wengi tena elimu za juu lakini bado wanaonekana maamuzi yao ni kama ile elimu waliyoipata haikuondoa huo ujinga au upumbavu?
Lengo kuu la shule ni kujenga wananchi bora. Shule inapaswa ifundishe watu ustaarabu, nidhamu, udadisi na mawasiliano bora.

Bahati mbaya kwenye nchi zetu masikini, hatuwezi kumudu kutoa elimu ya namna hii.

Kwahiyo kimsingi na kinadharia shule zinapaswa zitoe upumbavu, ila kwa muktadha wa kiafrika hilo halitokei. Ukiona mtu ana utofauti flani basi ujue ni mazingira yamembadilisha.
 
Back
Top Bottom