Ufahamu kuhusu nyota za angani

Constellation ya Virgo (au Mashuke) ni mkusanyiko wa nyota unaofananishwa na mwanamwali (Virgin). Kama uko Tanzania kwa sasa Virgo inajitokeza mashariki kuanzia saa moja usiku. Ikifika saa 6 na nusu usiku itakuwa utosini kwako. Kama uko sehemu nyingine duniani nitonye nitakueleza uangalie wapi.

Kwa hiyo kama unataka kujua blackhole yetu iko muelekeo gani, jua linapozama tu angalia mashariki ndipo ilipo au angalia straight up kwenye saa sita na nusu usiku. Wakati ukiiangalia hii constellation ya Virgo basi milkway galaxy yetu iko magharibi ya Virgo. Milkway galaxy huwezi kukosa kuiona (hasa usiku wa manane). Utaona nyota nyingi kama mtu amemwaga maziwa (hence milkway) huko angani.

Vitu vinavyomezwa na blackhole vinakuwa sehemu ya hiyo blackhole na inazidi kukua.
Mzee umepiga kitabu loh!
 
Mtazamo binafsi kuhusu ufo na aliens:

Hivi nyie watu ndege za wachawi mnaziweka kundi gani? Nadhani kila mtu anawafahamu magagula, msijifanye wa mjini sana au kwamba mmesooooma!

Usiku vyombo vyao huonekana kama vimondo (meteorites), lakini vinakuwa chini zaidi, kwa vyovyote rada zina detect picha flani lakini inashindwa kueleweka ni kitu gani, pia rada zinashindwa kuvinasa, unafikiri watafikia conclusion gani... (intelligent aliens flying with miraculous objects !)... Chezea wachawi wewe!
hahahaa upo right
 
Majibu ni kama yafuatayo:

Vipi kuhusu wanasayansi je huwa wanakwenda anga za mbali au hutumwa vyombo tu?
Kati ya hapa duniani na mwezi wetu binaadamu wamesafiri sana. Hata hivi sasa kuna wanasayansi kadhaa kwenye kituo cha utafiti angani (International Space Station) wakiendelea na tafiti zao. Kituo hiki siku zote kina watu. Huwa wanabadilishana tu mara kwa mara.

Nilisikia kujengwa kwa vituo vya utafiti wa anga huko kwenye sayari nyengine je ni kweli?
Ni kweli lakini kwa sasa hakuna kituo chenye binaadam. Nitakupa mifano michache ya vyombo vya tafiti vilivyokwenda kwenye sayari.

Mars: Safari za kwenda Mars zilianza tangu 1960. Nyingi zilipeleka vyombo kupitia tu au kuizunguuka. Sasa hivi kuna magari 2 (Rovers zilizotua 2003 na 2011) yaliotua na kuendelea na utafiti. Lengo ni kuona kama baadae wanaweza kujenga kituo cha kudumu ili watu waende.

Saturn: Mwaka 2004 chombo kiitwacho Cassini-Huygens kilifika Saturn. Cassini kinaizunguuka hii sayari hata leo. Mdogo wake Huygens kilitua kwenye mwezi mmoja wa Saturn uitwao TITAN na kuona kuwa unafanana sana na dunia yetu na kuwa una mito, maziwa na mvua. Lakini mvua hii sio ya maji bali ya Methane (methane ni hewa hapa kwetu lakini ni kama maji kule kwa ajili ya baridi kali)

Kuna vyombo vingi sana vilivyopelekwa angani. Vingine vinazunguuka sayari, vingine vinatoswa ndani ya sayari kuona kuna nini, na vingine vinaendelea tu kusafiri na kuna vinavyotoka sasa kwenye solar system yetu lakini bado vinawasiliana nasi.

Vifaa na vyombo vinavyokuwa huko vinatumia power source ya aina gani?
Vyombo vyote viendavyo angani hasa kama vimepangiwa kwenda masafa marefu vinatumia vyanzo viwili vya nishati.

  • Kwanza vinakuwa na solar panels kutengenezea umeme kutokana na mwanga wa jua.
  • Lakini chanzo cha muhimu sana kwa vyombo hivi ni nguvu za nyuklia. Hivi vyombo vinakuwa na nuclear reactors zinazotengeneza umeme na kuutumia moja kwa moja au kuuhifadhi kwenye batteries. Chanzo hiki cha nishati ni muhimu sana hasa ikifikia kuwa chombo kiko mbali sana na jua mpaka jua kuonekana kama nyota tu.
Mzee Aliyekusomesha tunamshukuru
 
Mkuu samahani. Naona nilipitiwa. Nilidhani nimekujibu.

Voyager1 na Voyager2 zilirushwa mwaka 1977 (September 5, na August 20) zikiwa na majukumu mawili kila chombo.

Voyager 1
Jukumu la kwanza:
Kutembelea na kuzichunguza sayari za Jupiter, Saturn (na mwezi wa Saturn uitwao Titan).

Jukumu la pili:
Kuendelea na safari mpaka kutoka nje ya solar system yetu (Heliosphere) na kutuma taarifa za anga la huko.

Iko wapi kwa sasa (May 2016):
Iko kwenye Interstellar space zaidi ya km 21,000,000,000 kutoka hapa. (Ni sawa na umbali wa duniani mpaka kwenye jua mara 136).

Bado inawasiliana nasi?
Ndio. Huchukua takriban masaa 20 hivi kwa ujumbe kutoka Voyager1 kutufikia kupitia mtandao wa Deep-Space-Network.

Lini mwisho wa hii mission?
Nishati ya hiki chombo inapatikana kwa jenerata la nuclear. Inakadiriwa ifikapo mwaka 2025 hili jenerata litaishiwa nguvu na hapo ndio itakuwa mwisho wa mission hii.

Je kikikamatwa na aliens?
Kama watakikamata kabla ya 2025 basi kitatufahamisha. Wakikikamata baada ya 2025 basi tena ndio tutakuwa tumeula.

*******************************************************
Voyager 2
Jukumu la kwanza:
Kutembelea na kuzichunguza sayari za Jupiter, Saturn (na mwezi wa Saturn uitwao Titan), Uranus na Neptune.

Jukumu la pili:
Kama la Voyager1

Iko wapi kwa sasa (April 2016):
Iko kwenye ukingo wa heliosphere zaidi ya km 17,000,000,000 kutoka hapa. (Ni sawa na umbali wa duniani mpaka kwenye jua mara 110).

Bado inawasiliana nasi?
Ndio. Huchukua takriban masaa 17 hivi kwa ujumbe kutoka Voyager2 kutufikia kupitia mtandao wa Deep-Space-Network.
Mmh
 
Ukisafiri kwa kasi yoyote ile muda wako unatembea taratibu kuliko sisi tuliokaa. Ukiweza kusafiri katika kasi ya mwanga basi muda wako unasimama. Ni kama uliegandishwa (yaani wenzio wanaendelea kukua lakini wewe unabaki na umri wako uleule). Kwa hiyo kama ukisafiri kwa kasi ya mwanga kwa miaka 50, kwako wewe utakuwa hujabadilika (itakuwa ni kama kufumba na kufumbua) lakini ukisimama (hapa duniani) basi itakuwa ni miaka 50 ya mbele. Uliotuacha hapa duniani tulikuwa tunapwaga tu kama kawaida na tunazeeka lakini wewe ulikuwa umedumaa na umri uleule ulioondokea nao. Hii ndio maana ya kusafiri into the future. Sasa kama kasi yako ni ndogo kuliko ya mwanga basi utazeeka lakini kwa rate ndogo kuliko uliotuacha.

Dhana ni kuwa ukiweza kusafiri kwa kasi kubwa kuliko kasi ya mwanga basi unaweza kurudi into the past. Hii sidhani kama itatokea au kuwezekana.
Hahaaha hapa sidhani kama utaweza! asa utapanda hicho chombo na kukielekeza wapi kwenda Past?
 
nyota ni ndogo sana kuliko dunia, ni kama mwezi. zinategemea mwanga wa jua. na nyota ulizoona zinazobadilika kutoka rangi kutokea ya blue kwenda ya kijani ni kutokana na kuzibwa na miti na bahari .na ukiona nyekundu ujue hapo kuna radi na mvua inanyesha.
 
nyota ni ndogo sana kuliko dunia, ni kama mwezi. zinategemea mwanga wa jua. na nyota ulizoona zinazobadilika kutoka rangi kutokea ya blue kwenda ya kijani ni kutokana na kuzibwa na miti na bahari .na ukiona nyekundu ujue hapo kuna radi na mvua inanyesha.
we jamaa balaa
 
Ukisoma namna hizi pyramids zilivyojengwa na kupangiliwa utaona maajabu kwa kweli. Inaelekea hawa wajenzi walikuwa na elimu ya hali ya juu sana kuhusu nyota na mahesabu. Sasa sijui walikuwa ni Waarabu hawa hawa wa Misri au walipata msaada kutoka viumbe wengine. Ningekushauri usome vitabu au uangalie documentaries zinazozungumzia maajabu ya taaluma zilizotumika kujengea hizi pyramids.

Kitu kimoja hakina utata. Pyramid zilijengwa na mafarao walizikwa humo ili waweze kuishi milele (after life). Hii ni kweli na inatokea sasa. Sote sisi tunawazungumzia na kujifunza hawa mafarao kuliko hata tunavyowajua mababu zetu. Huko ndio kuishi katika after-life.
Waliojenga Pyramid Si waarabu! mafarao ni watu weusi/Negro kutoka Ethiopia, Sudan na East Africa!
 
Hivi mkuu mlitaka nidelete hii post? Nasema na narudia tena nilisharekebisha.
Sikuifuta kwasababu nilitaka mliochelewa kuja kwenye uzi huu mjue hapo mwanzo wengine tulikosea au tulijua vingine kabla hatujaelimishwa. Nadhani umenielewa sasa mkuu, tuko pamoja
Acha masikhara wewe!
 
Ahsante Mkuu Kifyatu ...
Sababu hili ni jukwaa wazi na jukwaa la sayansi we gusa hili jambo kwa upana wake.
Kwa asilimia kubwa hapa watu tunafungua ufahamu kujua mambo ambayo yamefichwa kwenye sayansi ya ulimwengu ivyo watu wa jukwaa hili tunapenda kujifunza njee ya mipaka ya dini....
Nakusihi wewe zungumza na sisi ndo waamuzi wa nini cha kuchukua na kuachwa.

Shukrani tena.
Neo1
Hata hili nami naliunga mkono as long as tupo kwenye darasa letu la sayansi ya anga hapa. Kama kuna kitu chochote kinachohusiana na sayansi ya anga chenye muingiliano na spiritual life hatuna budi kukiongelea kwasababu ni part n parcel ya kitu tunachokijadili hapa tangia kwa kuanzishwa uzi huu. So mkuu Kifyatu please, if you have any thing to share with us concerning Quantum physics and consciousness life karibu sana
 
Hata hili nami naliunga mkono as long as tupo kwenye darasa letu la sayansi ya anga hapa. Kama kuna kitu chochote kinachohusiana na sayansi ya anga chenye muingiliano na spiritual life hatuna budi kukiongelea kwasababu ni part n parcel ya kitu tunachokijadili hapa tangia kwa kuanzishwa uzi huu. So mkuu Kifyatu please, if you have any thing to share with us concerning Quantum physics and consciousness life karibu sana
Sawa mkuu. Nasubiri mchango wa mkuu yonga kwanza.

Nitaizungumzia quantum physics kwa kina baadae ila tujue tu kuwa fizikia ya ndani ya atoms (quantum) ni ya ajabu sana. Kuna wakati kitu kimoja kinaweza kuwa sehemu mbili au zaidi kwa wakati mmoja.

Hii saa nyingine inaleta hisia kuwa pengine maisha yetu hapa duniani yana pacha wake kwenye parallel universe (je huko ni mbinguni, au kwenye spirit world).

Nitajaribu kuielezea kwa lugha rahisi na bila ya kuingiza dini au spirituality. Hizo conclusions nitawaachia wasomaji au wataalamu wengine humu jukwaani.

cc neo1
 
Mkuu Kifyatu ukipata muda pitia Yale Mambo ya quantum physics ya three dimensions.
Naona mkuu yonga yuko kimya atakuwa ametingwa na shughuli na pilika za maisha na Christmas na mwaka mpya life iko spidi....
Tafadhari tupate cha kujifunza na pengine kuongeza mdaharo WA kufungia mwaka.
Neo1
Nipe muda mkuu, sherehe za sikukuu zimenitinga kidogo.
 
Shukrani sana mkuu.. Pia naomba ugusie kidogo kuhusu laser light inatengenezwaje na inafanyaje kazi thanks.
Electromagnetic waves zote (radio waves, microwaves, infra-red, mwanga tunaouona, ultraviolet, x-rays, gamma rays, etc) zinafuata kanuni moja na zinasafiri kwa kasi hiyo hiyo ya mwanga.

Hizi waves zina tabia moja muhimu. Ukiziangalia kwa mtazamo fulani zinaonekana kama mawimbi (waves) na zinafuata kanuni zote za mawimbi. Ukiziangalia kwa upande mwengine zinakuwa kama chembechembe (particles au photons) na zinafuata kanuni zote za particles.

Kwa hiyo uko sahihi, mwanga na radio waves ni kitu kimoja kabisa. Tofauti yao iko kwenye urefu (pia frequency) wa mawimbi yao (angalia picha hapo chini). Kasi yao ni hiyo hiyo.


EMspectrum.gif
 
Sawa mkuu. Nasubiri mchango wa mkuu yonga kwanza.

Nitaizungumzia quantum physics kwa kina baadae ila tujue tu kuwa fizikia ya ndani ya atoms (quantum) ni ya ajabu sana. Kuna wakati kitu kimoja kinaweza kuwa sehemu mbili au zaidi kwa wakati mmoja.

Hii saa nyingine inaleta hisia kuwa pengine maisha yetu hapa duniani yana pacha wake kwenye parallel universe (je huko ni mbinguni, au kwenye spirit world).

Nitajaribu kuielezea kwa lugha rahisi na bila ya kuingiza dini au spirituality. Hizo conclusions nitawaachia wasomaji au wataalamu wengine humu jukwaani.

cc neo1
Nitafurahi sana mkuu maana kuna documentary ya Quantum theory moja nilishawahi iangalia wanaongelea hiki kitu cha being at two or multiple places at the same time nikajua yawezekana kwenye universe nyingine huko yupo fyddell mwingine. Swali linakuja mbona hakuna connection yoyote ile like nijue the way he behaves, feels na je wote tutauwacha uu uhai soku moja na kwa dakika moja?
Nausubili sana uchambuzi mkuu
 
Back
Top Bottom