Uelewa wa mambo kwa watanzania ni mdogo sana, Ujinga na upumbavu unaongezeka kila mwaka

GUSSIE

JF-Expert Member
Dec 2, 2014
3,866
11,100
Yanayoendelea kwa vijana wetu Wasomi na ambao sio Wasomi huwezi kutofautisha kitu Katika kundi hili. Hoja za matusi na kutukana ndio njia pekee ya hawa vijana, Wanaamini upande mmoja wa habari

Yawezekana ni makosa yetu wazazi kuwajaza watu ujinga na wao kuyaamini kama yalivyo bila kufikiria au kujiridhisha

Mambo yafuatayo yameonyesha aina ya watu na vijana tulionao hapa JF :

Mosi, Hoja za kuendeleza gesi na maamuzi ya kutafuta wanasheria wa nje kwa ushauri, Vijana wamejazwa upepo kuwa wao wanaweza kazi hii ya sheria za kimataifa kwa kusoma soma sheria za International law pale Udsm na Udom, Wamekaa wanakula popcorn hawaelewi kuwa serikali inalipa madeni mengi kwa kudharau sheria za kimataifa, Ushauri wa kipuuzi wa wanasheria wa ndani kuwa tunaweza serikali imeishia kulipa hasara na medeni

Pili, Hoja za Bandari ya Bagamoyo, Wengi wamejazwa upepo bandari haifai,Wachina wanatupiga. Ukiwauliza wewe unafahamu mkataba wake anajibu nilimsikia Rais na Waziri. Leo hii mtu anaweza sema tutaajiri vijana 100,000 serikalini na vijana wanapiga makofi, Ukiuliza ajira zitatoka wapi kwa pesa ipi hakuna majibu, Mtu haelewi hata maana ya kina cha bandari bali utasikia aaha kule Bagamoyo si kwa Mzee JK ndio maana wanajenga bandari, Ukimuuliza sasa ulitaka JK azaliwe Dodoma

Tatu, Hoja za Freeman Mbowe na kesi inayoendelea huko mahakamani, Utasikia Leo shahidi amegalagazwa vibaya sana, Tangu lini shahidi akagalagazwa? Shahidi anaeleza alichokiona Yeye na kukishuhudia, Maswali anayoulizwa nje ya yale aliyoyasema na kuyaandika hayamuhusu,Jaji anajenga msingi kwa alichokisema shahidi, Maswali ya kuwa una degree ngapi? Una wake wangapi? Unamfahamu Tundu Lisu? Uliona watu wakibeba petrol na magogo?. Haya yote inategemea kama shahidi aliyasema kama hakuyasema ni kupoteza muda kumuuliza, Maswali nje ya context ya alichokisema na kukiandika shahidi ndio vijana wanashabikia huku wakiwa na Tecno na itel za wachina wasiowataka kujenga bandari ya Bagamoyo

Hoja ya Ridhwani Kikwete kuwa naibu Waziri, Utasikia aaha yule Ridhwani hafai kabisa, Ukiuliza lini Ridhwani amewahi kuwa Waziri na akakosea hakuna Jibu lolote, Lipi baya alilofanya Ridhwani utasikia aahaa nchi sasa imerudishwa kwa wapigaji, amepiga pesa gani hakuna majibu, Kumbe wanaumia kwanini mtoto wa fulani kawa Waziri, Kwanini uumie mtoto wa Mo Dewji kuwa tajiri kama Baba yake ulitaka avae kandambili zilizoshonwa shonwa

Hoja za Spika Ndugai kujiudhuru na chama chake cha ccm, Utasikia Spika ameonewa na Rais ana nguvu zaidi. Je unafahamu taratibu za ndani za ccm kanuni na maadili ambayo chama kilimpendekeza Ndugai kuwa Spika, Utasikia sifahamu, Ndani ya ccm mtu anawajibika kwa chama chake kwanza halafu ndio anawajibika kwenye nafasi yako uliyopewa, Hata Rais Samia anawajibika kwenye chama kwanza halafu kama Rais, Chama ndio kimekupa nguvu na sio cheo, Ndugai alivunja maadili na kanuni za chama kilichompendekeza awe Spika kwa kushindwa kujizuia kutofautisha nafasi akiwa Bungeni na nje ya Bunge

Vijana ambao wanategemea akili za watu wengine wawafikirie kwa niaba yao, Hao ni vijana mfu
 
1643152619099.png
 
Sasa jombaaa kma hizo elimu za Udom&Udsm hazna viwango vya kuzalisha wanasheria wa kusimamia miradi ya nchi, sasa kuna umuhimu gan wa kuita hizi tahasisi ni vyuo vikuuu? Si bora vifungwe?

Alafu izo sheria za kimataifa sio sheria za Mungu kusema kwamba waliotunga ndio hao hao wanahaki za kutoa wasimamizi wa sheria na makubaliano baina yao na sisi , pia haina maana kama izo sheria ni lazima wahusike watu wa nje wakati hii nchi kuna wasomi weengi tena wenye elimu nje ya Afrika.

Kwann baadhi ya watz hamjikubali?

Nawew utaingia ktk lile kundi la watz wapumbavu na wajinga, maana unampa adui nguvu na mamlaka ktk ardh yako, pia hukiamini kile unachokisoma ktk ardhi yako,

Pia Kama umesema tusitazame upande mmoja wa shilingi ktk bandari hiyo ya bagamoyo ambyo wapingaji wengi wa ujenzi, upinzan wao ni mzuri maana wanatetea nchi, je huoni kuwa huo ndio upande sahihi?
Hata kama mikataba haijawekwa wazi,lkn yasemwayo yapo lzma tusimame kwenye haki daima.

Msipende kuwahukumu waTz wote kwenye upuuzi, kuwa ni wajinga, ujinga nowadays ulishaisha kama sio kupungua.
 
Mkuu hongera kwa kujaza madukuduku yako na kuyaleta katika hali ya kubeza walio kinyume na matamanio yako.

N ahapa ni sawa na kusema kwa kejeli kuwa unakuta mtu ni msomi au sio msomi analalamika hali ya hewa ya joto kali, wakati hajui mabadiliko ya tabia nchi. Ni sawa na kusema mtu analalamika mimea kuweka dawa wakati hajawahi kulima! Ulichokifanya ni kuweka mambo mengi kwa pamoja yanayokukera katika mfumo wa kubeza, lakini sioni kama una jipya kwenye bandiko lako. Inshort huna suluhisho lolote kwa uliyoyasema zaidi ya kuyaweka katika hali ya ujuaji.
 
Mbona na wewe umelelamika sana kwenye huu uzi kutetea tumbo lako kutoka kwa mabwana zako waliokutuma..kimsingi lisemwalo lipo..watu sio wajinga hata kama hawana taarifa kamili ila taarifa walizo nazo zinamaana..nani asiyejua msoga wamerudi kupiga..nani asiyejua awamu ya 4 ilivyogubikwa na kashfa nyingi za kipigani..leo hii kuwaona wanaingia tena kwenye system unadhani wamekuja kufanya nini kama sio kuendeleza ufisadi wao.

Kimsingi huna hoja..bora ukae kwa kutulia.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mkuu hongera kwa kujaza madukuduku yako na kuyaleta katika hali ya kubeza walio kinyume na matamanio yako.

N ahapa ni sawa na kusema kwa kejeli kuwa unakuta mtu ni msomi au sio msomi analalamika hali ya hewa ya joto kali, wakati hajui mabadiliko ya tabia nchi. Ni sawa na kusema mtu analalamika mimea kuweka dawa wakati hajawahi kulima! Ulichokifanya ni kuweka mambo mengi kwa pamoja yanayokukera katika mfumo wa kubeza, lakini sioni kama una jipya kwenye bandiko lako. Inshort huna suluhisho lolote kwa uliyoyasema zaidi ya kuyaweka katika hali ya ujuaji.
Hata mimi nimeshangaa
 
GISSIE Sasa kwa mfano kesi ya Mbowe ukiacha unafki na kuwa huru kabisa je huoni kwamba maswali yanayoulizwa na kujibiwa na hao mashihidi Huwa wanajibu utopolo? Una hoja lakini umeiandika kwa mahaba na Kila mtu anajua kesi ya Mbowe ni ya mchongo.
. Kuhusu bandari ya Bagamoyo tunaomba utuelimishe kwa kutuwekea masharti ya mkataba ili tujifunze.
 
Wamemgeukia Makamba tayari kwa kuileta Consultancy firm kwenye project kuuubwa ya LNG.... waulize sasa, kampuni gani Tanzania imeshawahi kufanya consultation kwenye mradi mkubwa kama huo wenye hela nyingi....
 
Hoja yako ina mantiki na ndio kitu kinachotufanya tuendelee kubaki nyuma siku hadi siku tuwe wasindikizaji wa wageni wanaokuja toka china kuja kuuza gypsum board gerezani na kutajirika huku sisi vijana wetu wakiishia kupiga soga vijiweni.

Moja ya kosa la kiufundi ni kumtoa mkoloni mapema ikiwemo na education system yake, thinking capacity yake, work and enterprenuer attitude. Nenda zimbabwe kuna commercial farmers wazawa wakubwa leo, ukienda SAfrica kuna mabilionea weusi sababu ya msingi wa kuishi na wakoloni na kufikiri kama wakoloni. Kenya kuna national largest brewer wa bia weusi akina Muigai baba mkwe kwa Benpol. Ile kufikiri kwa haraka, problem solving na vitu hivyo wabongo bado. Hata ukiangalia matumizi yenye tija ya mitandao utapata jibu kwenye matusi wabongo wamejaa mange kimambi app. Lakini sio African voices changemakers.
 
Yanayoendelea kwa vijana wetu Wasomi na ambao sio Wasomi huwezi kutofautisha kitu Katika kundi hili. Hoja za matusi na kutukana ndio njia pekee ya hawa vijana, Wanaamini upande mmoja wa habari

Yawezekana ni makosa yetu wazazi kuwajaza watu ujinga na wao kuyaamini kama yalivyo bila kufikiria au kujiridhisha

Mambo yafuatayo yameonyesha aina ya watu na vijana tulionao hapa JF :

Mosi, Hoja za kuendeleza gesi na maamuzi ya kutafuta wanasheria wa nje kwa ushauri, Vijana wamejazwa upepo kuwa wao wanaweza kazi hii ya sheria za kimataifa kwa kusoma soma sheria za International law pale Udsm na Udom, Wamekaa wanakula popcorn hawaelewi kuwa serikali inalipa madeni mengi kwa kudharau sheria za kimataifa, Ushauri wa kipuuzi wa wanasheria wa ndani kuwa tunaweza serikali imeishia kulipa hasara na medeni

Pili, Hoja za Bandari ya Bagamoyo, Wengi wamejazwa upepo bandari haifai,Wachina wanatupiga. Ukiwauliza wewe unafahamu mkataba wake anajibu nilimsikia Rais na Waziri. Leo hii mtu anaweza sema tutaajiri vijana 100,000 serikalini na vijana wanapiga makofi, Ukiuliza ajira zitatoka wapi kwa pesa ipi hakuna majibu, Mtu haelewi hata maana ya kina cha bandari bali utasikia aaha kule Bagamoyo si kwa Mzee JK ndio maana wanajenga bandari, Ukimuuliza sasa ulitaka JK azaliwe Dodoma

Tatu, Hoja za Freeman Mbowe na kesi inayoendelea huko mahakamani, Utasikia Leo shahidi amegalagazwa vibaya sana, Tangu lini shahidi akagalagazwa? Shahidi anaeleza alichokiona Yeye na kukishuhudia, Maswali anayoulizwa nje ya yale aliyoyasema na kuyaandika hayamuhusu,Jaji anajenga msingi kwa alichokisema shahidi, Maswali ya kuwa una degree ngapi? Una wake wangapi? Unamfahamu Tundu Lisu? Uliona watu wakibeba petrol na magogo?. Haya yote inategemea kama shahidi aliyasema kama hakuyasema ni kupoteza muda kumuuliza, Maswali nje ya context ya alichokisema na kukiandika shahidi ndio vijana wanashabikia huku wakiwa na Tecno na itel za wachina wasiowataka kujenga bandari ya Bagamoyo

Hoja ya Ridhwani Kikwete kuwa naibu Waziri, Utasikia aaha yule Ridhwani hafai kabisa, Ukiuliza lini Ridhwani amewahi kuwa Waziri na akakosea hakuna Jibu lolote, Lipi baya alilofanya Ridhwani utasikia aahaa nchi sasa imerudishwa kwa wapigaji, amepiga pesa gani hakuna majibu, Kumbe wanaumia kwanini mtoto wa fulani kawa Waziri, Kwanini uumie mtoto wa Mo Dewji kuwa tajiri kama Baba yake ulitaka avae kandambili zilizoshonwa shonwa

Hoja za Spika Ndugai kujiudhuru na chama chake cha ccm, Utasikia Spika ameonewa na Rais ana nguvu zaidi. Je unafahamu taratibu za ndani za ccm kanuni na maadili ambayo chama kilimpendekeza Ndugai kuwa Spika, Utasikia sifahamu, Ndani ya ccm mtu anawajibika kwa chama chake kwanza halafu ndio anawajibika kwenye nafasi yako uliyopewa, Hata Rais Samia anawajibika kwenye chama kwanza halafu kama Rais, Chama ndio kimekupa nguvu na sio cheo, Ndugai alivunja maadili na kanuni za chama kilichompendekeza awe Spika kwa kushindwa kujizuia kutofautisha nafasi akiwa Bungeni na nje ya Bunge

Vijana ambao wanategemea akili za watu wengine wawafikirie kwa niaba yao, Hao ni vijana mfu

Mbona unatufokea!!!!??
 
siku hizi jf kunazidi kujaa watu wa hovyohovyo yani mtu anakuwa na akili mgando kiasi ambacho unashanga kama huyu ni mtu alopita vidudu ama la.

Nianze tu na wale watu wa kupandikizana chuki dhidi ya mtu flani, kundi flani ama taasisi flan, Watanzania tuache hiyo mihemko ya kubeba chuki ndani ya mioyo yetu kisa flani kasema simpendi flani na nampenda flani unakuta mtanzania anachuki haswaa na tasisi flani ukimuuliza wamekufanyajee utasikia oooh sijui ilikuwa hivi mara vilee. kiufupi usimkumbatie adui wa mwenzako na kutembea nae,

Mtoa mada ka sijakuelewa kuhusu issue ya Bwagamoyo!
issue ya bwagamoyo binafsi sijawahi ielewa hata na sitokaa nielewe, sioni sababu ya kujenga bandari bwagamoyo wakati mtwara na tanga kuna bandari nzuri zenye kina kizuri tuu na hata kama tukizitengeneza hazita gharimu fedha nyingi kama kwenda kuchima huko bwagamoyo. Bandari ya Dar inagharama nyingi kutokana na utoaji wa mchanga wa mara kwa mara pili mji ushakuwa huu tunahitaji kukuza miji mingine.
binafsi napendekeza kama wanamalengo mazuri fedha za Bwagamoyo wazihamishie mtwara ambako kunabandari nzuri yenye kina kirefu kisichihitaji kuchimbwa tena pia itafanya mkoa wa mtwara kuinuka kiuchumi, ikumbukwe sina maslahi na Mtwara
 
Back
Top Bottom