Gang Chomba
Platinum Member
- Feb 29, 2008
- 20,734
- 4,869
BONGE LA MECHI: Ni UEFA 2013 semifinal kati ya Bayern Munich na Barcelona.
Champions League hii ya leo Apr 23, 2013, itakuwa kali sana.
Stay connected with JF Sports kupata Live Updates.
===
Uwezekano wa timu mbili kutoka Ujerumani au timu mbili kutoka Uhispania kukutana mwezi ujao katika fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya Champions League bado uko hai, na majibu, dalili za nani zaidi zikaanza kuonekana baada ya matanage wa leo.
Ni baada ya timu za Uhispania na Ujerumani kutenganishwa katika droo iliyofanywa katika makao makuu ya shirikisho la soka ulaya UEFA ya nusu fainali.
Fainali itafanyika uwanja wa Wembley jijini London huenda ikawa pambano jingine la Ujerumani na Uhispania.
Bayern Munich ambao walishindwa katika fainali mwaka jana, na ambao tayari wamenyakua taji la Bundesliga, wanaangushana na viongozi wa La liga Uhispania.
Katika mchuwano mwingine, Borussia Dortmund watakabana koo na Real Madrid wakati wawakilishi wa miamba ya sasa ya soka barani Ulaya wakiumiza nyasi.
Mechi za mkondo wa kwanza utachezwa leo Aprili 23 na kesho 24, huku za mkondo wa pili ukichezwa Aprili 30 na Mei mosi.
Fainali itachezwa jijini London katika uga wa Wembley mnamo Mei 25.
===
Kukosemakana kwa AC Milan katika hatua hii imepelekea Mashindano kukosa Ladha...