UEFA Champions League, Special Thread

UEFA Champions League, Special Thread

Status
Not open for further replies.
Kuanzia sasa naenjoy tu soka haijalishi ninaekutana nae!nasikia tukichomoka munich tunatua catalunya,oh i enjoy this one!halafu kuna asilimia kubwa nikichomoka kwa barca naenda wembley na Cr7,uuwii!ila sijui kwa nini galatasaray nawaona kikwazo kwa madrid!i just feel that way!
 
1. Madrid vs Galatasaray (Galatasaray Win)
2. Paris Saint German vs Barcelona (Barcelona Win)
3. Malaga vs Borussia Dortmund ( Dortmund Win)
4. Bayern Munich vs Juventus (Juventus Win)

Ni mtazamo wangu huo!!


Hapo kwa upande wangu Madrid na Galatasaray mie natoa 50/50
Ila kwa kuangalia historia Madrid anapita.

Kwengine huko niko. Pamoja na ww.

Barcelona timu ya kwanza Final
 
Gutierez mimi Gang Chomba, nikiwa na akili timamu pasipo kushinikizwa na mtu napenda kusema wazi kuwa Bayern safari imewadia.

Hii timu inaitwa Juve ni timu nzuri sana.
Kitu kinachowatia shaka wapenzi wa Soka ni kutopata wasaa wa kuwatazama wajukuu hawa wa Bibi Lavecchia Signora.

Juve wana kipa, ukuta, kiungo na pia wana washambuliaji wa uhakika na wenye uzoefu.
Kiungo cha Bayern ndio kiungo cha timu yao ya Taifa.
Ukizungumzia kiungo cha Bayern ndio kile ambacho Kina Kloose, Muller na Bastian.
Kiungo hiki kiliwahi kunyamazishwa na Panenca katika mashindano ya Euro yalopita.

Pia Juve wana Wing Back za kueleweka ambazo ni World Class player, hapa nawazungumzia Lichsteiner na nguli Giorgio Chielini.
Kisha Bianconelli wana dabali zenye akili na katili, na zimekaa muda kwa pamoja muda mrefu sasa na zinaelewana.

Kama yoote hio haitoshi narejea kumbukumbu ya kauli ya Elgodo Infernomena Ronaldo de Lima aliepata kunena kuwa endapo utaumaliza ukuta woote wa Juve basi usianze kujishaua kushangilia, subiri uone nyavu za ndani zikitikisika kisha ndio uanze kusasambua jezi na kuanza kushangilia.
Aliisema kauli hiyo baada ya kushindwa kumfunga Buffon 1 against 1 na kuweka bayana kuwa Gigi ni habari nyingine na hana mfano wake Duniani.

So Bayern waende wakijuwa wanakwenda kutana ka timu kwelikweli ambayo hairuhusu Goli na Inasaka Magoli.

Naomba niishie hapo ili kupisha wadau kama wana maswali ama hoja ili wapenyeze katika post yangu hii.

Bismillah

Amin.....
 
1/2FINAL hii hapa:
----real madrid
----barcelona
----bayern munchen
----borussia dortmund

2 za spain, 2 za german!!!!!
 
Haaaahaaaaahaaaaaaaa mbona unalo naona hilo jasho lakutoka baada ya timu yako kufungwa,haya nakuja kukupepea sasa hivi.
..........mbona sasa umechelewa hujaja kunipepea, sitaki sssasa, sitaki sssasa, eeeh sitaki, ndio sitaki.......
 
Michu alidai kuwa amekwenda EPL kukuza jina, na kweli ni nyeta hatari huko premier.

Ni kweli kabisa Spain La Liga nani angemuona? Hata hivyo vyombo hivyo hivyo vya Uingereza vinashinikiza kuwa sasa awe anaitwa nationala team, lakini ninavyojua hatacheza katika timu ya taifa kabsa hata kama watamuita.
 
Wenye weredi wa Soka washaelewa tukitoka hapa ni timu zipi zitakutana.
Wewe unaekaa na kusubiri ipangwe droo ya Nusu Fainali pole sana.

Weledi wa upenzi wa timu mbovu? Tusubiri na tuone sisi wengine tunapiga hesabu kisayansi sio uganga wa kienyeji na mapenzi ya timu.
 
Weledi wa upenzi wa timu mbovu? Tusubiri na tuone sisi wengine tunapiga hesabu kisayansi sio uganga wa kienyeji na mapenzi ya timu.


Mi nakutumia wewe kama ubao, uende ukawafundishe oya oya wenzio.
nusu Fainali haina upangaji mdogo wangu.
Yaani hapa timu zishajuwa kama zitafudhu zitakutana na timu gani mbeleni
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom