UDSM kwa sasa ni cha kata, imebaki historia tu

UDSM kwa sasa ni cha kata, imebaki historia tu

kujigamba kisa umesoma chuo "x" ni ushamba tu. Tunataka tuone mabadiriko chanya huku mtaani. Kupata GPA kubwa au ndogo alafu useless ni sawa na hamna ulichofanya. Soma vizuri (fuatilia na zingatia masomo) ili yakusaidie na usaidie binadamu wenzako.
 
Umenifungua macho mkuu. Mara nyingi nlikuwa najiuliza kwanini UDOM huwa inashambuliwa sana na watu kutoka UDSM wakati Tanzania ina vyuo vikuu vingi tu. Ni mara chache sana utakuta vipanga kutoka vyuo kama MZUMBE, SUA n.k wakiattack chuo cha UDOM.
 
Hakuna ambaye halijuhi hilo wanajisahurisha tu. Udsm haikufurahishwa kabisa na uanzishwaji wa course za sayansi ambazo nyingi ni kama za Udsm, kwa kuhofia competition wakaanzisha propaganda za kukichafua chuo cha udom, ndiyo maana udsm wanakiandama chuo cha udom kila uchao, jiulize kwa nini hakuna ushindani kati ya udsm na vyuo vingine, kibaya zaidi siasa hii ya elimu imepiga hodi kwenye ofisi na korido za wasimamizi wa hivi vyuo kitu ambacho hakina afya kwenye elimu yetu.
Umenifumbua macho maana mara nyingi nlikuwa najiuliza kwa nini UDOM inashambuliwa sana na watu kutoka UDSM wakat Tanzania ina vyuo vingi tu kama SUA na MZUMBE.
 
Sasa kama udsm ni cha kata. Hivyo vyuo vingine vitakua na hali gani?
Kwa Tanzania ebu tuwape credits zao tu udsm, sua na Muhas.
 
Back
Top Bottom