Artificial intelligence
JF-Expert Member
- Jan 28, 2021
- 1,262
- 2,191
Udsm ni chuo kilichokuwa kimejipambanua miaka hiyo kama chuo bora kabisa katika ukanda huu wa maziwa makuu na afrika kwa ujumla kwa kuzalisha viongozi na wasomi mahili katika nyanja ya siasa, uchumi, na sheria.
Sifa hiyo ilikijengea chuo uimara na kukifanya kiwe chuo bora afrika mashariki na kati kwa wakati ule huku kikiwa nguzo imara na tunu ya elima ya juu ya Tanzania miaka ile na siyo sasa.
Huku systems zote za nchi zikiwa zinasimamiwa na kuongozwa na wasomi na viongozi kutoka UDSM, ambao hata hvyo hawajaweza kulinufaisha taifa kimaendeleo bali wakijikita kwenye utunganji wa sera za hovyo na kusaini mikataba mibovu ya kulikwamisha taifa kimaendeleo.
Kwa sasa siyo tu kwamba elimu inayotolewa na udsm ni mbovu bali hata mifumo na sera za uendeshaji wa chuo hiki zimeparaganyika hasa kuanzia mwaka 2010, hivyo kupeleka kuzalisha wasomi wenye uelewa mdogo wa mambo na wasioweza kushindana tena katika soko la ajira kama zamani.
Hali hii imepelekea chuo hiki kujikuta kwenye ushindani mkubwa kutoka vyuo vingine kama SUA ambacho naweza sema ndicho chuo pekee kinachofanya tafiti za kweli na zenye tija hapa Tanzania , MUHAS, MZUMBE, UDOM, NELSON MANDELA na ARDHI.
Kutokana na sababu hizo chuo hiki kimebaki kutembelea historia kwenye nyanja zote na kujikita kwenye siasa ya elimu, kutokana na wigo mpana wa kuwa na wasomi wengi waliotapakaa kila idara za serikali, wasomi hawa muda wote wamejikuta kwenye propaganda za kushindanisha ubora wa elimu ya UDSM na vyuo vingine hasa UDOM, Kikifika mbali hadi kuanzisha course zisizotambuliwa na serikali mfano molecular biology and Biotechnology, hiki ni kiashiria tosha kwamba chuo kimeshuka ubora kwani kushindana na chuo chenye miaka 12 tu kwenye taaluma huku chenyewe kikiwa na miaka zaidi ya 40 haileti afya kwenye taaluma.
Katika jambo la kushangaza muhitimu bora wa chuo hichi mwaka huu aliyefanyiwa branding ya kutosha na kupewa airtime ya kutosha kwenye vyombo vya habari alisikika akisema "hakupata mkopo, alipewa boom tu", hii ni aibu kubwa kwa muhusika na chuo pia, na kama aliyesema hivyo angekuwa muhitimu wa chuo kingine hasa UDOM mitandaoni kusingekalika, kwa wasomi wa udsm kuhoji ubora wa muhitimu, GPA na chuo husika.
Mwaka huu ndugu yangu alihitimu shahada ya kemia Udsm akiwa na GPA ya 3.9, lakini hajui chochote kuhusu carbon NMR spectrum, IR spectrum, GC-MS,LC-MS, TGA vitu ambavyo ni basics kwenye instrumental analysis, hiki ni kiashiria kwamba ubora wa elimu ya udsm umeshuka.
Mwaka huu nilikuta muhitimu wa zoology stationery akiwa na cheti safi kabisa chenye GPA 4.2 kutoka Udsm, jambo la kushangaza muhitimu huyo hata basics za computer applications hajui, yaani alishindwa kabisa kutumia copy, cut, paste vitu ambavyo ni vya kawaida sana, je project alifanyaje?, anajua mwenyewe, hii yote inaonyesha jinsi gani ubora wa Udsm umeshuka.
Mwisho kabisa katika elimu hakunaga umungu mtu, ukijisahau kidogo tu wenzako wanakuongoza, hivyo udsm ijitafakari upya, udsm siyo ya kushindana na Udom nyakati hizi labda miaka ijayo , udsm mnatakiwa mshindane na NAIROBI, MAKERERE, PRETORIA universities kutokana na ukongwe wenu kwenye taaluma.
Sifa hiyo ilikijengea chuo uimara na kukifanya kiwe chuo bora afrika mashariki na kati kwa wakati ule huku kikiwa nguzo imara na tunu ya elima ya juu ya Tanzania miaka ile na siyo sasa.
Huku systems zote za nchi zikiwa zinasimamiwa na kuongozwa na wasomi na viongozi kutoka UDSM, ambao hata hvyo hawajaweza kulinufaisha taifa kimaendeleo bali wakijikita kwenye utunganji wa sera za hovyo na kusaini mikataba mibovu ya kulikwamisha taifa kimaendeleo.
Kwa sasa siyo tu kwamba elimu inayotolewa na udsm ni mbovu bali hata mifumo na sera za uendeshaji wa chuo hiki zimeparaganyika hasa kuanzia mwaka 2010, hivyo kupeleka kuzalisha wasomi wenye uelewa mdogo wa mambo na wasioweza kushindana tena katika soko la ajira kama zamani.
Hali hii imepelekea chuo hiki kujikuta kwenye ushindani mkubwa kutoka vyuo vingine kama SUA ambacho naweza sema ndicho chuo pekee kinachofanya tafiti za kweli na zenye tija hapa Tanzania , MUHAS, MZUMBE, UDOM, NELSON MANDELA na ARDHI.
Kutokana na sababu hizo chuo hiki kimebaki kutembelea historia kwenye nyanja zote na kujikita kwenye siasa ya elimu, kutokana na wigo mpana wa kuwa na wasomi wengi waliotapakaa kila idara za serikali, wasomi hawa muda wote wamejikuta kwenye propaganda za kushindanisha ubora wa elimu ya UDSM na vyuo vingine hasa UDOM, Kikifika mbali hadi kuanzisha course zisizotambuliwa na serikali mfano molecular biology and Biotechnology, hiki ni kiashiria tosha kwamba chuo kimeshuka ubora kwani kushindana na chuo chenye miaka 12 tu kwenye taaluma huku chenyewe kikiwa na miaka zaidi ya 40 haileti afya kwenye taaluma.
Katika jambo la kushangaza muhitimu bora wa chuo hichi mwaka huu aliyefanyiwa branding ya kutosha na kupewa airtime ya kutosha kwenye vyombo vya habari alisikika akisema "hakupata mkopo, alipewa boom tu", hii ni aibu kubwa kwa muhusika na chuo pia, na kama aliyesema hivyo angekuwa muhitimu wa chuo kingine hasa UDOM mitandaoni kusingekalika, kwa wasomi wa udsm kuhoji ubora wa muhitimu, GPA na chuo husika.
Mwaka huu ndugu yangu alihitimu shahada ya kemia Udsm akiwa na GPA ya 3.9, lakini hajui chochote kuhusu carbon NMR spectrum, IR spectrum, GC-MS,LC-MS, TGA vitu ambavyo ni basics kwenye instrumental analysis, hiki ni kiashiria kwamba ubora wa elimu ya udsm umeshuka.
Mwaka huu nilikuta muhitimu wa zoology stationery akiwa na cheti safi kabisa chenye GPA 4.2 kutoka Udsm, jambo la kushangaza muhitimu huyo hata basics za computer applications hajui, yaani alishindwa kabisa kutumia copy, cut, paste vitu ambavyo ni vya kawaida sana, je project alifanyaje?, anajua mwenyewe, hii yote inaonyesha jinsi gani ubora wa Udsm umeshuka.
Mwisho kabisa katika elimu hakunaga umungu mtu, ukijisahau kidogo tu wenzako wanakuongoza, hivyo udsm ijitafakari upya, udsm siyo ya kushindana na Udom nyakati hizi labda miaka ijayo , udsm mnatakiwa mshindane na NAIROBI, MAKERERE, PRETORIA universities kutokana na ukongwe wenu kwenye taaluma.