Udondozi katika ripoti ya CAG kuhusu Dr.Dau na NSSF

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
49,582
105,607
Ubia katika kuendeleza mji wa Kigamboni

NSSF iliiingia ubia na Kampuni ya Azimio Housing Estate.Katika mkataba huo Azimio ilitakiwa kuendeleza ekari 20,000 za ardhi iliyopo Kigamboni ambapo kwa hatua ya awali ingeanza na ekari 300. Jumla ya gharama za mradi ni USD 653.44M ambapo NSSF ingetoa 45% ya gharama na Azimio ingetoa 35% na ardhi inayodhaminiwa kwa 20% ya gharama ya mradi.

Ukaguzi wa hatimiliki unaonyesha kuwa Azimio inamiliki viwanja viwili yenye ukubwa wa 1.98 hekta na 114.11 hekta, hatimiliki hizi jumla zina ukubwa wa ekari 286.74, pungufu ya ekari 13.26 kutoka kwenye hekari 300 zilizopangwa.

Hata hivyo CAG hakupatiwa ya hatimiliki ya ardhi ambayo Azimio iliahidi kutoa kama uhangiaji katika mtaji. Hivyo hakuna uthibitisho wa uwepo wa viwanja hivyo ekari 19,700. Fedha za NSSF zipo kwenye hatari kubwa ya kupotea.


Utekelezaji wa Mkataba wa Ubia katika mradi wa Mji wa kisasa Arumeru kati ya NSSF na Azania Housing Estate

Kwa mwaka 2014/2015 NSSF ilipokea upembuzi yakinifu wa mradi pendekezwa kutoka Azania ambapo bodi ya wazamini iliidhinisha kuingiza katika ubia ardhi iliyotolewa na Azania mkoa wa Lindi, Mtwara, Mwanza na Arusha.

Ada ya Ushauri kwa kampuni iliyobuni mradi huo ilikuwa ni bilioni 468.9 na ilipangwa bilioni 2.4 itumike katika awamu ya upangaji.Hata hivyo kiasi kiliongezwa mpaka bilioni 43.9 bila idhini ya bodi ya uthamini.

Tarehe 20 January 2016 NSSF na kampuni ya Azania walisaini kusitisha utekelezaji wa mradi huo kwa makubaliano ya pamoja


Malipo yaliyofanywa na NSSF zaidi ya kiasi kilihokubali USD 9M

CAG aligundua kuwa NSSF imewekeza bilioni 205.14, kampuni ya Azania imechangia USD 5.5M kwenye mradi husika.

Makubaliano kati ya NSSF na Azania ilikuwa NSSF itawekeza mpaka thamini ya uwekezaji uwe sawa na thamini ya ardhi iliyotolewa na Azania ndipo pande zote zianze kuchangia katika uwiano ulio sawa. Hii ina maana kuwa NSSF ilichangia USD 9M zaidi ya kiasi ilichotakiwa kuchangia.

Kutolewa kwa Mikopo kwa SACCOS zaidi ya inavyostahili

Katika mradi wa mikopo kwa SACCOS, NSSF ilitoa mikopo kwa SACCOS tisa ikiwamo Bumbuli Development Corporation kinyume na sera ya kukopesha shirika. Mikopo ilitolewa zaidi ya 50% ya mali za SACCOS. Upembuzi wa awali ulionyesha kuwa SACCOS hizo ziliomba kiasi ambacho hazikustahili. Hata hivyo ushauri ulipuuzwa na uongozi. Hizo SACCOS ni za nani utajaza mwenyewe



S/N JINA LA SACCOS Ziada iliyotolewa

1 Bumbuli Development 948,956,192

2 Korongo SACCOS 481,630,640

3 UMMA SACCOS 63,469,000

4 SBC Saccos 384,770,255

5 Hekima saccos 39,782,033

6 Ukombozi SACCOS 137,097,246

7 Uzinza SACCOS 69,056,896

8 Harbor SACCOS 7,000,000

9 Umoja SACCOS 52, 348,000

To be continued
 
Katika mradi wa mikopo kwa SACCOS, NSSF ilitoa mikopo kwa SACCOS tisa ikiwamo Bumbuli Development Corporation kinyume na sera ya kukopesha shirika. Mikopo ilitolewa zaidi ya 50% ya mali za SACCOS. Upembuzi wa awali ulionyesha kuwa SACCOS hizo ziliomba kiasi ambacho hazikustahili. Hata hivyo ushauri ulipuuzwa na uongozi. Hizo SACCOS ni za nani utajaza mwenyewe

Haya maneno nayo ni ya CAG?
 
Ritz njoo uweke siti ya mbele
Teh teh teh!

Hiyo ripoti ya uongo bana naitaka hii hapa ndiyo ya kweli.


Tunamuomba Rais John Magufuli amchukulie hatua za kisheria kama wanavyofanyiwa wakubwa wengine waliolitia taifa letu hasara. Hiki ni kiasi kikubwa cha fedha ambacho kingeweza kutumiwa kutatua kero mbalimbali zinazotukabili Watanzania,” alisema msomaji aliyejitambulisha kwa jina la Seve Nyari kutoka Singida.Joji Salum, aliyepiga simu kutoka Kigamboni, Dar alisema ni kweli mradi wa ujenzi wa Jiji Jipya la Kigamboni umesimama na hawajui ni kwa sababu gani, lakini kwa ufisadi wa fedha zinazotajwa, hakuna jinsi zaidi ya kumsulubu Dau ambaye aliteuliwa na Rais Magufuli kuwa balozi lakini bado hajapangiwa kituo cha kazi kwa sababu alishiriki kwa asilimia mia moja si kwa kuzichukua bali kama mtendaji mkuu.Kutoka Arusha, ambako NSSF inaendelea na mradi mwingine wa ujenzi wa nyumba wilayani Arumeru, Maige Joseph alisema:


Wakati umefika kwa mifuko ya jamii kama huu, kudhibitiwa katika uanzishaji wa miradi yake, kwani mingi ni ya kifisadi yenye kuwanufaisha wakubwa.“Sasa mtu una ardhi yako, lakini unanunua tena ya mtu mwingine, tena kwa bei ghali zaidi. Yaani unatoka kilometa 30 kutoka Arusha mjini, unakwenda kununua heka moja kwa shilingi bilioni moja!? Hii haijapata kutokea, labda Tanzania tu. Wasulubiwe walioshiriki,” alisema Maige.Akaongeza: “Nasema Dau anahusika kwa sababu si ndiyo alikuwa bosi mkuu? Maana yake ni kwamba hakuna kilichokuwa kikifanyika bila ya yeye kujua.

Ni lazima anajua mwanzo mwisho. Mimi naona hata huo ubalozi ungetenguliwa tu kwani ameacha doa NSSF.”Kauli ya kutaka watu wote waliohusika kufisadi fedha hizo wasubulubiwe, pia ilitoka kwa wananchi waliopiga simu kutoka Mwanjelwa Mbeya, Tukuyu (pia Mbeya), Iringa mjini, Mtwara, Simiyu, Kondoa (Dodoma), Tanga na Mwanza.Ufisadi ulioibuliwa hivi karibuni ni kiasi cha shilingi trilioni 1.3 kinadaiwa kutumiwa na NSSF katika mazingira yanayotia shaka katika ununuzi wa ardhi ili kutekeleza miradi miwili ya ujenzi wa nyumba huko Kigamboni na Arumeru mkoani Arusha. Jijini Dar es Salaam, mfuko huo ulianzisha mradi uitwao Dege Eco Village ambao Bodi ya NSSF iliunda Kampuni ya Hifadhi Builders inayosimamia ujenzi huo ikishirikiana na Kampuni ya Azimio Housing Estate Limited.Inadaiwa Azimio Housing Estate inayomiliki ekari 20,000 huko Kigamboni, iliiuzia NSSF eneo la ekari 300 kwa shilingi milioni 800 kwa ekari moja, badala ya bei halali ya shilingi milioni 39 kwa ekari tofauti na bei iliyotangazwa na Manispaa ya Temeke mwaka 2012 wakati ikiuza eneo lake kwa shilingi elfu nane kwa mita ya mraba.Katika ujenzi wa Arumeru, inadaiwa kampuni hiyo ya Azimio, iliiuzia NSSF ekari moja kwa shilingi bilioni 1.8, wakati bei halisi ya ukubwa huo kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo lililo umbali wa zaidi ya kilometa 30 kutoka jijini Arusha, ni kati ya shilingi laki tano hadi milioni moja.

Uchunguzi unaonesha Azimio iliuza eka 300 za Kigamboni kwa dola 108, 906,113 (sawa na madafu bilioni 217.8), wakati huko Arumeru mfuko huo uliuziwa ekari 655 kwa dola 556, 764, 924 (trilioni 1.13) na hivyo kuifanya jumla ya fedha ambazo ‘zimeliwa’ katika miradi hiyo miwili katika ardhi peke yake kufikia trilioni 1.3.
 
Makamba na Bumbuli Developmentwatajwa kuvuta NSSF
Kama kawaida yenu hapa unamuwekea maneno CAG.

"Katika mradi wa mikopo kwa SACCOS, NSSF ilitoa mikopo kwa SACCOS tisa ikiwamo Bumbuli Development Corporation kinyume na sera ya kukopesha shirika. Mikopo ilitolewa zaidi ya 50% ya mali za SACCOS. Upembuzi wa awali ulionyesha kuwa SACCOS hizo ziliomba kiasi ambacho hazikustahili. Hata hivyo ushauri ulipuuzwa na uongozi. Hizo SACCOS ni za nani utajaza mwenyewe"
 
Since 2010 tumekuwa tunaambiwa NSSF imefilisika imebaki fupa lakini ndio unazidi kufanya uwekezaji wa Mabilion ikiwemo daraja la kihistoria sasa sijui Kamusi zao neno kufilisika linatafsiriwa vipi?
Hawezi kuweka ripoti za mashirika mengine tofauti na NSSF watu wanavyopiga pesa tutayaweka sisi.
 
Teh teh teh!

Hiyo ripoti ya uongo bana naitaka hii hapa ndiyo ya kweli.


Tunamuomba Rais John Magufuli amchukulie hatua za kisheria kama wanavyofanyiwa wakubwa wengine waliolitia taifa letu hasara. Hiki ni kiasi kikubwa cha fedha ambacho kingeweza kutumiwa kutatua kero mbalimbali zinazotukabili Watanzania,” alisema msomaji aliyejitambulisha kwa jina la Seve Nyari kutoka Singida.Joji Salum, aliyepiga simu kutoka Kigamboni, Dar alisema ni kweli mradi wa ujenzi wa Jiji Jipya la Kigamboni umesimama na hawajui ni kwa sababu gani, lakini kwa ufisadi wa fedha zinazotajwa, hakuna jinsi zaidi ya kumsulubu Dau ambaye aliteuliwa na Rais Magufuli kuwa balozi lakini bado hajapangiwa kituo cha kazi kwa sababu alishiriki kwa asilimia mia moja si kwa kuzichukua bali kama mtendaji mkuu.Kutoka Arusha, ambako NSSF inaendelea na mradi mwingine wa ujenzi wa nyumba wilayani Arumeru, Maige Joseph alisema:


Wakati umefika kwa mifuko ya jamii kama huu, kudhibitiwa katika uanzishaji wa miradi yake, kwani mingi ni ya kifisadi yenye kuwanufaisha wakubwa.“Sasa mtu una ardhi yako, lakini unanunua tena ya mtu mwingine, tena kwa bei ghali zaidi. Yaani unatoka kilometa 30 kutoka Arusha mjini, unakwenda kununua heka moja kwa shilingi bilioni moja!? Hii haijapata kutokea, labda Tanzania tu. Wasulubiwe walioshiriki,” alisema Maige.Akaongeza: “Nasema Dau anahusika kwa sababu si ndiyo alikuwa bosi mkuu? Maana yake ni kwamba hakuna kilichokuwa kikifanyika bila ya yeye kujua.

Ni lazima anajua mwanzo mwisho. Mimi naona hata huo ubalozi ungetenguliwa tu kwani ameacha doa NSSF.”Kauli ya kutaka watu wote waliohusika kufisadi fedha hizo wasubulubiwe, pia ilitoka kwa wananchi waliopiga simu kutoka Mwanjelwa Mbeya, Tukuyu (pia Mbeya), Iringa mjini, Mtwara, Simiyu, Kondoa (Dodoma), Tanga na Mwanza.Ufisadi ulioibuliwa hivi karibuni ni kiasi cha shilingi trilioni 1.3 kinadaiwa kutumiwa na NSSF katika mazingira yanayotia shaka katika ununuzi wa ardhi ili kutekeleza miradi miwili ya ujenzi wa nyumba huko Kigamboni na Arumeru mkoani Arusha. Jijini Dar es Salaam, mfuko huo ulianzisha mradi uitwao Dege Eco Village ambao Bodi ya NSSF iliunda Kampuni ya Hifadhi Builders inayosimamia ujenzi huo ikishirikiana na Kampuni ya Azimio Housing Estate Limited.Inadaiwa Azimio Housing Estate inayomiliki ekari 20,000 huko Kigamboni, iliiuzia NSSF eneo la ekari 300 kwa shilingi milioni 800 kwa ekari moja, badala ya bei halali ya shilingi milioni 39 kwa ekari tofauti na bei iliyotangazwa na Manispaa ya Temeke mwaka 2012 wakati ikiuza eneo lake kwa shilingi elfu nane kwa mita ya mraba.Katika ujenzi wa Arumeru, inadaiwa kampuni hiyo ya Azimio, iliiuzia NSSF ekari moja kwa shilingi bilioni 1.8, wakati bei halisi ya ukubwa huo kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo lililo umbali wa zaidi ya kilometa 30 kutoka jijini Arusha, ni kati ya shilingi laki tano hadi milioni moja.

Uchunguzi unaonesha Azimio iliuza eka 300 za Kigamboni kwa dola 108, 906,113 (sawa na madafu bilioni 217.8), wakati huko Arumeru mfuko huo uliuziwa ekari 655 kwa dola 556, 764, 924 (trilioni 1.13) na hivyo kuifanya jumla ya fedha ambazo ‘zimeliwa’ katika miradi hiyo miwili katika ardhi peke yake kufikia trilioni 1.3.
teh teh teh
naona umeanza kuiita na hii ya uongo.

Mwaka huu Dau hachomoki aiseeee
 
Kama kawaida yenu hapa unamuwekea maneno CAG.

"Katika mradi wa mikopo kwa SACCOS, NSSF ilitoa mikopo kwa SACCOS tisa ikiwamo Bumbuli Development Corporation kinyume na sera ya kukopesha shirika. Mikopo ilitolewa zaidi ya 50% ya mali za SACCOS. Upembuzi wa awali ulionyesha kuwa SACCOS hizo ziliomba kiasi ambacho hazikustahili. Hata hivyo ushauri ulipuuzwa na uongozi. Hizo SACCOS ni za nani utajaza mwenyewe"
maneno hapo ni Hizo SACCOS ni za nani utajaza mwenyewe...mengine nimeweka kama yalivyo.acha upunguani mkuu
 
Back
Top Bottom