Udini waingilia Rasmi kampeni Igunga

Udini waingilia Rasmi kampeni Igunga

sasa kama ndo tumefika huko kazi ipo, na wale walioana mkristo na muislamu wafanyeje, acheni jamani mnataka kuleta mambo ya sudan kaskazin na kusini ss sijui ss watz wakristo watakuwa mikoa gani na waislamu watakuwa wapi, OOH LORD HAVE MERCY!
 
Taarifa ya habari ya ITV saa mbili imeonyesha tamko Rasmi la Bakwata kuwataka waislam wa Igunga wasimpigie kura mgombea wa chadema.Nimepata mshtuko mkubwa na kuona taifa letu sasa linaangamia.Hivi ni halali kwa mujibu wa sheria za uchaguzi dini kutangaza rasmi chama fulani kisipigiwe kura? Watu wote wapenda haki demokrasia na amani walaani tamko hili haramu.

Ningependa mashehe watoe tafsiri sahihi la vazi la hijab ambalo limepelekea haya yote kutokea. Hii itasaidia kujua kweli DC alivuliwa hijab au ushungi.
 
Nawapongeza sana waislamu! Huu ni uamuzi wa kishujaa sana. Hawa chadema na wapenzi wao wanawadharau sana waislamu. Me nawashauri waislamu wote wenye kadi za uanachama za chadema wazirudishe and wajiunge na chama kingine

Upo mwenyewe kwenye mawazo mgando yako
 
Taarifa ya habari ya ITV saa mbili imeonyesha tamko Rasmi la Bakwata kuwataka waislam wa Igunga wasimpigie kura mgombea wa chadema.Nimepata mshtuko mkubwa na kuona taifa letu sasa linaangamia.Hivi ni halali kwa mujibu wa sheria za uchaguzi dini kutangaza rasmi chama fulani kisipigiwe kura? Watu wote wapenda haki demokrasia na amani walaani tamko hili haramu.

NI sawa kabisa kuwalaumu hawa waliotoa tamko.
Lakini kwa namna ya pakee mimi natoa lawama zangu kwa wamiliki wa vyombo vya habari, mana hao ndio wanakoleza huu moto.
Hivi chombo kama ITV au vingine visivyo na mlengo wa kidini kwa nini wanatoa nafasi kwa matamko ya Kidini?
Kama nchi yetu inasema haina dini nadhani vyombo vyote vya kitaifa ambavyo sio vya kidini inabidi kupigwa marufuku kutoa habari zenye mlengo wa kidini.
Mimi naamini kasa game hii inachezwa na CCM, hasa viongozi wake wa juu wakiwashirikisha wenye vyombo vya habari.
Haiwezekani ITV, au Mwananchi watoe habari kwa uzito huo kuwa waislamu waaswa wasimchangue mtu wa Chadema.... hapa kuna walakini.
Pia sina uhakika kwa hivi vyombo vinajua maudhui yao....narudia sio sahihi kwa vyombo vya kitaifa kutoa habari yeyote ile yenye mlengo wa kidini, kikabila etc mana ndio wanachochea mgawanyo.
Siku hizi kila dini wana vyombo vyao vya habari, basi waachiwe huko na vyombo vya kitaifa viepushane na hizi propaganda!
 
Hawa mashekhe wanatumiwa kwa njaa zao, mbona hawajalaani CCM na kada wao aliyefumaniwa na mke wa tu Igunga???lipi kubwa kumvua mtu hijab au kutembea na mke wa mtu????ndio hapo viongoz wa din yangu ninapowatoaga maana.
 
viumbe wote mungu katupatia akili, isipokuwa binadamu aliongezewa hekima, busara pamoja na utashi, basi binadamu anapokosa hivi vitu vitatu huwa na akili tu.
Unapokuwa na akili tu matokeo ni :fencing: na mwisho wa ni :confused2:
 
CHONDE TAASISI ZINAZOTUONGOZAA KIDINI NCHINI ZISIWE ZIKIKIMBILIA SANA KWENYE KIOO KUTEKELEZA MATAKWAA YA WANASISA WAASIOAMINIKA KATIKA JAMII

Ama kweli ajizi nyumba ya njaa; CCM kumbe walikua wamewaingiza porini kabisa baadhi ya ndugu zetu Waislamu kwa taarifa za uongo kama hivi???

Kwa kweli sikujua kwamba ni yule yule mama Kimario jirani yetu kule Mbezi ndiye aliyekua akizungumziwa muda wote. Jamani yule mama wala si Muislamu ni mkristo safi tena Mzee wa Kanisa pale Wazo, duuuhh hawa jamaa jamani!!!!!!

JF team tayari ilishazuru kule kwenye shamba lake la pili kule Tegeta na picha zote za shamba lake tayari ziko hewani JF kusaidia kuthibitisha ukweli kwamba kasingiziwa na CCM taarifa hizo hapo juu.

Mpaka hapa sasa sijui kwamba BAKWATA watalazimika kuitisha mkutano mwingine kukana taarifa zao za awali juu ya huyu mama. Jamani
si kila Fatuma ni Muislamu WAKATI MWINGINE NI JINA TU LA UKOO hivyo kukimbilia kutolea tamko hata mtandio tu wa urembo mtu eti ni hijabu ni makosa sana tu.

Hijabu sisi sote tunaifahamu na kuiheshimu sana; kwa kawaida hutanda kichwani hadi miguuni tena kushitiri mwili mzima sembuse kale ka ulimi wa ng'ombe aliojitupia Mama Kimario kuwahi kwenye kutengeneza misheni za kura zisizoibika Igunga???????????
 
Hii habari kwa kweli ni ya kusikitisha na kukatisha tamaa kwa mustakabali mwema wa nchi yetu.

Binafsi nimekerwa sana na hawa BAKWATA ku stoop so low, na kujipendekeza kwa chama fulani kiasi hiki.

Naamini waislam wa Igunga ni werevu kuliko BAKWATA inavyodhani, na kamwe hawatapiga kura kwa maagizo
ya BAKWATA, bali kwa kufuata sera zinazotekelezeka kwa mgombea watayeona anawafaa kwa mazingira ya Igunga.

BAKWATA iache kutumika kisiasa... hii ni aibu, aibu, aibu yenu BAKWATA. Bahati nzuri BAKWATA sio kama TEC, no sane
muslim ever cares to listen about what opinion they have. Its just a bunch puppets trying too hard to impress their master.
 
MIKURUPUKO YA BAKWATA NA USHABIKI WAKE KISIASA NCHINI HUENDA UKAZAA TAASISI NYINGINE IMARA ZAIDI KUJUMUISHA WAISLAMU WA MATABAKA YOTE NCHINI

Wala haikua lazima kiasi hicho kwa taasisi hii ya BAKWATA kudhaalilisha Uislamu nchini kwa kukurupukia tu matukio bila hata kuyatthmini kiundani kwanza.

Kuna uwezekano Wanaharakati maarufu kama Sheikh Ponda Issa Ponda na wengine wengi tu wakapinga vikali mno hii taabia ya hivi karibuni ya baadhi ya BAKWATA kuligeuza KIMBILIO LA CCM wakati wa shida za kukataliwa kisiasa.

BAKWATA na mikurupuko yake ya kuaibisha Waislamu SAFI nchini kama vile kwa huyu Mzee wa Kanisa Katoloki pale Wazo-Tegeta, Mama Fatuma Joseph Kimario, huenda ikageuka BOMU LA HATARI sana kuliangamiza taasisi hii tuliokua tukiiheshimu saana nchini.

Kwa kweli pengine taasisi nyingine ya maana zaidi na yenye Uwakilishi wa kweli wa WAUMINI WA KIISLAMU (wala si CCM) nchini huenda ikaibuka na kuungwa mkono kuchukua nafasi yake hivi karibuni.

Hii habari kwa kweli ni ya kusikitisha na kukatisha tamaa kwa mustakabali mwema wa nchi yetu.

Binafsi nimekerwa sana na hawa BAKWATA ku stoop so low, na kujipendekeza kwa chama fulani kiasi hiki.

Naamini waislam wa Igunga ni werevu kuliko BAKWATA inavyodhani, na kamwe hawatapiga kura kwa maagizo
ya BAKWATA, bali kwa kufuata sera zinazotekelezeka kwa mgombea watayeona anawafaa kwa mazingira ya Igunga.

BAKWATA iache kutumika kisiasa... hii ni aibu, aibu, aibu yenu BAKWATA. Bahati nzuri BAKWATA sio kama TEC, no sane
muslim ever cares to listen about what opinion they have. Its just a bunch puppets trying too hard to impress their master.
 
MIKURUPUKO YA BAKWATA NA USHABIKI WAKE KISIASA NCHINI HUENDA UKAZAA TAASISI NYINGINE IMARA ZAIDI KUJUMUISHA WAISLAMU WA MATABAKA YOTE NCHINI

Wala haikua lazima kiasi hicho kwa taasisi hii ya BAKWATA kudhaalilisha Uislamu nchini kwa kukurupukia tu matukio bila hata kuyatthmini kiundani kwanza.

Kuna uwezekano Wanaharakati maarufu kama Sheikh Ponda Issa Ponda na wengine wengi tu wakapinga vikali mno hii taabia ya hivi karibuni ya baadhi ya BAKWATA kuligeuza KIMBILIO LA CCM wakati wa shida za kukataliwa kisiasa.

BAKWATA na mikurupuko yake ya kuaibisha Waislamu SAFI nchini kama vile kwa huyu Mzee wa Kanisa Katoloki pale Wazo-Tegeta, Mama Fatuma Joseph Kimario, huenda ikageuka BOMU LA HATARI sana kuliangamiza taasisi hii tuliokua tukiiheshimu saana nchini.

Kwa kweli pengine taasisi nyingine ya maana zaidi na yenye Uwakilishi wa kweli wa WAUMINI WA KIISLAMU (wala si CCM) nchini huenda ikaibuka na kuungwa mkono kuchukua nafasi yake hivi karibuni.
 
Ina maana huyo muhuni anayetumia mwavuli wa dini kutukaribishia machafuko bado hajakamatwa?
Kwani ni mgombea gani muislam wanayemtetea kama sio uhuni wa CCM.
 
Huyo ustaghi angejaribu kutamka hayo maneno huku kwetu Pemba nadhani asingetoka msikitini salama,kwani 90%ni againist CCM.
 
Hii ndio mbegu ambayo kikwete amepigania sana kuipanda ''UDINI''sasa imekamilika kupitia kwa hawa waislam wa igunga,ccm inaomba kura za huruma na giriba kwa waislam nao wanakubali na kwa sababu waislam waliowengi uwezo wao wa kufikiri ni mdogo wanakubali kubuluzwa wacha iwe hivyo lakini baadae wasije walaumu wakristo na CDM isiseme chochote iendelee na kampeni zake.
 
kumbe mnajua waislam ni wachache sasa wasiwasi wanini hata nyie si mulimchagua slaa na mlijua hatashinda si mumesema wakristo mko wengi nyie mulianza sisi tunamalizia subirini maaskofu wawapigie debe kama sakata la madiwani waislam tunapiga kura kwa malengo hatakama tutakae mchagua hatashinda lengo ni kumridhisha mungu sio makengeza mbowe

kwa hili ndugu unakosea tufikie sehemu tuipende tanzania yetu kuliko cdm/ccm/cuf vyote vitapita lakin TZ ITABAKI,madhara tuyatendenenezao kwa njaa zetu ni makubwa mno tunaishi kwa kuchangamana wenye dini na wasio nazo tunako kwenda tutaanza ulizana ww dini gani msikiti gan nk which is na gud
 
WADAU NIMEPITA BANDIKO LA uwezo tunao ANASEMA MH F KIMARIO NI MKATOLIKI,MWENYE KUMFAHAM KWA UNDANI ATUJUZE TUJUE
 
[h=3][FONT=d742ee695d1fc218051bb8d8#1c0400]Mkanganyiko Wa Leo: Nini Tofauti Ya Hijab Na Mtandio?![/FONT][/h]Posted by Mjengwa |


Tafsiri Ya Hijab Yavunja Mkutano Wa Bakwata Igunga
Linaandika gazeti Mwananchi....


'Vazi la hijab' jana lilivunja Mkutano wa Bakwata na waandishi wa
habari baada ya baadhi ya viongozi wa Baraza hilo Kuu la
Waislamu,kushindwa kueleza maana yake.

Mkutano huo uliitishwa na Katibu wa Bakwata Wilaya Igunga, Maulid
Athman Mussa ambaye alitoa tamko la kukilalamikia Chadema kwamba
kiliudhalilisha uislamu katika sakatabaina ya cahama hicho na Mkuu wa
Wilaya ya Igunga, Fatma Kimario.

Kuvunjika kwa mkutano huo kulitokana na maswali yaliyo ulizwakwamba
vazi la hijabu linalodaiwa kudhalilisha dini hiyo inabidi liweje,
hivyo viongozi hao kupandwa na jazba.
Maswali hayo yalionekana kuwachanganya na kuwapandisha jazba viongozi
hao, lakini wakijitahidi kutoa ufafanuzi ingawa wao wenyewe
walionekana kupishana kauli.

Shehe wa wilaya, Ally Rage alisema, hijabu inanatakiwa isitiri mwili
wote wa mwanamke wa kiislamu na kuacha tusehemu ya uso wake ndio
ionekane. Ufafanuzi huo ulionekana kushahibiana na wa mwanamke mmoja
wa Kiislamu aliyekuwepo ndani yamkutano huo, Amina Billal aliyekuwa
amevaa Hijabu aliyesema ni lazima lifunike miguu na mikono.

"Hijabu ni vazi la mwanamke wa Kiislamu linalositiri mwili ambalo
akivaa nguo yenye mikono mirefu ni lazima liwerefu hadi chini,"alisema
Amina na kuwaonyesha wanahabari vazi lakelilikuwa limefunika mikono na
miguu.
Kutokana na maelezohayo, waandishi wa habari waliwataka viongozi hao
watazame picha za tukio la Chadema na Kimario katika gazetimoja
walilokuwa nalo meza kuu (sio Mwananchi) na waeleze kama DC alivaa
hijabu au mtandio.

Hata hivyo, katika kujibu maswali hayo, kiongozi mmoja alitumia aya za
kitabu kitakatifu cha Quaran akisema Hijabu lazima lifunikenywele kwa
vile ni haramu mwanamke wa Kiislamu kuonekana nywele zake. Majibu
hayo bado yalionekana kujichanga zaidi na kushindwa kufafanuakama mkuu
huyo wa wilaya alikuwa amevaa jijabu au mtandio hali iliyomsukuma
Imamuwa msikiti huo, Swalehe Hamisi kufafanua zaidi.

Imamu alisema vazi la hijabu liko katika aina tatu moja likiwani lile
lililokuwa likivaliwa na wake zamtume Mohamed ambalo lilikuwa
likifunika maeneo yote ya mwili bila kuacha sehemu moja ya mwili
inayoonekana.
"Vazi la pili la mwanamke wa Kiislamu ni lile lilokuwa likivaliwa na
wafanyakazi kwa maana ya wakulima ambalo lilikuwa likimsitiri mwanamke
mwili wote isipokuwa sehemu ya usoni tu,"alisema. Alifafanua hijabu
ya tatu, Imamu huyo alisema ni vazi ambalo linamfanya mwanamke asiwe
amejisetiri mwili wote na kwamba vazi hilo linamruhusumwanamke huyo
kusogelewa tu na ndugu wa damu na simtu mwingine.

"Hawa Chadema waowalienda kumwondolea hijabu mwanamke wa Kiislamu
ambaye hawajazaliwa naye tumbo moja na sio ndugu zake
kabisa…hawakupaswa kumsogelea kabisa DC,"alisema Imamu huyo. Pamoja
na ufafanuzi huo, waandishi wa habari waliendelea kuwabana viongozi
hao watoe ufafanuzi wakiegemea katika kitabu cha Quoran kwamba
kinaeleza nini kuhusu hijab jambo ambalo liliwaudhi.

Chanzo. Mwananchi.
 
Back
Top Bottom