DALA
JF-Expert Member
- Aug 24, 2009
- 2,259
- 4,690
dah umeongea kitu kizito sana mkuu yani umenifanya nitoe machozi
Nimekuwa muhanga wa hilo jambo kama ilo nilipishana na lecturer kauli wakati nadai haki yangu badala yake alinifanyia visa mpaka akanidisco kwa ajili ya somo lake tu na maisha yangu yote ya chuo sikuwahi pata sup zaidi ya iyo moja ya huyo jamaa ambayo mwisho wake ilinifanya nidisco
Huwa naumia sana nikimkumbuka jamaa ila ninachomshukuru mungu sikukataa tamaa na sasa ninasonga mbele
Mi niliamua kuachana nae tu kwa sababu nilikuwa siwezi kabisa eleza popote nilijawa na hisira nilikua najikuta nalia tu badala ya kueleza shida yangu kwenye mamlaka husikaa kwa kwel iliniumiza sana mwishowe nikaamua ondoka tu na kuachana kabisa na ilo jambo mana nilihisi kabisa naweza kufa mana hayo ndo mawazo pekee yaliyoutawala moyo wangu kwa kipindi kile, na hapo kumbuka nilikuwa nimeshamaliza semister yangu ya mwisho ya mwaka wa tatu.
Ila kiukwel nashindwa kabisa msamehe mshikaji moyo wangu umejawa na kisasi juu yake huwa naomba mungu anisaidie niweze msamehe lakin kibinadamu siwezi kabisaa
Pole sana mkuu ila binafsi ninaamini maisha siyo elimu tu. You can make life better even if you don't have the papers.
Ushauri wangu kwako ni umsamehe na umwachie kwani moyo utakuwa na amani zaidi ya unavyodhani