Bwana Nasami. Waambie hao wanawake unaosema wanaonewa na kunyanyaswa na wahadhiri, wajitokeze, watetee haki zao. Kwani sheria ipo upande wao. Kama kweli wamenyimwa alama katika mitihani na majaribio kwa sababu za kingono, wana uhakika kuwa walifanya vizuri mitihani yao, walihudhuria madarasa bila tatizo, hawajaruka kufanya majaribio hata mara moja, waelekeze sasa waende kwa dean of students, wakitoka hapo wakajaze fomu za kukata rufaa na nakuhakikishia watafaulu, na wahadhiri wataumbuja na kuchkuliwa hatua. Lakini kama hao mabinti ni wale wale, wategemea huruma na miili yao, wasijaribu hilo, kwani wataonekana hawafai hata kuwepo chuoni. Kwa uzoefu wangu, hakuna mwanamke mwenye akili za kutosha darasani aliyeiosa alama zake za masomo kwa sababu za mizengwe ya wahadhiri.