Uchumi ni nini?

stakehigh

JF-Expert Member
Aug 9, 2019
6,385
3,494
  • Uchumi ni nini?
  • Uchumi ni jumla ya shughuli zote za binadamu zinazolenga kutosheleza mahitaji yao. Ni hasa uzalishaji, usambazaji na utumiaji wa bidhaa pamoja na kutolewa kwa huduma kwa njia mbalimbali.
  • Uchumi mara nyingi hutazamwa kwenye ngazi za kijiji, eneo, taifa au dunia.
  • Sayansi ya Uchumi (kwa Kiingereza economics) ni tawi la elimu inayochunguza masharti ya uchumi kufaulu au kushindwa.
Baada ya kujua uchumi haswa ni nini, basi niende moja kwa moja kwenye mada. Kuna units ama njia mbalimbali za kupima ukuaji wa uchumi lakini mara nyingi hua hazina uhalisia kwa mtu wa kawaida kwa sababu ya siasa huambatana na data za uchumi, wanasiasa wanatumia uwanja huu wa wananchi kutoelewa uchumi ili kujipatia political gain, kwa manufaa yao na kuacha mwananchi akiwa katika sintofahamu ya nini kinaendelea. Uchumi ni mpana sana lakini nitumie hii nafasi hii kuelezea upande unaomgusa mwananchi kabisa
  • Uchumi unaendeshwa na kitu kinaitwa (TRANSACTION) au kwa lugha rahisi mwamala, kwa kawaida hakunaga kitu kama uchumi upo vibaya ama uchumi vizuri, ukiona pesa zmepotea kwenye mfuko wako basi kwa haraka unatakiwa kujua kuna mtu/watu ameacha kufanya spending kwenye budget yake ya kila sku, na wewe ukiona kuna hela haikufikii basi na wewe kuna huduma unazikata haraka haraka na anaekutegemea kwa namna moja nae anapata joto la uchumi
Transactions znahusiana vp na mimi?
  • Unapoenda kununua kitu chochote unabadilishana pesa na huduma ama bidhaa , kila dakika nchi nzima hiki ndo kinachofanyika, sasa kila mtu akiwa anafanya transaction pesa inakua kwenye mzunguko na unaweza tumia end point yoyote kujipatia pesa, tatizo la mfumo huu ni kwamba unapopata pesa lazima na wewe upitishe kwa mtu mwingine, ni tafauti kwenye uchumi mdogo! Nchi zenye uchumi mkubwa duniani pesa zinatembea sana , (with bonus ya high value currency), mfano nchi kama marekani $100 znatembea sana lakini hio noti bado ina thamani kubwa! Anyway ni nje ya topic, Basi kila mtu akiwa anafanya transactions serikali inauwezo wa kutap pesa kwa kuzidumbukiza kwenye miradi mipya ambayo ikasababisha pesa pia kusogea na kuzunguka zaidi, hio ndo maaana ya transaction kwako! Ili kuweza kufika hatua hii inabidi nchi iwe productive(uzalishaji), endapo wananchi watakua productive wengi basi economy inakua kwenye mstari wa kupanda always bila shuka, kwa lugha nyepesi ni hivi
  • _qHQP3__uwl5Qx--QZCN8lMjXerYDnBSFu5MXSLr5Jr8kItwxV6yJbqT6rVkifF9czughg46Bz1bdsSMGR6nas2lNTS4VTBK8MwM5Jbwy7IuVYs7Mr6P4UmIXrsjDSZPBiJ99iNf
  • Nchi ikiweza kupata ukuaji huu basi serikali itafanya kazi kwa ufanisi mkubwa katika makusanyo ya kodi, lakini kibaya ni kwamba hakuna nchi yoyote yenye productivity kama hio, basi serikali inashindwa kua na constant supply of cash kwa sababu kuna watu wanaofanya kazi sana, na kuna wengine ambao ni wavivu, upatikanaji wa mapato pia unakua mdogo na huduma mpya znaanzishwa kwa taratibu sana! Lakini kwa kua pesa za dunia ni karatasi plain, ili kufidia watu ambao hawana spidi hio serikali inaweza kukopa kufidia ukuaji mdogo wa uchumi kwa wananchi.

  • Lakini kuna tatizo kwenye hili jambo, ukikopa ina maaana lazima ulipe na kwa riba, ina maaana kipindi serikali inapokea hio hela, na kudumbukiza kwenye huduma za kijamii kunakua na pesa nyingi zilizojazwa kwenye mzunguko bila uwiano wa uzalishaji, lakini pia kuna kitengo kinaitwa (BENKI KUU) wao wakiona uchumi unazidi kua dim and slower wanapunguza interest rate kwenye mabenki na watu wengi zaidi wanaenda kukopa, ukijumlisha serikali + mikopo ya mashirika na watu binafasi kwenye mabenki basi watu wanaona uchumi unaenda sawa kwa sababu kila kitu wanachotaka wanakipata! Hakuna wa kuuliza kwa sababu serikali na mabenki wamemwaga pesa nyingi kwa wananchi, hii inaitwa (BOOM) everyone feels rich, u can buy anything and spend anywhere, hata zile huduma ulikua unasita kwenda kwa sababu ulikua unaona znatumia mapato yako na hazina umuhimu unaanza kurudi sehem kama hizi, kwa lugha rahisi kila mtu anakua tajiri mpaka yule mwenye huduma ya kawaida,

  • Hiki ndicho wananchi hua wanalilia kila sku uchumi uwe ivi, lakni hii ni hatari, kuna kundi la watu wanaitwa wafanya biashara endapo wataona wateja wana uwezo sana basi wao hupandisha bei ya bidhaa na huduma, ili kuhakikisha hatufiki uku BOT lazima wapandishe interest rate (RIBA): Lakini pia unatakiwa kujua inapofika kipindi pesa zpo nyingi kuliko huduma unazotaka kitalaamu tunaiita (INFLATION), situation hii husababisha pesa nyingi kutokua na thamani, sasa BOT kuona hili hua wanaongeza interest rates, sasa hapa ndo tatizo linapotokea
Kwanza wananchi hawataki tena kukopa kwa sababu rates zko juu, na wale waliokopa sasa wanatakiwa kurudisha pesa walizokopa, hapa ndo tunapaita kufunga mkanda! Zile huduma ambazo sio za muhimu basi unakua huzihitaji lakini hzi huduma pia zilikua na watu wanaziendesha na wanategemea kutoka kwako, basi biashara yake inakufa na wewe unatakiwa kufunga mkanda zaidi, kwa kua rates zmekua kubwa sana the other option imebaki inaitwa (DEFAULT) sasa hapa ndo watu wanakuja kujua kwamba vyote walivokua navyo wakidhan ni pesa kumbe hazikua pesa( mtu anaweza kuuza nyumba yake ama benki kuchukua mali zake ikiwemo nyumba pia), kama ulikopa ili ununue nyumba ama gari basi inakua ni mda wako kwa kwenda ndan zaidi kulipa kwa sababu ulitumia pesa ambayo hauna, kipindi kama hki ndo wananchi huanzisha maandamano ama vurugu za apa na pale ikiwemo maandamano situation kama hii inaitwa (DEFLATION) , nkimaanisha hauna pesa lakini kuna huduma zako zinazohitaji pesa, hatua zingine ni kama watu kupunguzwa ofisini ama biashara kufungwa kabisa! Hatua hii amra nyingi default hua ndo suluhisho lakini sasa kila mtu amefunga mkanda na malipo yamefanyika bila cash, watu wameuza ama kuchukuliwa nyumba zao na mabenki ama biashara zao pia kwa kushindwa kulipa! Tatizo lingine ni kwamba wananchi wakijua kwamba haya yanatokea basi na wao hukimbia kutoa pesa zao zote kwenye mabenki, basi benki nazo hupitia katika hali hio! Kwenye hatua hii hauezi tena kushusha rates kwa sababu watu wamedefault kwenye nyumba zao ama biashara zao, kuna masuluhisho matatu apa, kwanza serikali inaweza kuwakaba matajiri kwa kuwapandishia kodi (ambayo ni ngumu), 2 (kukata madeni yote waliopo ama kupunguza kiasi anachotakiwa kulipa mtu) (ambayo pia ni ngumu) suluhisho la mwisho ni kuchapisha pesa mpya! Ambayo ndo linafanyika sana
  • Kwanini natakiwa kujua haya yote?
Kwanza kabisa uchumi wa nchi yoyote una majira na ni vema kujua haya yote yatakusaidia katika kufanya maamuzi yanayohusu maisha yako! Watu wengi hupiga sana kelele serikalini ila ni kwa sababu hawana uelewa wa yote haya na hawakufanya maamuzi sahihi
= mimi sio mwandishi mzuri ila elimu hii ni muhimu kwa wote kuijua
 
Sawa,

Noted kwamba ktk Nchi yyte uchumi huwa na majira yake.
 
Back
Top Bottom