Uchumba wa muda mrefu umenichosha

Uchumba wa muda mrefu umenichosha

Kama mnaishi pamoja tatzo huanzia hapo, kuna wengine wamebariki ndoa juz wamekaa uchumba miaka 30. Wana wajukuu sasa, ila yako inanitsha maana hataki hata mpate na watoto, hii ni changamoto sasa.

Vp wazazi wako wanasemaje katika hilo?! Na ww unaonaje!? Maana kisheria mkishaishi miez mitatu mshakuwa mke na mume, muda mwingine tunafanya mambo yawe magumu mnaishi wote kama mke na mume na bado anakuambia ajajipanga mnh! Inafkirisha.
 
Binafsi niko kwenye uchumba tangu mwaka 2014. Ninahudumiwa kila kitu.

Kuanzia kula, kuvaa, matembezi na hata mitoko mbalimbali. Tatizo nikimgusia suala la ndoa, anasema tujipange kwanza.

Tujipange mwaka wa 11 huu? Na hata mtoto hatujazaa? Kuna dalili ya ndoa kweli hapa? Nimechunguza kila mahala, kiukweli hana mtoto wala mwanamke mwingine, ila kwanini uchumba umekuwa mrefu hivi?

Wenzangu mlioolewa mlifanyaje mpaka ndoa zenu zikafungwa mapema? Naombeni mbinu mlizotumia ili na mimi niweze kuzitumia katika mahusiano yangu.

Mbarikiwe na muwe na asubuhi njema.
Nusratt Mohamed.
Ila mnatuchanganya, kule umesema ulikuwa unajiuza, huku tena.. aargh!
 
Back
Top Bottom