ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,018
- 7,222
Gazeti la Mtanzania leo hii limetoa habari hii:
Source: http://www.wavuti.co
My take: Hawa madaktari "uchekibobu" ndio unaowaponza. Wanaongea vitu kama viajna wa kijiweni vile!
1. Chitage ananukuliwa akisema hali ya Rais wa MAT kufikishwa mahakamani imewashtua! Hivi huyu Chitage hajui kuwa Rais wa MAT alipewa amri na mahakama? Ukipewa amri na mahakama una options mbili, aidha kuitekeleza au kuiambia mahakama kuwa hujaridhika na amri hiyo. Huyo Rais wa MAT alifanya chochote kati ya hivyo? Yeye amepewa amri ya mahakama akaifungia sandukuni na kuendelea na shughuli zake za kichekibobu. Sasa kinachowashtua ni nini?
2. Chitage ananukuliwa akisema swala la interns kufutiwa usajiri halijawashtua kwa sababu walilitegemea! Wakati huohuo anasema viongozi wa interns wanajadiliana na mwanasheria na baada ya majadiliano hayo ndipo Chitage na wenzake waangalie nini cha kufanya. Sasa Chitage kama walishalitegemea hilo, kwanini majadiliano na mwanasheria yanafanyika mpaka baada ya leseni kufutwa? Chitage haoni kuwa anawachelewesha vijana wa internship katika safari yao ya kupata usajiri wa kudumu kwa sababu yeye ana mipango mingine ya maisha! Lakini najiuliza hawa kina Chitage kwanini swala la interns wanawaachia viongozi wa interns? kwa nini wasilisimamie wao kama viongozi wa madaktari? Huu uchekibobu utawaponza vijana wasio na hatia.
3. Chitage ananukuliwa akisema madaktari wanafanya kazi lakini hawana moyo wa kufanya hiyo kazi. Hivi huyu Chitage ni lini alikuja kuuambia umma kuwa mgomo umeisha? Kwa lugha nyingine ni kwamba mgomo ulioitishwa na kina Chitage umekataliwa na madaktari na Chitage na wenzake wanaona haya kusema ukweli kuwa mpango wao wa kuivuruga nchi umekwama. Labda tumuulize Chitage amejuaje kuwa madaktari hawana ari ya kuwatibu watanzania wenzao. Yeye Chitage kama kagoma, anafuata nini maeneo ya kazi?
Nawashauri viongozi wa hospitali kuhakikisha machekibobu kama kina Chitage hawaruhusiwi kuingia katika sehemu za kazi. Wao waendelee kugoma na wawaache madaktari wanaotibia watanzania wenzao waendelee na shughuli zao. Wameshawaharibia vijana programs zao za internship sasa wanataka kuharibu na mengine. Hawa wakiachwa wanaweza kuwa radhi kuharibu hata hivyo vifaa vichache chakavu vilivyopo.
[h=2]Dkt. Chitage azungumzia Dkt. Namala kushitakiwa; Interns kufutiwa leseni; Hali ya Dkt. Ulimboka[/h]12/07/2012 Siku moja baada ya Rais wa MAT, Dk. Namala Mkopi kufikishwa mahakamani kwa madai ya kuchochea mgomo, Katibu wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dkt. Edwin Chitage amesema hali hiyo imewashitua na lolote linaweza kutokea. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Dkt. Chitage alisema hali hiyo imeongeza hasira na kushusha morali wa Madaktari, Kweli hiki kitendo cha Dkt. Mkopi kufikishwa Mahakamani kimetushtua na ukweli kimesababisha kuwepo na fukuto la chini chini. Madaktari wamekatishwa tamaa lakini kitendo hiki pia kimeshusha morali ya wale ambao walirudi kazini kwa hiyo wapo Madaktari ambao wapo kazini, kwa maana ya eneo la kazi lakini wanachokifanya hiyo wanajua wao,alisema Chitage. Akizungumzia suala la madaktari wa walioko katika mafunzo (Interns) 390 kufutiwa leseni alisema, kitendo hicho kilitegemewa na hakikuwashitua kwa sababu ni kitu ambacho tayari kilipangwa. Kwetu sisi tulitegemea jambo hilo kwa hiyo hatukushtuka sana kwetu hiki ni kitu kidogo sana, kwa sasa viongozi wa Interns wanafanya kikao na wanasheria wao wanaangalia jinsi uamuzi huo ulivyotolewa na baadaye tutakutana nao kwa ajili ya kuangalia ni namna gani tutalifanyia katika suala hili,alisema Dkt. Chitage. Akizungumzia hali ya Dkt.Stephen Ulimboka alisema kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na ameanza kutembea na kufanya mazoezi vizuri, Hivi sasa hali yake imeanza kuimarika. Anaweza kutembea na anafanya mazoezi yake vizuri. Kinachoendelea kumkalisha hospitali ni uangalizi wa karibu wa figo lakini ingekua si figo angekuwa amesharudi nchini, alisema. |
Source: http://www.wavuti.co
My take: Hawa madaktari "uchekibobu" ndio unaowaponza. Wanaongea vitu kama viajna wa kijiweni vile!
1. Chitage ananukuliwa akisema hali ya Rais wa MAT kufikishwa mahakamani imewashtua! Hivi huyu Chitage hajui kuwa Rais wa MAT alipewa amri na mahakama? Ukipewa amri na mahakama una options mbili, aidha kuitekeleza au kuiambia mahakama kuwa hujaridhika na amri hiyo. Huyo Rais wa MAT alifanya chochote kati ya hivyo? Yeye amepewa amri ya mahakama akaifungia sandukuni na kuendelea na shughuli zake za kichekibobu. Sasa kinachowashtua ni nini?
2. Chitage ananukuliwa akisema swala la interns kufutiwa usajiri halijawashtua kwa sababu walilitegemea! Wakati huohuo anasema viongozi wa interns wanajadiliana na mwanasheria na baada ya majadiliano hayo ndipo Chitage na wenzake waangalie nini cha kufanya. Sasa Chitage kama walishalitegemea hilo, kwanini majadiliano na mwanasheria yanafanyika mpaka baada ya leseni kufutwa? Chitage haoni kuwa anawachelewesha vijana wa internship katika safari yao ya kupata usajiri wa kudumu kwa sababu yeye ana mipango mingine ya maisha! Lakini najiuliza hawa kina Chitage kwanini swala la interns wanawaachia viongozi wa interns? kwa nini wasilisimamie wao kama viongozi wa madaktari? Huu uchekibobu utawaponza vijana wasio na hatia.
3. Chitage ananukuliwa akisema madaktari wanafanya kazi lakini hawana moyo wa kufanya hiyo kazi. Hivi huyu Chitage ni lini alikuja kuuambia umma kuwa mgomo umeisha? Kwa lugha nyingine ni kwamba mgomo ulioitishwa na kina Chitage umekataliwa na madaktari na Chitage na wenzake wanaona haya kusema ukweli kuwa mpango wao wa kuivuruga nchi umekwama. Labda tumuulize Chitage amejuaje kuwa madaktari hawana ari ya kuwatibu watanzania wenzao. Yeye Chitage kama kagoma, anafuata nini maeneo ya kazi?
Nawashauri viongozi wa hospitali kuhakikisha machekibobu kama kina Chitage hawaruhusiwi kuingia katika sehemu za kazi. Wao waendelee kugoma na wawaache madaktari wanaotibia watanzania wenzao waendelee na shughuli zao. Wameshawaharibia vijana programs zao za internship sasa wanataka kuharibu na mengine. Hawa wakiachwa wanaweza kuwa radhi kuharibu hata hivyo vifaa vichache chakavu vilivyopo.