Uchakachuaji wa Ting na Startimes kwa njia ya satellite

wadau nilitoa suala moja hapo juu kua hili suala linawezekana kuna watu wakaanza kunidis kiukweli nilimaind kwani hapa tunajifunza ili nasi tuweze kuendelea kutengeneza vitu vyetu wenyewe na huku ndo kunaonyesha kukua kwa techno,hata wachina waliaanza na vitu km hivi ndomana wapo hapo walipo,mfn ndomana kuna watu wanatengeneza virus ili wapate hela zakuuza antivirus,vyote hivyo ni maujanja,there4 sis kuchakachua vingamuzi hatukosei kwani tunaonyesha kukua kwa techno,nitaendelea kuwapa ujanja vizuri khs hili suala subirini nipate muda mzuri wakuandika na kupost enough material na yakueleweka,ndo naandaa hii elimu vizuri,subirini
 
wadau nilitoa suala moja hapo juu kua hili suala linawezekana kuna watu wakaanza kunidis kiukweli nilimaind kwani hapa tunajifunza ili nasi tuweze kuendelea kutengeneza vitu vyetu wenyewe na huku ndo kunaonyesha kukua kwa techno,hata wachina waliaanza na vitu km hivi ndomana wapo hapo walipo,mfn ndomana kuna watu wanatengeneza virus ili wapate hela zakuuza antivirus,vyote hivyo ni maujanja,there4 sis kuchakachua vingamuzi hatukosei kwani tunaonyesha kukua kwa techno,nitaendelea kuwapa ujanja vizuri khs hili suala subirini nipate muda mzuri wakuandika na kupost enough material na yakueleweka,ndo naandaa hii elimu vizuri,subirini
Mkuu, wasikukatishe tamaa hao tunaomba utupatie maujanja pls.
 
Du!
Guys, give a break to these companies!...watalipanaje mishahara sasa?

Anawaza atatoboaje katikati ya msitu wa PIPOZ PAWA

Kweli Tanganyika tuna madudu haiwezekani tatizo la televisheni ya taifa lighalimu miezi yote hiyo bila matengenezo.Kama hawa hawataki tupate habari kuhusu nchi yetu wahamishie matangazo yao Aljeezra ili tuwe tunapata taarifa za nchi yetu bila usumbufu wowote kama ni spea alitumwa mtu akainunue watutangazie kuwa amekula nayo kona Haiwezekani miezi takribani 6 sasa inatusumbua why!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Tanzaniaaaaaaaa????????


Hawa ndio wanaotaka kuja kushika serikali mbona tutakoma!
 
nimeona hichi kitu lakini sikielewi,Bravehost - sat keys viacsses

Jana nlijisikia vibaya kukosa mechi eti kama huna decoda ya ting huwezi kuangalia UEFA wakati ATN ndo walokuwa wanarusha
pia KBC hawakuwa hewani kupitia STARTIME nlikasirika kwa sababu nimelipia ila sijaona gemu kama walivyonadi startime
 
Nimecheka sana, wezi watu waajabu sana lazima atafute kila sababu ili mradi aitulize nafsi yake kuwa analofanya ni safi! Mara mafisadi mara sio Watanzania, mara wanaweza kujiendesha kwa hela ya decoder tu! Utajiendesha vipi kwa hela ya decoder wakati license fees za programming (Series,Sports etc) inabidi ulipe kila mwezi? Au mwafikiri unarusha tu production za watu?

Kulipokuwa na DSTV tu watu walidai wananyonywa kwa sababu ya bei kubwa, sasa zimekuja hadi za buku 9 lakini kuiba tunataka! Kazi ipo hii nchi.

Anyway kwa kifupi kupata matangazo ya decoder bure itakuwa ngumu sana unless hawafuati standards au wanatumia encryption system ya zamani sana.
Maana watangazo yapo encrypted kisha decoder ndo inabeba keys na algorithm za ku-decrypt na keys zinakuwa update kupitia satellite signal, kwa hiyo ukiipata key itakuwa valid for a very short period.
Method za siku hizi za encryption kwa kifupi zipo secure, method mpya ya DSTV haijawahi kuchakachulika as far as I know.
Na ting na startimes kama kampuni mpya hawana sababu ya kutumia method za zamani.
 
We achana na hao ting kukukwamishia bori kupitia kbc1 kwa njia ya hayo matransmita yao kama una dish la cband au kuband ipate kbc1 live kwa njia ya satellite kwa parametre hizi 11026/9693 wanarusha UEFA live bila zengwe
 
We achana na hao ting kukukwamishia bori kupitia kbc1 kwa njia ya hayo matransmita yao kama una dish la cband au kuband ipate kbc1 live kwa njia ya satellite kwa parametre hizi 11026/9693 wanarusha UEFA live bila zengwe
Mkuu hebu fafanua zaidi, satellite ipi?.
 
aaaaa angalia sasa.
hili sio jukwaa la siasa na mambo ya kulipa kodi. thread imekuwa ndefu longo longo nyingi. hapa ni technology kwenda mbele. muhimu ni elimu . mie nipo hapa ku exchange elimu, kama mtu atachakachua au atalipa kodi hiyo ni juu yake.
technology forum ni kwa ajili ya ku exchange HOW TO........
somebody please delete those post zinoleta siasa huku. sio pahali pake. na zinanitia kichefu chefu
sasa ili ufaham njia ya uchakachuaji kuna thread maalumu nimeiandaa ambayo inatumika kuchakachua tv zote, popote duniani provided that some conditions are met.
thread yenyewe ni hiii
https://www.jamiiforums.com/tech-ga...m/136933-card-sharing-multichoice-africa.html
isome kwa makini fuata all links given kabla hujauliza swali jengine kwani ni kitu kipya kwa wabongo ila ni technique ambayo ipo for years now kule abroad.
kama una swali lolote ila baada ya kusoma thread kwa makini uliza kwenye thread huko huko. nimefanya commitment kuijibu hiyo thread kila swali litaloulizwa huko.

KIBURUDISHO weye uko wapi na hiyo satellite yako imeelekea upande gani. angle gani?
 
KBC1,K24,Family tv na WBS ya Uganda zinapatikana kwenye satellite ya NSS12 57.E ku-band njia mbili utakazotumia uzipate hizo chaneli.1 unatumia dish la ku-band 2 ambayo ni rahisi zaidi kama una dish hili la ft6 au ft8 la c-band unalotumia kupokea chaneli hizi za Tanzania palepale dish lilipo bila kulihamisha funga lnb ya ku-band kwenye hiyo plate iliyofungwa hiyo lnb ya c-band hesabu nyuzi 6 mbele ya hiyo lnb ya c-banb funga hapo iko fasta sana.Michuano yote inarusha kwa sababu yenyewe ndo chaneli mama kwenye startimes ya Kenya. ANGALIZO:Kama uko kusini mwa Tanzania kama huko Mtwara itakuzingua. Kama vp ni PM
 
Ni PM nikupe maujanja ya STAR TIMEuweze kupata more channels kwa single kick!
 
ngoja ukishafungua biashara yako sisi ndo tutakuja na njia ya kukuibia ili uone kuwa ni tamu au chungu
 
Jambo wote wanaJF leo nimekuja tofauti kidogo na wengine japo wote ni uchakachuaji ila kwa njia tofauti mbalimbali. Kwa wataalam wa JF hakuna mwenye ujuzi wa kuchakachua hawa jamaa wa startimes na ting kwenye decoda kwa njia ya satellite? Maana ukizisearch unazinasa ila zinakuwa zimefungwa kwa VIACSSES,BETACRYPT,IRDETO mwenye maujanja ya unlock code atasaidie!!!!!!!

Kifupi ni Kwamba HAIWEZEKANI. Ni sawa na Mtu kutaka kupokea Simu ya Mobile kwa Kutumia Redio ya Mkulima
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom