Maalim Seif ana siasa za jazba na chuki,
Maalim Seif anautaka urais wa Zanzibar kwa jazba, nguvu na usongo akiamini urais wa Zanzibar ni kama kitumbua chake alichopokwa kabla hakijaafika mdomoni ili hali ana njaa ya kufa mtu. Nadhani ni kweli siku zote anashinda uchaguzi Maalim ila nani atakubali kumpa urais mtu mshari mwenye kila dalili ya kulipiza kisasi na hata kuuvunja muungano hivyo hata akisimama mara mia hapewi dola ng'o labda adhikr ....
Tatizo jingine la Maalim Seeifu ni nasaba na sultan aliyepinduliwa,mpaka sasa mfadhili mkuu wa Maalim ni Sultan wa Brunei ndiye anayempa kiburi cha kuishi hotelini hapa bara kwa siku zote, sijui sasa. Sultani wa Brunei ni ukoo -ule ule wa Sultani wa Oman na ndio unaomgharimia Sultan wa mwisho aliyepinduliwa Zanzibar, Sultan Jamsed kuishi London mpaka sasa. Kwa vile Maalim ni ukoo huo, anahofiwa ataurudisha usultani na kuyakana mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yaliyouwa ndugu zake na labda ndio maana jamaa ana hasira na usongo.
Tatizo kubwa la baadhi ya washabikiwa CUF ni mafanatik wa siasa za jino kwa jino huwaelezi kitu wao wanaangalia sura na sharubu sio uwezo wa mtu.