Uchaguzi ni wa nini basi?

Uchaguzi ni wa nini basi?

Swadakta mkuu Uchaguzi huu ni kwa ajili ya kuwaonesha mabeberu kwamba hat sisi bado tuko kwenye domokrasia na watu wana kikubali sana chama kikongwe na wamechoka na fyama pinga maendeleo na wasio wazalendo. Ndio maana mtu kama mimi bora niendelee kuuza zangu dagaa na sangara nipate ugali kuliko kwenda kwenye usanii au unafiki. Rai yangu siku zote turudi kwenye Chama kimoja maana haitakuwa mara ya kwanza na pia ukizingatia Rais wetu anafanana sana na Mwalimu kwa maana naye alipoona fyama pinzani vitarejesha nyuma mpango wa maendeleo miaka ya Sitini alifutilia mbali vyama hivo so naye afutilie mbali. Na pia ni ushauri wangu akina Mbowe na wenzake waondolewe kabisa katika uongozi wao na wahukumiwe kwa kumuua Akwilina.
Tufute vyama vingi tuwe huru. Pia Katiba impe mamlaka Raisi kuwachagua Watawala wengine kuanzia ngazi ya vitongoji na mitaa hadi huko juu

Kwenye hili la mwisho ni hoja inayohitaji kuangaliwa kwa ukaribu zaidi ukizingatia hili swali la mada hii. "Uchaguzi ni wanini basi"? Naona unapendekeza jibu ambalo linafikirisha. Inawezekana uchaguzi kutumika kama namna ya "kuhalalisha" madaraka? Kwamba, lengo la uchaguzi siyo haya mawili niliyoyataja hapo juu bali kuhalalisha uwepo wa watu madarakani?
 
Kuna dhana potofu ya kwamba, wananchi ni majuha hawajui au hawajitambui.
Kuna kusahau kuwa Tanzania ya 1951, 1961, 1981 na 2019 ni tofauti kabisa.

Hili la wananchi kususia kujiandikisha ni ujumbe mzito sana.
Wananchi hawasusii uchaguzi kama tukio , wanasuasia mchakato mzima

Wananchi wanajua kura zao hazina maana, isipokuwa uwepo wao vituo vya kura una maana ya kuhalalisha hujuma dhidi ya kura zao.

Ikiwa wasimamizi wameambiwa wasitangaze mshindani nje ya CCM! kura ina maana gani?

Ikiwa NEC wapo, hawakemei vitendo vya ''dhulma'' kwasababu vinafanywa na wateuzi wao , kura ina maana gani?

Ikiwa NEC wanaruhusu watumishi wao kukimbia ofisi ili wasipokee fomu za wasiowataka, kura ina maana gani?

Ikiwa Polisi wanaimba nyimbo za vyama achilia mbali kusherehekea ushindi wa chama ndani ya Barracks, kura ina maana gani?

Ikiwa DC kaamuriwa ''ole wako' eneo lako lipoteze ushindi, na DC huyu ndiye mkuu wa vyombo vya usalama, kura ina maana gani?

Ikiwa kampeni ni za chama kimoja, kura ina maana gani?

Ukisikia wanasisitiza kuhusu kujiandikisha, si kwamba wanahitaji ushiriki wako katika mchakato wa utawala, la hasha! hawahitaji kura yako kwasababu haiwezi kubadili kilichopangwa.
Wanahitaji uwepo wako ili kuhalalisha mchakato wa uchaguzi!
Mkuu kwa hayo uliyoyaeleza ni sawa kwa asilimia 100 Sasa na tujiulize kwanini Viongozi wa vyama vya upinzani bado wanataka ligi iendelee pamoja na kwamba wamefungwa mikono na miguu? Kwanini wasije na plan B ?
 
Katika nchi ya kidemokrasia uchaguzi unafanyika kwa sababu mbili kubwa.

Kwanza, ni kwa ajili ya wananchi kupima na kutoa hukumu juu ya yale yaliyofanywa katika kipindi kilichopita. Wale wanaomaliza muda wao waliingia na ahadi kadha wa kadha. Je, wametimiza ahadi hizo kwa kiasi gani? Je, wapewe muda mwingine wa kumalizia zile ambazo hazikutimizwa? Je, wanastahili Kuelewa nafasi nyingine?

Hivyo, wananchi wanapewa nafasi ya kufanya uamuzi juu ya uongozi na utawala wa maeneo yao. Endapo wananchi wanakubali na kuridhishwa na kilichofanywa basi watawarudisha viongozi waliopita. Na kama ni la, basi watawaingiza madarakani viongozi wengine.

Sababu ya pili ya kufanya uchaguzi katika nchi ya kidemokrasia inatokana na sababu ya kwanza. Nayo ni kutoa hukumu ya kisiasa juu ya chama tawala. Chama kilichopo madarakani kinaweza kudhania kuwa kinastahili kuwepo madarakani. Hata hivyo ni wananchi ndio wanatakiwa kutoa hukumu hiyo kila baada ya muda fulani, kwa Tanzania ni kila baada ya miaka mitano, kwa Marekani ni kila baada ya miaka minne kwa Urais, miaka miwili kwa wawakilishi na sita kwa maseneta.

Lengo la hili la pili ni kutoa nafasi kwa chama mwingine kuja na mwelekeo tofauti na ule wa chama tawala na kuwapa wananchi viongozi wapya nje ya wale wanaomaliza muda wao kutoka chama tawala.

Katika kuhakikisha sababu hizi mbili zinafanikiwa, nchi zenye demokrasia iliyokomaa zimefanya mambo makubwa kadhaa:

1. Kutengeneza na kusimika mfumo wa uchaguzi unaoweka uwezekano wa aliyeko madarakani (incumbent) kushindwa. Mfumo, unahakikisha aliyeko madarakani anaweza kushinda au kushindwa bila dhulma, hadaa, au matumizi ya njia za mkato.

2. Walioko madarakani hawaogopi au kuhofia wapinzani wao walio nje. Kama wanaongoza vizuri na wanatimiza ilani yao, hawahitaji virungu au vurugu kujitangaza. Kazi zao zinajionesha na mafanikio yao yanajipigia panda yenyewe.

3. Ili kuhakikisha kila mtu yuko sawa, nauli zozote au maagizo yoyote yenye kuashiria kutokujiamini au yenye kutaka kuvuruga mfumo wa uchaguzi yatapingwa na kukataliwa. Ukimpa mtu nafasi ya kuchagua vitu vitatu halafu ukamwekea bastola kichwani na kumwambia achague cha kwanza basi kinachofanyika siyo uchaguzi bali uchafuzi wa kidemokrasia! Hakuna uchaguzi mbele ya shurti! Huwezi kuwa huru kuchagua kama familia, mtaa, jamii yako inashikiliwa mateka.

Ni kwa sababu hiyo naamini ukuu wa dhamira na ukweli (the supremacy of conscience and truth) unamtaka mtu kuamua kama anaitaka kushiriki katika uchaguzi au uchafuzi wa kidemokrasia. He, mtu ajiandikishe kupigika kura wakati chama chake hakiko huru kufanya shughuli same za kisiasa? Je, ashikiri huku akijua wasimamizi wamekatazwa kumtangaza mshindi kama akiwa wa chama chá upinzani? Je, ashiriki uchaguzi huku akijua muda yake haitahesabiwa?

Basi katika nchi ya kidemokrasia Ni muhimu sana kuhakikisha kuwa kinachofanyika ni uchaguzi na siyo uchafuzi, na mfumo ni wa demokrasia na siyo demoghasia na kuwa mwisho wa siku watawala hawageuki kuwa watuwala.
Kwa mawazo haya, uchaguzi ni uchafuzi na matumizi mabaya ya fedha za umma.
IMG_20191015_164248.png
 
Ehee, tuambie Mzee Mwanakijiji. Yamekukuta yepi hadi unaandika namna hii? ushaacha miaka mingi ati!!
 
Katika nchi ya kidemokrasia uchaguzi unafanyika kwa sababu mbili kubwa.

Kwanza, ni kwa ajili ya wananchi kupima na kutoa hukumu juu ya yale yaliyofanywa katika kipindi kilichopita. Wale wanaomaliza muda wao waliingia na ahadi kadha wa kadha. Je, wametimiza ahadi hizo kwa kiasi gani? Je, wapewe muda mwingine wa kumalizia zile ambazo hazikutimizwa? Je, wanastahili Kuelewa nafasi nyingine?

Hivyo, wananchi wanapewa nafasi ya kufanya uamuzi juu ya uongozi na utawala wa maeneo yao. Endapo wananchi wanakubali na kuridhishwa na kilichofanywa basi watawarudisha viongozi waliopita. Na kama ni la, basi watawaingiza madarakani viongozi wengine.

Sababu ya pili ya kufanya uchaguzi katika nchi ya kidemokrasia inatokana na sababu ya kwanza. Nayo ni kutoa hukumu ya kisiasa juu ya chama tawala. Chama kilichopo madarakani kinaweza kudhania kuwa kinastahili kuwepo madarakani. Hata hivyo ni wananchi ndio wanatakiwa kutoa hukumu hiyo kila baada ya muda fulani, kwa Tanzania ni kila baada ya miaka mitano, kwa Marekani ni kila baada ya miaka minne kwa Urais, miaka miwili kwa wawakilishi na sita kwa maseneta.

Lengo la hili la pili ni kutoa nafasi kwa chama mwingine kuja na mwelekeo tofauti na ule wa chama tawala na kuwapa wananchi viongozi wapya nje ya wale wanaomaliza muda wao kutoka chama tawala.

Katika kuhakikisha sababu hizi mbili zinafanikiwa, nchi zenye demokrasia iliyokomaa zimefanya mambo makubwa kadhaa:

1. Kutengeneza na kusimika mfumo wa uchaguzi unaoweka uwezekano wa aliyeko madarakani (incumbent) kushindwa. Mfumo, unahakikisha aliyeko madarakani anaweza kushinda au kushindwa bila dhulma, hadaa, au matumizi ya njia za mkato.

2. Walioko madarakani hawaogopi au kuhofia wapinzani wao walio nje. Kama wanaongoza vizuri na wanatimiza ilani yao, hawahitaji virungu au vurugu kujitangaza. Kazi zao zinajionesha na mafanikio yao yanajipigia panda yenyewe.

3. Ili kuhakikisha kila mtu yuko sawa, nauli zozote au maagizo yoyote yenye kuashiria kutokujiamini au yenye kutaka kuvuruga mfumo wa uchaguzi yatapingwa na kukataliwa. Ukimpa mtu nafasi ya kuchagua vitu vitatu halafu ukamwekea bastola kichwani na kumwambia achague cha kwanza basi kinachofanyika siyo uchaguzi bali uchafuzi wa kidemokrasia! Hakuna uchaguzi mbele ya shurti! Huwezi kuwa huru kuchagua kama familia, mtaa, jamii yako inashikiliwa mateka.

Ni kwa sababu hiyo naamini ukuu wa dhamira na ukweli (the supremacy of conscience and truth) unamtaka mtu kuamua kama anaitaka kushiriki katika uchaguzi au uchafuzi wa kidemokrasia. He, mtu ajiandikishe kupigika kura wakati chama chake hakiko huru kufanya shughuli same za kisiasa? Je, ashikiri huku akijua wasimamizi wamekatazwa kumtangaza mshindi kama akiwa wa chama chá upinzani? Je, ashiriki uchaguzi huku akijua muda yake haitahesabiwa?

Basi katika nchi ya kidemokrasia Ni muhimu sana kuhakikisha kuwa kinachofanyika ni uchaguzi na siyo uchafuzi, na mfumo ni wa demokrasia na siyo demoghasia na kuwa mwisho wa siku watawala hawageuki kuwa watuwala.

Mzee Mwanakijiji uko sahihi kabisa kwa asilimia mia moja.
 
Ni kituko kwa awamu hii kufanya uchaguzi,siwezi poteza muda ilhali mshindi teyari wameshampanga watawala
Nalog off
 
Kazi ilimalizwa pale ikulu kwenye kikao cha watendaji wa kata.

Maelekezo, nyenzo na bahasha walizopewa tunaona matokeo yake huku mitaani.

Hakuna mpinzani,

kwenye kata yako akishinda mpinzani huna kazi.

Wapinzani nitateua mwenyewe.
 
Kwenye hili la mwisho ni hoja inayohitaji kuangaliwa kwa ukaribu zaidi ukizingatia hili swali la mada hii. "Uchaguzi ni wanini basi"? Naona unapendekeza jibu ambalo linafikirisha.Inawezekana uchaguzi kutumika kama namna ya "kuhalalisha" madaraka?Kwamba, lengo la uchaguzi siyo haya mawili niliyoyataja hapo juu bali kuhalalisha uwepo wa watu madarakani?

Ni sahihi kabisa hasa kutokana na yalio kwisha kutokea hapo kabla.
 
Watumishi et wanalazimishwa kujiandikisha. So WHAT?

Hawataenda piga kura
 
Wakati wengine walikuwa wanalia na kutokubaliana na mfumo mzima wa uchaguzi pamoja na hitaji kuu la uwepo wa tume huru ya uchaguzi mlijitaidi kukosoa kweli na kujinadi kwamba walikuwa wanalialia ..
Wakilalamika polisi kutumika kimabavu kupendelea chama kimoja mliziba masikio kabisa...
Wqnanchi wamekata tamaa. .wanaona hawana haja ya kupiga kura isiyo na thamani

Yet siku ya kupiga kura uwezekano wa risasi kupotea njia upo..
Watu wapo majumbani jichagueni nyie wenyewe na mjitangaze. .
RIP Akwilina.
Maneno mazima sana haya... je tunahakikishiwaje risasi kutopotea njia kwa mara nyingine kisa uchaguzi?
 
Yako wapi?

Tuliandika wiki moja tu iliyopita kuhusu uchaguzi. Tukasema lengo la kupiga debe watu wajiandikishe ni kutafuta uhalali wa idadi ya waliojiandikisha.

Wangapi watapiga kura hilo si tatizo. Je, kura zitahesabiwa hilo si tatizo!

Lengo ni ushindi kwa asilimia 100.
Mbinu ya kubadilisha masanduku haifanyi kazi siku hizi. Mbinu mpya ni kuwaondoa wagombea.

Ikiwa nia ilikuwa nzuri ya watu kushirikia uchaguzi, nia hiyo isingekuwa tofauti na kuwa na wagombea pia. Kilichotokea ni kutafuta idadi halafu kuondoa wagombea!

Wapinzani ni watu wa ajabu sana. Hivi haya hawakuyaona?
Hadi yanaandikwa hawakuweza kusoma na kufikiri japo kidogo?

Leo Chadema wanasema hawatashiriki! inashangaza maana maandiko yalikuwa ubaoni.
Kwa Zitto na ACT, nanyi mtatumika kama hamtakuwa makini

Kuweni makini na mtego uliowekwa! usijekuwachonganisha na wenzenu mkiwa wakiwa wote

Kinachotakiwa ni vitongoji 2 ACT, 2 CUF-Lipumba, 2 TLP Mrema.
Tayari uchaguzi utakuwa wa vyama vingi, huru na haki

Kwa asilimia hiyo itakuwa kama 0.2 na Chama chetu cha CCM kitashinda kwa asilimia 99.8!!
 
Katika nchi ya kidemokrasia uchaguzi unafanyika kwa sababu mbili kubwa.

Kwanza, ni kwa ajili ya wananchi kupima na kutoa hukumu juu ya yale yaliyofanywa katika kipindi kilichopita. Wale wanaomaliza muda wao waliingia na ahadi kadha wa kadha. Je, wametimiza ahadi hizo kwa kiasi gani? Je, wapewe muda mwingine wa kumalizia zile ambazo hazikutimizwa? Je, wanastahili Kuelewa nafasi nyingine?

Hivyo, wananchi wanapewa nafasi ya kufanya uamuzi juu ya uongozi na utawala wa maeneo yao. Endapo wananchi wanakubali na kuridhishwa na kilichofanywa basi watawarudisha viongozi waliopita. Na kama ni la, basi watawaingiza madarakani viongozi wengine.

Sababu ya pili ya kufanya uchaguzi katika nchi ya kidemokrasia inatokana na sababu ya kwanza. Nayo ni kutoa hukumu ya kisiasa juu ya chama tawala. Chama kilichopo madarakani kinaweza kudhania kuwa kinastahili kuwepo madarakani. Hata hivyo ni wananchi ndio wanatakiwa kutoa hukumu hiyo kila baada ya muda fulani, kwa Tanzania ni kila baada ya miaka mitano, kwa Marekani ni kila baada ya miaka minne kwa Urais, miaka miwili kwa wawakilishi na sita kwa maseneta.

Lengo la hili la pili ni kutoa nafasi kwa chama mwingine kuja na mwelekeo tofauti na ule wa chama tawala na kuwapa wananchi viongozi wapya nje ya wale wanaomaliza muda wao kutoka chama tawala.

Katika kuhakikisha sababu hizi mbili zinafanikiwa, nchi zenye demokrasia iliyokomaa zimefanya mambo makubwa kadhaa:

1. Kutengeneza na kusimika mfumo wa uchaguzi unaoweka uwezekano wa aliyeko madarakani (incumbent) kushindwa. Mfumo, unahakikisha aliyeko madarakani anaweza kushinda au kushindwa bila dhulma, hadaa, au matumizi ya njia za mkato.

2. Walioko madarakani hawaogopi au kuhofia wapinzani wao walio nje. Kama wanaongoza vizuri na wanatimiza ilani yao, hawahitaji virungu au vurugu kujitangaza. Kazi zao zinajionesha na mafanikio yao yanajipigia panda yenyewe.

3. Ili kuhakikisha kila mtu yuko sawa, nauli zozote au maagizo yoyote yenye kuashiria kutokujiamini au yenye kutaka kuvuruga mfumo wa uchaguzi yatapingwa na kukataliwa. Ukimpa mtu nafasi ya kuchagua vitu vitatu halafu ukamwekea bastola kichwani na kumwambia achague cha kwanza basi kinachofanyika siyo uchaguzi bali uchafuzi wa kidemokrasia! Hakuna uchaguzi mbele ya shurti! Huwezi kuwa huru kuchagua kama familia, mtaa, jamii yako inashikiliwa mateka.

Ni kwa sababu hiyo naamini ukuu wa dhamira na ukweli (the supremacy of conscience and truth) unamtaka mtu kuamua kama anaitaka kushiriki katika uchaguzi au uchafuzi wa kidemokrasia. He, mtu ajiandikishe kupigika kura wakati chama chake hakiko huru kufanya shughuli same za kisiasa? Je, ashikiri huku akijua wasimamizi wamekatazwa kumtangaza mshindi kama akiwa wa chama chá upinzani? Je, ashiriki uchaguzi huku akijua muda yake haitahesabiwa?

Basi katika nchi ya kidemokrasia Ni muhimu sana kuhakikisha kuwa kinachofanyika ni uchaguzi na siyo uchafuzi, na mfumo ni wa demokrasia na siyo demoghasia na kuwa mwisho wa siku watawala hawagki kuwa watuwala.
Hakika huwezi ukakiita hiki kinachoendekea, kitachohitimisha tarehe 24 mwezi huu kama UCHAGUZI bali inastahili kwa asilimia 100 kuita ni UCHAFUZI
 
Back
Top Bottom