Uchaguzi ni wa nini basi?

Uchaguzi ni wa nini basi?

Naona dalili zoote za mtanzania kuanza kujitambua ingawa mchakato unaenda taratibu sana. Ila kuna tatizo ninaloliona hapa kama ifuatavyo
1; Hivi kuna mtumishi wa umma hata mmoja atakwenda kujiandikisha kupiga kura au kwenda kupiga kura yenyewe? kama hivyo ndivyo basi kuanzia sasa waache malalamiko yao ya kila siku maana wanao uwezo mkubwa sana wa kuutingisha utawala huu lakini wao ndio wa wa kwanza kuuwezesha
2; Watumishi wa umma kote nchini wanashindwa kuwashawishi wake zao/ waume zao na familia zao kususia uchaguzi huu ili kumuonyesha tu mwamba mkuu kuwa na yeye ni mtumishi tu wa umma
3; Kwenye sakata la vyeti fake kuna watu wanajulikana wameonewa tu na wengine walikosea padogo tu hawa nao hawaoni umuhimu wa kuungana na kushawishi wanafamilia zao kumtingisha mwamba hadi aite jeshi?
4; Kuna wafanyabiashara walioahidiwa kuishi kama mashetani wapo tu nao kazi kujipendekeza tu
 
Uchaguzi ni wa nini Basi?
As usual, always helping our country to do the best and to be more pure than pure. Tatizo ni vyama vya upinzani ambavyo vimekuwa vya ukoo zaidi au vimekuwa binafsi zaidi. Wengine vyama vyao vimekuwa vya mfukoni zaidi. Zito Kabwe amejitajirisha kutokana na position aliyokuwanayo i.e kufahamu the working of Government system na kuchuma pesa yeye mwenyewe binafsi, Mbowe kujitajirisha yeye mwenyewe binafsi nk. sasa katika hali kama hiyo utaona kabisa Watanzania walio wengi hawawezi kuwapa kura. Hata pale wakati Dr. Slaa alipokuwa Chadema alipigwa vita, its all about money and not democracy.

Watu wanashabikia democracy iliyopo UK, USA nk lakini angalia hizo democracy ni za miaka mingapi? UK more than 500 yrs Vile vile hakuna democracy ki-vile ambavyo wengi Africa wanaaminishwa, there is a lot of money behind the scenes supported by the media and financial services, campaign rules etc. the white man w ill always undermine the black man because they are afraid one of these days Africa will have more JPM 's and they will have more trouble. Its a pity that many Tanzanians and especially those who migrated to USA and other countries have joined the band wagon of opposition parties who are there for themselves (money). Their main agenda is to discredit the current government effort to improve the lives of Tanzanians. People should look at the big picture and challenge the government on basic issues which affect the majority of Tanzanians. JPM has transformed this country in barely 4yrs, improvements of many sectors etc.

Swala la kutojiandikisha sina facts hivi sasa kufahamu ni wangapi hawajajiandikisha lakini mara nyingi wengi huenda karibu na siku za mwisho etc.

Kuhusu swala la kupiga kura hilo lazima litokee hata kama atakayepiga kura ni moja kwa sababu hiyo ndio mandate tuliyojiwekea kikatiba. Nafahamu wengi hawatakwenda kupiga kura lakini hilo ni shauri lao watakapokwama ndio watafahamu umuhimu wa kupiga kura.
 
Mimi nawashauri wapinzani na nimeshatia ushauri hata kwa baadhi ya viongozi wa upinzani humu kwenye mitandao ya kijamii, badala ya kuhamasisha watu kwenda kupiga kura ni bora wakatumia mwitikio huu wa umma kudai tume huru ya uchaguzi. Nimemshauri kuanzia mwaka kesho mwezi wa tatu au wanne kutangaza maandamano ya amani mara moja kila jumamosi ya mwanzo au ya mwisho wa mwezi kudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya juu.

Madai hayo yatakuwa na uhalali wa umma kwani mpaka sasa umma umedhibitisha kwamba hakuna uchaguzi bali uhuni wa kiwango cha juu. Nina hakika umma uko tayari kwa hilo, Hapa inabidi hata JWTZ washawishiwe kwenye hili kama kuna uwezekano.
JF ingekuwa sehemu ya kutafuta njia za ufumbuzi wa matatizo kama hivi, nina hakika isingekuwepo.
Sasa hivi imevumiliwa kuwepo kwa sababu imeonekana ni mahali pa kubadilishana mipasho tu basi.

Heshima Mkuu 'Tindo.' Sijui kama mapendekezo yako haya yatasikilizwa na kufanyiwa kazi.
 
Kuna dhana potofu ya kwamba, wananchi ni majuha hawajui au hawajitambui.
Kuna kusahau kuwa Tanzania ya 1951, 1961, 1981 na 2019 ni tofauti kabisa.

Hili la wananchi kususia kujiandikisha ni ujumbe mzito sana.
Wananchi hawasusii uchaguzi kama tukio , wanasuasia mchakato mzima

Wananchi wanajua kura zao hazina maana, ili uwepo wao vituo vya kura una maana ya kuhalalisha hujuma dhidi ya kura zao.

Ikiwa wasimamizi wameambiwa wasitangaze mshindani nje ya CCM! kura ina maana gani?

Ikiwa NEC wapo, hawakemei vitendo vya ''dhulma'' kwasababu vinafanywa na wateuzi wao , kura ina maana gani?

Ikiwa NEC wanaruhusu watumishi wao kukimbia ofisi ili wasipokee fomu za wasiowataka, kura ina maana gani?

Ikiwa Polisi wanaimba nyimbo za vyama achilia mbali kusherehekea ushindi wa chama ndani ya Barracks, kura ina maana gani?

Ikiwa DC kaamuriwa ''ole wako' eneo lako lipoteze ushindi, na DC huyu ndiye mkuu wa vyombo vya usalama, kura ina maana gani?

Ikiwa kampeni ni za chama kimoja, kura ina maana gani?

Ukisikia wanasisitiza kuhusu kujiandikisha, si kwamba wanahitaji ushiriki wako katika mchakato wa utawala, la hasha! hawahitaji kura yako kwasababu haiwezi kubadili kilichopangwa.
Wanahitaji uwepo wako ili kuhalalisha mchakato wa uchaguzi!
Duh nimekuelewa mwamba
 
Swali linalonitatiza ni moja. Tukishawanyima 'uwepo wetu,' na bado wakajitangaza washindi hata kwa kura 50 zilizopigwa na makada; kwa maana kwao lililo mhimu ni 'ushindi' wa aina yoyote.... ni kipi kitakachoonekana tumefaidika nacho sisi ambao hatukupiga kura kwa kugomea uovu wao?

Sijui kama tuna kundi tena linalojali 'heshima na kuheshimika'.
Ni bora wajitangazie wao maana hukua sehemu ya dhuluma. Kwavyovyote itakavyokua lazima watashinda tu.
 
Swali zuri sana kama swali la Mzee Mwanakijiji . Ni maswali yanayofikirisha.

Naomba niweke sawa kauli zako. Sina uhakika kama watu ''wanaogomea '' kama usemavyo.
Mada nyingi zinazozungumzia hili suala zinazungumzia ''kususia'' kauli isiyo ya kweli.

Wananchi hawajasusia au kugomea uchaguzi.

Wananchi wanatafsiri na kutekeleza kauli za ma-DC, Wakurugenzi na viongozi wote wa chama na serikali isemayo ole wako umtangaze mtu nje ya CCM. DC wa Dodoma alisema hilo ni tatizo lako. Hivyo basi kauli hiyo inatoa tafsiri hii;
1. CCM unasababu gani za kujiandikisha ikiwa una uhakika mgombea wako atatangazwa mshindi?
2. Ukiwa mpinzani unasababu gani za kujiandikisha ikiwa umehakikishiwa mgombea wako hatatangazwa mshindi?

Pengine wananchi wanatafsiri hivyo ! sina uhakika ni maoni tu

Kuhusu swali la pili, kuna kitu kinaitwa '' legal legitimacy'' Kwa maana ya uhalali wa kisheria hata kama mtu atashinda kwa kura 7. Ni halali kwasababu mchakato mzima umekamilika, kura zimepigwa, zimehasabiwa na mshindi katangazwa.

Halafu kuna kitu kinaitwa ''political legitimacy'' yaani uhalali wa kisiasa. Kwamba, kura zimepigwa, zimehesabiwa au kutohesabiwa, mshindi katangazwa.

Huyu ana uhalali wa kisiasa kwasababu kafuata utaratibu mzima hadi kutangazwa hata kama utaratibu huo haukupata ''legal legitimacy''

Kwa taarifa, wanasiasa hawaogopi ''legal legitimacy'' wanaogopa sana ''political legitimacy''

Political legitimacy ndiyo inawapa ''authority to influence''
Wanapiokosa hulazimika kurudi katika mstari wa tafakuri.

Angalia historia ya nchi za dunia hii. Hata viongozi walioingia madarakani kwa nguvu, iwe za kijeshi n.k. au kwa kutumia 'Falme'' bado hubumba bumba ''uchafuzi'' ili wapate political legitimacy.
Heshima mkuu Nguruvi. Uliyoandika hapa ni ukweli mtupu katika muonekano wa nadharia za 'kisomi' (academic theories).
Ukitazama hali ya kidunia, mambo haya ya 'uhalali' (legitimacy) iwe kisheria au kisiasa, ni mambo yanayotengenezewa nafasi yawepo baada ya unajisi wake.
Tawala za akina Idd Amin Dada na wengine, sijui kama tunaweza kusema kwamba walikosa 'legitimacy' ya aina yoyote baada ya uwepo wao, hata kupitia njia zisizo sahihi.

Hali sasa hivi imezidi kuwa mbaya kwa sababu mifumo ya kimataifa iliyokuwa inapingana haipo tena. Kwa hiyo tunaona ilivyo rahisi sasa kwa viongozi kukandamiza na hata kuua wananchi bila ya uoga wa makaripio toka nje. Hali imekuwa ngumu sana sasa. Hata mahakama, kama ICC, kumshitaki kiongozi aliyepo kwenye madaraka inakuwa ngumu sana, kama ilivyoonekana na Bashir kule Sudan.

Hali hii imewapa viongozi wenye tabia za ukandamizaji kuwa na ujasiri wa kufanya wanavyopenda nchini mwao.
Suluhisho lipo kwa wananchi pekee, wanapoamua kukataa kukandamizwa.
 
Sidhani kama itakuwa shida sana kuunganisha kupungua kwa watu kujiandikisha kupiga kura na hali ya kisiasa nchini. Sasa, watu wanaweza kuandika kwa hisia lakini kuna haja ya kuwa na taarifa sahihi (facts). Ni makosa kudhania tu kuwa watu hawajiandikishi kwa kiwango kikubwa kwa sababu moja au nyingine. Ni muhimu kukusanya taarifa sahihi na za uhakika na hivyo kuwa na data za nini kinaendelea.

Kwa maoni yangu hali iko hivi:

1. zuio la Raisi dhidi ya wapinzani limesababisha siasa zetu kukosa msisimko ambao ungepelekea watu kujiandikisha.

2. wananchi na wapiga kura hawauchukulii kwa uzito uchaguzi wa serikali za mitaa. Wapiga kura hawaoni umuhimu wa nafasi zinazogombewa ktk uchaguzi huu.

3. CCM au chama tawala hawaoni kama kuna tishio kwa chama chao hivyo hawaoni ulazima wa kujiandikisha kupiga kura na kukihami chama chao.

4. Wapinzani hawaoni kama uchaguzi wa serikali za mitaa au ushindi ktk uchaguzi huu utabadili mazingira mabaya ya kisiasa yaliyoko nchini.

5. Vyama vyote vya siasa vimejikita zaidi ktk harakati za udiwani, ubunge, na Uraisi. Wananchi wamejengwa kiimani kuwa uchaguzi muhimu ni ule wa madiwani, wabunge, na Raisi.
 
Ni asilimia 0.00000000000000001 ya watanzania ndio wamo humu JF...JF had never been a true reflection of the situation at ground...wananchi wenye nia ya kujiandikisha wanaendelea kujiandikisha kwa wingi
Ok hizo data zako nadhani haziko sahihi.Taarifa inayotokea kwenye mtandao wa JF kwa mtu mmoja tu,baada ya dakika tano tu, imeshasambaa kijiji kizima.Nikupe mfano kidogo tu.Walipochomoa waya kule Morogoro dakika taarifa ilienea nchi nzima na sisi huku kijijini tulizipata.

Kwa hiyo kutudanganya kwamba eti hawapati taarifa unajindanganya mwenyewe.Na kama wanajiandikisha kwa wingi iweje ma dc na ma rc kupewa tahadhari ya kibarua chao, endapo watu hawatajiandikisha.Hii ni hali halisi kuwa zoezi ni teeeteee sio nzuri.

Muda wa kujiandikisha kwa miaka ya nyuma,ulikuwa unaongezwa kutokana na wingi wa watu waliojitokeza,lakini sasa hivi muda unaongezwa kwa watu kutokujitokeza.

Hata mimi binafsi sijashawishiwa na yeyote kutokujiandikisha au kujiandikisha ila sitapoteza hata nusu dakika kwenda kujiandikisha kwa sababu kama viongozi wote wameshateuliwa,kuna haja gani ya kujiandikisha.Yaani wanatufanya Watanzania wote kuwa rubber stamp.Tumewaona na tumewasoma kwa maneno ya vinywa vyao.

Mtoa post nakuambia hivi juzi hapa kwetu walikuja maafisa kutaka kuhamasisha watu wakajiandikishe,kilichowapata tutawaomba watujulishe humu,ili ujue mambo sio kama unavyotaka kutudanganya.

Ieo hii Jumapili maafisa watendaji wamepita kwetu kijijini kwa zoezi hilohilo wakanikuta, wakaniomba niende kujiandikisha.Jibu nililowapa niliwaambia sitajiandikisha na muda huo sina.Waliponiuliza ni kwa nini,niliwaambia warudi baadae niwape jibu nikiwa na nafasi nzuri.

Viongozi wetu wasitufunike kwa neti ya mbu wakiamini kuwa hatuoni.Nawaambia hivi hiyo neti waliyotufunika nayo ina matundu tena mengi tu, tunaona.

"Haki huinua taifa,bali dhambi ni aibu kwa kila mtu"
 
usipojiandikisha ni wewe mwenyewe umepoteza haki yako na baada ya uchaguzi ukiinua sauti kulaumu utakuwa ni mnafiki kwani kura hukupiga kwa hiyo kaa kimya tu
 
usipojiandikisha ni wewe mwenyewe umepoteza haki yako na baada ya uchaguzi ukiinua sauti kulaumu utakuwa ni mnafiki kwani kura hukupiga kwa hiyo kaa kimya tu
....amepoteza haki ya kufanya nini?
Kwa nini ni mazuzu kiasi hiki? Mnawachukuliaje hasa Watanzania, kwamba ni watu wasio na uelewa, who need decisions to be made for them??
 
M
As usual, always helping our country to do the best and to be more pure than pure. Tatizo ni vyama vya upinzani ambavyo vimekuwa vya ukoo zaidi au vimekuwa binafsi zaidi. Wengine vyama vyao vimekuwa vya mfukoni zaidi. Zito Kabwe amejitajirisha kutokana na position aliyokuwanayo i.e kufahamu the working of Government system na kuchuma pesa yeye mwenyewe binafsi, Mbowe kujitajirisha yeye mwenyewe binafsi nk. sasa katika hali kama hiyo utaona kabisa Watanzania walio wengi hawawezi kuwapa kura. Hata pale wakati Dr. Slaa alipokuwa Chadema alipigwa vita, its all about money and not democracy.

Watu wanashabikia democracy iliyopo UK, USA nk lakini angalia hizo democracy ni za miaka mingapi? UK more than 500 yrs Vile vile hakuna democracy ki-vile ambavyo wengi Africa wanaaminishwa, there is a lot of money behind the scenes supported by the media and financial services, campaign rules etc. the white man w ill always undermine the black man because they are afraid one of these days Africa will have more JPM 's and they will have more trouble. Its a pity that many Tanzanians and especially those who migrated to USA and other countries have joined the band wagon of opposition parties who are there for themselves (money). Their main agenda is to discredit the current government effort to improve the lives of Tanzanians. People should look at the big picture and challenge the government on basic issues which affect the majority of Tanzanians. JPM has transformed this country in barely 4yrs, improvements of many sectors etc.

Swala la kutojiandikisha sina facts hivi sasa kufahamu ni wangapi hawajajiandikisha lakini mara nyingi wengi huenda karibu na siku za mwisho etc.

Kuhusu swala la kupiga kura hilo lazima litokee hata kama atakayepiga kura ni moja kwa sababu hiyo ndio mandate tuliyojiwekea kikatiba. Nafahamu wengi hawatakwenda kupiga kura lakini hilo ni shauri lao watakapokwama ndio watafahamu umuhimu wa kupiga kura.
Mazuzu nchi hii hamuwezi kuisha hivi na Elim yako unataka utuaminishe kwamba hapo alipo Mbowe yupo kwaajili ya kuutafuta utajili? Huna aibu LA sivyo wewe ni wale wale lumumba buku 7
 
Katika nchi ya kidemokrasia uchaguzi unafanyika kwa sababu mbili kubwa.

Kwanza, ni kwa ajili ya wananchi kupima na kutoa hukumu juu ya yale yaliyofanywa katika kipindi kilichopita. Wale wanaomaliza muda wao waliingia na ahadi kadha wa kadha. Je, wametimiza ahadi hizo kwa kiasi gani? Je, wapewe muda mwingine wa kumalizia zile ambazo hazikutimizwa? Je, wanastahili Kuelewa nafasi nyingine?

Hivyo, wananchi wanapewa nafasi ya kufanya uamuzi juu ya uongozi na utawala wa maeneo yao. Endapo wananchi wanakubali na kuridhishwa na kilichofanywa basi watawarudisha viongozi waliopita. Na kama ni la, basi watawaingiza madarakani viongozi wengine.

Sababu ya pili ya kufanya uchaguzi katika nchi ya kidemokrasia inatokana na sababu ya kwanza. Nayo ni kutoa hukumu ya kisiasa juu ya chama tawala. Chama kilichopo madarakani kinaweza kudhania kuwa kinastahili kuwepo madarakani. Hata hivyo ni wananchi ndio wanatakiwa kutoa hukumu hiyo kila baada ya muda fulani, kwa Tanzania ni kila baada ya miaka mitano, kwa Marekani ni kila baada ya miaka minne kwa Urais, miaka miwili kwa wawakilishi na sita kwa maseneta.

Lengo la hili la pili ni kutoa nafasi kwa chama mwingine kuja na mwelekeo tofauti na ule wa chama tawala na kuwapa wananchi viongozi wapya nje ya wale wanaomaliza muda wao kutoka chama tawala.

Katika kuhakikisha sababu hizi mbili zinafanikiwa, nchi zenye demokrasia iliyokomaa zimefanya mambo makubwa kadhaa:

1. Kutengeneza na kusimika mfumo wa uchaguzi unaoweka uwezekano wa aliyeko madarakani (incumbent) kushindwa. Mfumo, unahakikisha aliyeko madarakani anaweza kushinda au kushindwa bila dhulma, hadaa, au matumizi ya njia za mkato.

2. Walioko madarakani hawaogopi au kuhofia wapinzani wao walio nje. Kama wanaongoza vizuri na wanatimiza ilani yao, hawahitaji virungu au vurugu kujitangaza. Kazi zao zinajionesha na mafanikio yao yanajipigia panda yenyewe.

3. Ili kuhakikisha kila mtu yuko sawa, nauli zozote au maagizo yoyote yenye kuashiria kutokujiamini au yenye kutaka kuvuruga mfumo wa uchaguzi yatapingwa na kukataliwa. Ukimpa mtu nafasi ya kuchagua vitu vitatu halafu ukamwekea bastola kichwani na kumwambia achague cha kwanza basi kinachofanyika siyo uchaguzi bali uchafuzi wa kidemokrasia! Hakuna uchaguzi mbele ya shurti! Huwezi kuwa huru kuchagua kama familia, mtaa, jamii yako inashikiliwa mateka.

Ni kwa sababu hiyo naamini ukuu wa dhamira na ukweli (the supremacy of conscience and truth) unamtaka mtu kuamua kama anaitaka kushiriki katika uchaguzi au uchafuzi wa kidemokrasia. He, mtu ajiandikishe kupigika kura wakati chama chake hakiko huru kufanya shughuli same za kisiasa? Je, ashikiri huku akijua wasimamizi wamekatazwa kumtangaza mshindi kama akiwa wa chama chá upinzani? Je, ashiriki uchaguzi huku akijua muda yake haitahesabiwa?

Basi katika nchi ya kidemokrasia Ni muhimu sana kuhakikisha kuwa kinachofanyika ni uchaguzi na siyo uchafuzi, na mfumo ni wa demokrasia na siyo demoghasia na kuwa mwisho wa siku watawala hawageuki kuwa watuwala.
Kama ataendelea kuminya demokrasia akifikiria watanzania hawana akili ,uchaguzi mķuu ujao hali itakua mbaya zaid. Uwezo wa viongoz kutafakari impact ya maamuz yao ni mdogo sana. Mh bado hajajua ukubwa wa nafasi yake kuwa kila jambo analolisema huchukuliwa kama sheria yeye analipuka tu.
 
Kwa Tanzania uchaguzi wa haki bado sana. Kiukweli sioni haja ya kujiandikisha zaidi ya kupata kitambulisho kwa ajili ya shughuli zenye kuhitaji uwepo wa kitambulisho, ila si kwa kupiga kura.
wameanza lini kutoa hivyo vitambulisho?
 
Back
Top Bottom