Uchaguzi ni wa nini basi?

Uchaguzi ni wa nini basi?

Unafahamu jumla ya wapiga walioiandikisha 2015!!?? .... Ni 23.78M.. Leo uje useme upande wa ccm tu na mazombi yetu tufike 20M !!?? Fuvu lako litakuwa na matege linapitisha upepo.
 
Swali linalonitatiza ni moja. Tukishawanyima 'uwepo wetu,' na bado wakajitangaza washindi hata kwa kura 50 zilizopigwa na makada; kwa maana kwao lililo mhimu ni 'ushindi' wa aina yoyote.... ni kipi kitakachoonekana tumefaidika nacho sisi ambao hatukupiga kura kwa kugomea uovu wao?

Sijui kama tuna kundi tena linalojali 'heshima na kuheshimika'.
Uwanyime au uwape uwepo wako, wao hawajali, .........kama hata damu ya asiye mwana CCM haitakiwi kule blood bank, kura ilopigwa kwa mpinzani itahesabiwa kweli?????.. kumbuka pia kumchagua mpinzani ni kum-expose kwenye mauti.
 
Ni muhimu kukusanya taarifa sahihi na za uhakika
Ndugu yangu, kama kutangaza tu matokeo sahihi wahusika wanapigwa mkwara, je huo umuhimu wa kukusanya taarifa sahihi na za uhakika utawezekanaje? Ili iweje? Ngoja nikukumbushe kidogo...katika uchaguzi wa mwaka 2015, idadi ya waliodaiwa kujiandikisha kupiga kura walikuwa ni watu 23,254,485. Hata hivyo idadi ya kura alizodaiwa kupata jiwe na kutangazwa mshindi ilikuwa ni 8,882,935 sawa na asilimia 38% ya waliojiandikisha. Hiyo ndio Tanzania...karibu sana nyumbani.
...na hivyo kuwa na data za nini kinaendelea.
Mmm, mzee mwenzangu, kweli unaishi dunia hii! Eti tuwe na data za nini kinaendelea...hapa naomba nikumbushie alichosema Nguruvi3, utawala huu wa kidikteta hauhitaji kura yako kwa sababu ya kufanya maboresho, wanahitaji uwepo wako ili kuhalalisha mchakato wa uchaguzi, oops, mchakato wa uchafuzi!
 
Mmm, mzee mwenzangu, kweli unaishi dunia hii! Eti tuwe na data za nini kinaendelea...hapa naomba nikumbushie alichosema Nguruvi3, utawala huu wa kidikteta hauhitaji kura yako kwa sababu ya kufanya maboresho, wanahitaji uwepo wako ili kuhalalisha mchakato wa uchaguzi, oops, mchakato wa uchafuzi!

Kwenye hili la mwisho ni hoja inayohitaji kuangaliwa kwa ukaribu zaidi ukizingatia hili swali la mada hii. "Uchaguzi ni wanini basi"? Naona unapendekeza jibu ambalo linafikirisha. Inawezekana uchaguzi kutumika kama namna ya "kuhalalisha" madaraka? Kwamba, lengo la uchaguzi siyo haya mawili niliyoyataja hapo juu bali kuhalalisha uwepo wa watu madarakani?
 
"Mzee Mwanakijiji, post: 33118308, member: 118"]
Sidhani kama itakuwa shida sana kuunganisha kupungua kwa watu kujiandikisha kupiga kura na hali ya kisiasa nchini. Sasa, watu wanaweza kuandika kwa hisia lakini kuna haja ya kuwa na taarifa sahihi (facts).
Nikweli

Ni makosa kudhania tu kuwa watu hawajiandikishi kwa kiwango kikubwa kwa sababu moja au nyingine. Ni muhimu kukusanya taarifa sahihi na za uhakika na hivyo kuwa na data za nini kinaendelea.
Kiuhalisia hiki ndicho kinapaswa kufanyika, kutafuta 'data'

Katika mazingira yaliyopo hilo nalo ni gumu, litapotosha zaidi kuliko kutoa jibu sahihi.
Kuna sheria ya takwimu iliyoundwa makusudi kabisa kudhibiti upatikanaji wa takwimu kutoka taasisi nyingine huru nje ya zile za serikali.

Tamisemi watatoa takwimu halisi ? Yaani wajikaange na mafuta yao!

Tukirudi kwa tume (NEC) nadhani wanadhamana ya ''takwimu'' kiaina
Nao hunyooshewa kidole kila uchao

Wameshindwa kukemea ma-DC kuhusu kutangaza wagombe ikiwa na mamlaka ya kisheria.

NEC imeshindwa kueleza lini kampeni zinazuiliwa lini zinapaswa kuanza.

NEC imeshindwa kueleza sanduku linatokaje kituoni na kurejeshwa nje ya utaratibu.

NEC imeshindwa kueleza kwanini wasimamizi wanakimbia vituo kuchukua fomu wasizopendezwa nazo.

Leo tutegemee takwimu za NEC kuwa tofauti na NEC ilivyo. Real!
NEC kama taasisi nao pia walisikia tangazo la ole wako, sidhani kama wangependa iwe ''ole wao''

Hapa ndipo tunarudi nyumbani Bondei kucheza mdumange!
 
Sisi wananchi tupo pembeni tunaangalia kama watapika data au watajitangaza wameshinda Kwa kishindo.
Maana mwitikio wa wananchi kujiandikisha tunaujua na lolote litakalofanyika hasa Kwenye kuiba Kura na kuongeza idadi ya wapigakura hapo ndipo watazidi kutukoroga.

Tunamsihi raisi asithubutu kuwatumbua wakuu wa mikoa na wilaya eti kwasabb kuna idadi ndogo ya wapigakura Kwenye maeneo yao....

Itakuwa aibu kwake na kujishusha hadhi na hata ule uaminifu Kwa wananchi utapungua zaidi,miaka yote hakujawahi kusikia lawama kama hizi zinaenda Kwa wakuu wa wilaya na mikoa huyu raisi ajipime matendo yake kwetu kama anatosha kutuongoza!!!!! Dalili hizi za watu kuchoshwa na udikteta zitazidi zaidi hapo mwakani
 
Kwetu inashangaza sana..
Watu wamegomea kimtindo maana kila kitu kinaenda sawa kabisa, mamiradi mikubwa inafanywa na mapesa ya ndani.....
 
Wasilielie mazingira ya kuendelea kutawala wameyaweka wao na wataendelea shida ni nn. Sisi tunachapa kazi na watawale hadi milele ya duniani. Sio ile ya Muumba
Wakati wengine walikuwa wanalia na kutokubaliana na mfumo mzima wa uchaguzi pamoja na hitaji kuu la uwepo wa tume huru ya uchaguzi mlijitaidi kukosoa kweli na kujinadi kwamba walikuwa wanalialia ..
Wakilalamika polisi kutumika kimabavu kupendelea chama kimoja mliziba masikio kabisa...
Wqnanchi wamekata tamaa. .wanaona hawana haja ya kupiga kura isiyo na thamani

Yet siku ya kupiga kura uwezekano wa risasi kupotea njia upo..
Watu wapo majumbani jichagueni nyie wenyewe na mjitangaze. .
RIP Akwilina.
 
Wasilielie mazingira ya kuendelea kutawala wameyaweka wao na wataendelea shida ni nn. Sisi tunachapa kazi na watawale hadi milele ya duniani. Sio ile ya Muumba
Shida ni pale wanapotumia hata hela zako za NSSF kujipa mikopo na kutengeneza miradi hewa........Milele ya duniani kama ulivosema... no longer at ease....
 
Tunaweza hata tukaacha kulitumia hilo neno "Demokrasia," badala yake tukaamua maksudi kuheshimu HAKI za watu kuchagua kwa uhuru na utashi wao wenyewe kuwachagua viongozi miongoni mwao wanaotaka wawaongoze.

Mtu anapoporwa haki yake kwa kura yake isihesabike baada ya kupiga kura, mtu huyo ananajisiwa na anayemnyima haki hiyo ni mharifu anayestahili kuadhibiwa.

Kuna watu wanasema wapinzani wanachochea vurugu kwa kuwahimiza wananchi kuhakikisha kwamba kura zao haziibiwi, au mtu ambaye hawakumchagua ndie anatangazwa kuwa mshindi!
Na kuna watu wanashangilia wanaposikia upotoshaji huu. Mharifu ni anayeiba kura. Huyo ndie anayesababisha vurugu na sio wapinzani.

Kinachokosekana sasa ni kumkosa mtu mwenye ushawishi, anayeaminiwa na wengi. Akipatikana mtu kama Dr Martin Luther King Jr, au Mwalimu Kambarage Nyerere, vitisho na mitutu inayotangulizwa mbele kuwatia hofu wananchi itageuzwa na kuelekezwa kwa wahalifu wenyewe.

Nadhani ni swala la muda tu. Taratibu watu wataanza na kugoma kujiandikisha kupiga kura..., na tutaanzia hapo kwenda mbele kama wanaowakandamiiza wenzao hawatajirudi.

Vitisho na ubabe havijawahi kuwa njia za kudumu za kuwanyamazisha watu.

Mimi nawashauri wapinzani na nimeshatia ushauri hata kwa baadhi ya viongozi wa upinzani humu kwenye mitandao ya kijamii, badala ya kuhamasisha watu kwenda kupiga kura ni bora wakatumia mwitikio huu wa umma kudai tume huru ya uchaguzi. Nimemshauri kuanzia mwaka kesho mwezi wa tatu au wanne kutangaza maandamano ya amani mara moja kila jumamosi ya mwanzo au ya mwisho wa mwezi kudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya juu.

Madai hayo yatakuwa na uhalali wa umma kwani mpaka sasa umma umedhibitisha kwamba hakuna uchaguzi bali uhuni wa kiwango cha juu. Nina hakika umma uko tayari kwa hilo, Hapa inabidi hata JWTZ washawishiwe kwenye hili kama kuna uwezekano.
 
Hivi yule Naibu Waziri aliyewaombea msamaha kwa Rais wananchi wa jimbo fulani kwa kumchagua mmbunge wa upinzani alijibiwa nini na yule aliyeombwa msamaha?
 
Ni asilimia 0.00000000000000001 ya watanzania ndio wamo humu JF...JF had never been a true reflection of the situation at ground...wananchi wenye nia ya kujiandikisha wanaendelea kujiandikisha kwa wingi
 
Katika nchi ya kidemokrasia uchaguzi unafanyika kwa sababu mbili kubwa.

Kwanza, ni kwa ajili ya wananchi kupima na kutoa hukumu juu ya yale yaliyofanywa katika kipindi kilichopita. Wale wanaomaliza muda wao waliingia na ahadi kadha wa kadha. Je, wametimiza ahadi hizo kwa kiasi gani? Je, wapewe muda mwingine wa kumalizia zile ambazo hazikutimizwa? Je, wanastahili Kuelewa nafasi nyingine?

Hivyo, wananchi wanapewa nafasi ya kufanya uamuzi juu ya uongozi na utawala wa maeneo yao. Endapo wananchi wanakubali na kuridhishwa na kilichofanywa basi watawarudisha viongozi waliopita. Na kama ni la, basi watawaingiza madarakani viongozi wengine.

Sababu ya pili ya kufanya uchaguzi katika nchi ya kidemokrasia inatokana na sababu ya kwanza. Nayo ni kutoa hukumu ya kisiasa juu ya chama tawala. Chama kilichopo madarakani kinaweza kudhania kuwa kinastahili kuwepo madarakani. Hata hivyo ni wananchi ndio wanatakiwa kutoa hukumu hiyo kila baada ya muda fulani, kwa Tanzania ni kila baada ya miaka mitano, kwa Marekani ni kila baada ya miaka minne kwa Urais, miaka miwili kwa wawakilishi na sita kwa maseneta.

Lengo la hili la pili ni kutoa nafasi kwa chama mwingine kuja na mwelekeo tofauti na ule wa chama tawala na kuwapa wananchi viongozi wapya nje ya wale wanaomaliza muda wao kutoka chama tawala.

Katika kuhakikisha sababu hizi mbili zinafanikiwa, nchi zenye demokrasia iliyokomaa zimefanya mambo makubwa kadhaa:

1. Kutengeneza na kusimika mfumo wa uchaguzi unaoweka uwezekano wa aliyeko madarakani (incumbent) kushindwa. Mfumo, unahakikisha aliyeko madarakani anaweza kushinda au kushindwa bila dhulma, hadaa, au matumizi ya njia za mkato.

2. Walioko madarakani hawaogopi au kuhofia wapinzani wao walio nje. Kama wanaongoza vizuri na wanatimiza ilani yao, hawahitaji virungu au vurugu kujitangaza. Kazi zao zinajionesha na mafanikio yao yanajipigia panda yenyewe.

3. Ili kuhakikisha kila mtu yuko sawa, nauli zozote au maagizo yoyote yenye kuashiria kutokujiamini au yenye kutaka kuvuruga mfumo wa uchaguzi yatapingwa na kukataliwa. Ukimpa mtu nafasi ya kuchagua vitu vitatu halafu ukamwekea bastola kichwani na kumwambia achague cha kwanza basi kinachofanyika siyo uchaguzi bali uchafuzi wa kidemokrasia! Hakuna uchaguzi mbele ya shurti! Huwezi kuwa huru kuchagua kama familia, mtaa, jamii yako inashikiliwa mateka.

Ni kwa sababu hiyo naamini ukuu wa dhamira na ukweli (the supremacy of conscience and truth) unamtaka mtu kuamua kama anaitaka kushiriki katika uchaguzi au uchafuzi wa kidemokrasia. He, mtu ajiandikishe kupigika kura wakati chama chake hakiko huru kufanya shughuli same za kisiasa? Je, ashikiri huku akijua wasimamizi wamekatazwa kumtangaza mshindi kama akiwa wa chama chá upinzani? Je, ashiriki uchaguzi huku akijua muda yake haitahesabiwa?

Basi katika nchi ya kidemokrasia Ni muhimu sana kuhakikisha kuwa kinachofanyika ni uchaguzi na siyo uchafuzi, na mfumo ni wa demokrasia na siyo demoghasia na kuwa mwisho wa siku watawala hawageuki kuwa watuwala.
Leo umeongea ukweli una siku nyingi Sana husemi Maneno mazito Kama Haya
 
Back
Top Bottom