Haya yanayoendelea kwenye kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi, yamedhihirisha pasi na shaka kile tunachosema kila siku rais na chama chake hawakubaliki, bali hutisha watu ili waonekane wanakubalika. Haiwezekani useme unakubalika, siasa ufanye mwenyewe ww na chama chako, hujuma ufanyie wapinzani wako, kisha siku ya ukweli wa hiyo hadithi kuwa unakubalika watu hawatokei kupiga kura. Hii inathibitisha wananchi wana uelewa wa kupima mambo, na wanafahamu fika uhuru na demokrasia yao hauporwi kwa sababu ya uwepo wa vitu.
Kuna dhana potofu ya kwamba, wananchi ni majuha hawajui au hawajitambui.
Kuna kusahau kuwa Tanzania ya 1951, 1961, 1981 na 2019 ni tofauti kabisa.
Hili la wananchi kususia kujiandikisha ni ujumbe mzito sana.
Wananchi hawasusii uchaguzi kama tukio , wanasuasia mchakato mzima
Wananchi wanajua kura zao hazina maana, isipokuwa uwepo wao vituo vya kura una maana ya kuhalalisha hujuma dhidi ya kura zao.
Ikiwa wasimamizi wameambiwa wasitangaze mshindani nje ya CCM! kura ina maana gani?
Ikiwa NEC wapo, hawakemei vitendo vya ''dhulma'' kwasababu vinafanywa na wateuzi wao , kura ina maana gani?
Ikiwa NEC wanaruhusu watumishi wao kukimbia ofisi ili wasipokee fomu za wasiowataka, kura ina maana gani?
Ikiwa Polisi wanaimba nyimbo za vyama achilia mbali kusherehekea ushindi wa chama ndani ya Barracks, kura ina maana gani?
Ikiwa DC kaamuriwa ''ole wako' eneo lako lipoteze ushindi, na DC huyu ndiye mkuu wa vyombo vya usalama, kura ina maana gani?
Ikiwa kampeni ni za chama kimoja, kura ina maana gani?
Ukisikia wanasisitiza kuhusu kujiandikisha, si kwamba wanahitaji ushiriki wako katika mchakato wa utawala, la hasha! hawahitaji kura yako kwasababu haiwezi kubadili kilichopangwa.
Wanahitaji uwepo wako ili kuhalalisha mchakato wa uchaguzi!