Uchaguzi 2020 Uchaguzi Mkuu 2020 bila Tume huru wala Waangalizi wa Kimataifa

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,921
31,161
Heshima kwenu Ndugu wanajamvi,

Dalili zote zinaonyesha uchaguzi mkuu wa Rais,Wabunge na madiwani utafanyika October 2020.

Ni wazi yapo mambo mawili ambayo hayajakaa sawa.

Mosi ni Tume huru ya uchaguzi.Suala hili limekuwa likipigiwa debe na wadau mbali mbali wakiwemo wansiasa,viongozi wa dini na jumuiya ya kimataifa.Tumekuwa na uchaguzi mkuu tangu mwaka 1995 na tume hii ambayo sasa inalalamikiwa na wadau mbali mbali.Katika chaguzi zilizopita pamoja na ubovu wa tume lakini walionyesha uwanja sawa wasiasa.Chaguzi ndogo za marudio Tume ilipwaya sana na kuonyesha kiwango cha upendeleo ambao haupata kutokea tangu kuundwa kwa taifa leo.Tumeona wakurugenzi wakijificha wakati wapinzania wakirejesha au kuchukua fomu.

Ni wazi tena pasipo shaka uchaguzi mkuu wa October 2020 tutawaona wakurugenzi wakiwakimbia wapinzani katika level mbali mbali,tunshuhudia wapinzani walioshinda wakitangazwa wameshindwa,tutashuhudia wananchi wakiporwa haki za kuchagua kiongozi wanayemtaka,tutashuhudia vituko kuliko uchaguzi wa serekali za mitaa.

Uchaguzi mkuu 2020 utafanyika katika mazingira ambayo Dunia imekumbwa na ugonjwa wa CORONA sioni waangalizi wa uchaguzi wa kimataifa wakitia mguu Tanzania.Hii bahati mbaya la hasha wanajua ugonjwa wa CORONA ni tishio hawatakuwa tayari kuhatarisha maisha yao kwaajili ya uchaguzi wa Tanzania.

Mazingira haya ya uchaguzi 2020 October ni rafiki kwa chama kinachopenda kuiba kura,kukandamiza haki za wananchi wake kuchagua viongozi wanaowataka.Ni hakika uchaguzi huu wagombea wa CCM watasaidiwa na tume na vyombo vya dola.

Vyama vya upinzani sijui kama wamejiandaa kukabiliana na hujuma ambazo wakati huu zitakuwa kubwa kuliko kipindi kingine chochote katika uhai wao.Tumesikia kupitia viongozi wa upinzani John Mnyika kwamba mawakala hawatapewa fomu sijui wamejiandaa vipi kukabiliana na hicho kitisho.Kwasababu kama mgombea wa upinzania atashinda halafu akatangazwa mgombea wa CCM mkienda mahakamani mtatakiwa kuleta ushahidi sasa sijui mtepeleka vielelezo gani ?.

Nadhani badala ya vyama vya upinzani kukimbilia kututangazia idadi ya wagombea waliochukua fomu za kugombea uRais ni vyema wakapambana kisheria kwa kuipeleka tume na mwanasheria mkuu wa serekali Mahakamani na si kusubiri kushindwa halafu mkaja na maelezo yasiyokuwa na maana.Sijasikia Katibu Mkuu wa ACT au CDM wakiwaleza wapiga kura namna walivyojiandaa na uchaguzi huu wakati wanaelewa tayari yapo mazingira mabovu.
 
Well said.nadhani ni vyema vyama vyote kujitathimini juu ya huu uchaguzi nashauri serikali ijitathimi vyema ili kuleta haki ya mwananchi/mwanachama .

CCM, CHADEMA na wengine wote wajitafakari .
 
Ccm haiwezi kukubali uwepo wa Tume huru maana wanajua hawawezi kushinda uchaguzi wowote huru.

Tume huru inawezekana kuanzishwa kwa shuruti tuu
 
Yaani ikosekane Tume Huru na hao waangalizi wakosekane, then jukumu lote litahamia kwa wapiga kura kulinda kura zao, tukikimbia maji ya kuwasha ndio itakuwa the end of our story.

Lakini kwa namna tunavyoonekana sasa kwenye jumuia ya kimataifa, na itategemea hali ya Corona itakavyokuwa mpaka kufikia mwezi October, hao jamaa wanaweza kuwepo.
 
Ccm haiwezi kukubali uwepo wa Tume huru maana wanajua hawawezi kushinda uchaguzi wowote huru.

Tume huru inawezekana kuanzishwa kwa shuruti tuu

Ni kweli lakini ACT & CDM wamefanya nini mpaka sasa !.

Nilitegemea kama vyama makini wangetafuta njia nyingine mbadala kama kuangalia uwezekano wa kwenda mahakamani kupinga maamuzi ya tume kuwanyima fomu mawakala.Mahakama kuu au Mahakama ya Katiba au Mahakama ya Afrika ?.Badala yake ACT wanafurahia kupokea wabunge 21 kutoka CUF hii si habari hata kidogo huu ni ujinga napenda kuwaambia wapo waTanzania makini wanatarajia mambo ya maana kutoka kwako.CDM wanakazana kutuletea majina ya wanachama wanaotarajia kugombea uRais huu n upuuzi wa kiwango cha SGR yaani badala ya kupambana na vikwazo vya tume wanakazana kuopokea majina ya nini ?.

Nilitarajia vyama makini vingepaza sauti kupitia balozi mbali mbali na mashirika ya umoja wa mataifa kuelekea uchaguzi 2020 lakini wapo kimya utafikiri kila kitu kipo sawa nilifikiri uchaguzi wa serekali za mitaa uliwafunza kitu kumbe badooo.

Salary Slip Erythrocyte @
 
Ni kweli lakini ACT & CDM wamefanya nini mpaka sasa !.

Nilitegemea kama vyama makini wangetafuta njia nyingine mbadala kama kuangalia uwezekano wa kwenda mahakamani kupinga maamuzi ya tume kuwanyima fomu mawakala.Mahakama kuu au Mahakama ya Katiba au Mahakama ya Afrika ?.Badala yake ACT wanafurahia kupokea wabunge 21 kutoka CUF hii si habari hata kidogo huu ni ujinga napenda kuwaambia wapo waTanzania makini wanatarajia mambo ya maana kutoka kwako.CDM wanakazana kutuletea majina ya wanachama wanaotarajia kugombea uRais huu n upuuzi wa kiwango cha SGR yaani badala ya kupambana na vikwazo vya tume wanakazana kuopokea majina ya nini ?.

Nilitarajia vyama makini vingepaza sauti kupitia balozi mbali mbali na mashirika ya umoja wa mataifa kuelekea uchaguzi 2020 lakini wapo kimya utafikiri kila kitu kipo sawa nilifikiri uchaguzi wa serekali za mitaa uliwafunza kitu kumbe badooo.

Salary Slip Erythrocyte @
Nitarudi mkuu
 
Heshima kwenu Ndugu wanajamvi,

Dalili zote zinaonyesha uchaguzi mkuu wa Rais,Wabunge na madiwani utafanyika October 2020.

Ni wazi yapo mambo mawili ambayo hayajakaa sawa.

Mosi ni Tume huru ya uchaguzi.Suala hili limekuwa likipigiwa debe na wadau mbali mbali wakiwemo wansiasa,viongozi wa dini na jumuiya ya kimataifa.Tumekuwa na uchaguzi mkuu tangu mwaka 1995 na tume hii ambayo sasa inalalamikiwa na wadau mbali mbali.Katika chaguzi zilizopita pamoja na ubovu wa tume lakini walionyesha uwanja sawa wasiasa.Chaguzi ndogo za marudio Tume ilipwaya sana na kuonyesha kiwango cha upendeleo ambao haupata kutokea tangu kuundwa kwa taifa leo.Tumeona wakurugenzi wakijificha wakati wapinzania wakirejesha au kuchukua fomu.

Ni wazi tena pasipo shaka uchaguzi mkuu wa October 2020 tutawaona wakurugenzi wakiwakimbia wapinzani katika level mbali mbali,tunshuhudia wapinzani walioshinda wakitangazwa wameshindwa,tutashuhudia wananchi wakiporwa haki za kuchagua kiongozi wanayemtaka,tutashuhudia vituko kuliko uchaguzi wa serekali za mitaa.

Uchaguzi mkuu 2020 utafanyika katika mazingira ambayo Dunia imekumbwa na ugonjwa wa CORONA sioni waangalizi wa uchaguzi wa kimataifa wakitia mguu Tanzania.Hii bahati mbaya la hasha wanajua ugonjwa wa CORONA ni tishio hawatakuwa tayari kuhatarisha maisha yao kwaajili ya uchaguzi wa Tanzania.

Mazingira haya ya uchaguzi 2020 October ni rafiki kwa chama kinachopenda kuiba kura,kukandamiza haki za wananchi wake kuchagua viongozi wanaowataka.Ni hakika uchaguzi huu wagombea wa CCM watasaidiwa na tume na vyombo vya dola.

Vyama vya upinzani sijui kama wamejiandaa kukabiliana na hujuma ambazo wakati huu zitakuwa kubwa kuliko kipindi kingine chochote katika uhai wao.Tumesikia kupitia viongozi wa upinzani John Mnyika kwamba mawakala hawatapewa fomu sijui wamejiandaa vipi kukabiliana na hicho kitisho.Kwasababu kama mgombea wa upinzania atashinda halafu akatangazwa mgombea wa CCM mkienda mahakamani mtatakiwa kuleta ushahidi sasa sijui mtepeleka vielelezo gani ?.

Nadhani badala ya vyama vya upinzani kukimbilia kututangazia idadi ya wagombea waliochukua fomu za kugombea uRais ni vyema wakapambana kisheria kwa kuipeleka tume na mwanasheria mkuu wa serekali Mahakamani na si kusubiri kushindwa halafu mkaja na maelezo yasiyokuwa na maana.Sijasikia Katibu Mkuu wa ACT au CDM wakiwaleza wapiga kura namna walivyojiandaa na uchaguzi huu wakati wanaelewa tayari yapo mazingira mabovu.
Uko sahihi mkuu hakika bila Tume Huru Vyama vya Upinzani vingeacha Kushiriki Uchaguzi huu,Wakumbuke Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ulivyokuwa
 
Hivi kumbe hao waangalizi wa kimataifa ni big deal sana?

Ni UCHAGUZI MKUU wa mwaka gani Tz wamewahi kusema haukuwa wa huru na haki?

Na ni mwaka gani upinzani umewahi kukubali uchaguzi kuwa huru na haki?
 
Ni kweli lakini ACT & CDM wamefanya nini mpaka sasa !.

Nilitegemea kama vyama makini wangetafuta njia nyingine mbadala kama kuangalia uwezekano wa kwenda mahakamani kupinga maamuzi ya tume kuwanyima fomu mawakala.Mahakama kuu au Mahakama ya Katiba au Mahakama ya Afrika ?.Badala yake ACT wanafurahia kupokea wabunge 21 kutoka CUF hii si habari hata kidogo huu ni ujinga napenda kuwaambia wapo waTanzania makini wanatarajia mambo ya maana kutoka kwako.CDM wanakazana kutuletea majina ya wanachama wanaotarajia kugombea uRais huu n upuuzi wa kiwango cha SGR yaani badala ya kupambana na vikwazo vya tume wanakazana kuopokea majina ya nini ?.

Nilitarajia vyama makini vingepaza sauti kupitia balozi mbali mbali na mashirika ya umoja wa mataifa kuelekea uchaguzi 2020 lakini wapo kimya utafikiri kila kitu kipo sawa nilifikiri uchaguzi wa serekali za mitaa uliwafunza kitu kumbe badooo.

Salary Slip Erythrocyte @

Mkuu nashukuru umeona jambo ninaloliona kuhusu tume huru ya uchaguzi. Kabla ya kutangazwa kwa janga la Corona cdm ilisema itafanya mikutano nchi nzima, na ajenda ya kutoka nayo ilikuwa ni kudai tume huru ya uchaguzi. Joto lile lilikuwa limekaa vizuri kimkakati, ajabu baada ya bunge kuvunjwa sisikii sauti ya kudai tena tume huru ya uchaguzi, bali naona wapinzani kuridhika kuingia kwenye uchaguzi bila uwepo wa tume hiyo!

Ni hivi, hapa tulipofikia ni vyema wapiga kura wa upinzani, tuwaambie viongozi wa vyama vya upinzani kuingia kwenye huu uchaguzi bila tume huru ya uchaguzi ni kupoteza muda na raslimali fedha, kwani wengi wetu hatutashiriki huo uhuni, na wao ndio watapoteza maana wapiga kura wa ccm wao hawawezi kudhurika na matokeo ya dhuluma. Ni vyema wapinzani kudai tume huru ya uchaguzi, kuliko kishiriki kubariki uchaguzi wa hujuma. Ccm hawaogopi kufanya hujuma kwenye uchaguzi, bali wasilolitaka ni wapinzani kususia huo uchaguzi, maana wanajua utakuwa na impact mbaya kwao na taswira mbaya duniani. Tuwahimize kutangaza kuwania uchaguzi huu ni lazima ufanyike chini ya tume huru ya uchaguzi.
 
Sasa mahakama ziko wapi hapa. Mimi naona hivi ni vyombo vya kisheria vya ccm kuwasadia kutawala.

Ukiona wawekezaji wa nje kwenye mikataba yao kile kifungu kinachohusika na mambo ya suluhu wamesema suluhu itafanyika nje ya Tanzania ujue wana akili sana.

Waliishaona hapa hakuna mahakama, waliishajua watafanyiwa uhuni tu kama wanavyofanyiwa wapinzani.

Sasa nakushangaa wewe unayesema eti wapinzani waende mahakamani inaonekana wewe huishi Tanzania hii, inaonekana uko nje ya nchi.
 
Dalili zote zinaonyesha uchaguzi mkuu wa Rais,Wabunge na madiwani utafanyika October 2020.

Ni wazi yapo mambo ambayo hayajakaa sawa.

Mosi ni Tume huru ya uchaguzi.
Kwa mujibu wa sheria iliyounda Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC ni tume huru ila sio Shirikishi.
Pascal Mayalla: NEC ni Tume huru ya uchaguzi kama lilivyo bunge na mahakama kwa sababu vyote hivi msingi wake ni Rais

TV Prog. Alert: Tume ya Uchaguzi, NEC, Yajibu Hoja za JF Kuhusu Uchaguzi Huru na Wa Haki!

P
 
Urejee na majibu ya maana kweli kweli leo tarehe 21 June 2020 ACT & CDM wanafanya nini kupinga hii dhulma sitaki ngonjera.Katibu Mkuu John Mnyika alituambia kungekuwa na marekebisho kabla bunge halijavunjwa,Bunge limevunjwa hakuna marekebisho what's plan B !.
nitakuja mkuu
 
Heshima kwenu Ndugu wanajamvi,

Dalili zote zinaonyesha uchaguzi mkuu wa Rais,Wabunge na madiwani utafanyika October 2020.

Ni wazi yapo mambo mawili ambayo hayajakaa sawa.

Mosi ni Tume huru ya uchaguzi.Suala hili limekuwa likipigiwa debe na wadau mbali mbali wakiwemo wansiasa,viongozi wa dini na jumuiya ya kimataifa.Tumekuwa na uchaguzi mkuu tangu mwaka 1995 na tume hii ambayo sasa inalalamikiwa na wadau mbali mbali.Katika chaguzi zilizopita pamoja na ubovu wa tume lakini walionyesha uwanja sawa wasiasa.Chaguzi ndogo za marudio Tume ilipwaya sana na kuonyesha kiwango cha upendeleo ambao haupata kutokea tangu kuundwa kwa taifa leo.Tumeona wakurugenzi wakijificha wakati wapinzania wakirejesha au kuchukua fomu.

Ni wazi tena pasipo shaka uchaguzi mkuu wa October 2020 tutawaona wakurugenzi wakiwakimbia wapinzani katika level mbali mbali,tunshuhudia wapinzani walioshinda wakitangazwa wameshindwa,tutashuhudia wananchi wakiporwa haki za kuchagua kiongozi wanayemtaka,tutashuhudia vituko kuliko uchaguzi wa serekali za mitaa.

Uchaguzi mkuu 2020 utafanyika katika mazingira ambayo Dunia imekumbwa na ugonjwa wa CORONA sioni waangalizi wa uchaguzi wa kimataifa wakitia mguu Tanzania.Hii bahati mbaya la hasha wanajua ugonjwa wa CORONA ni tishio hawatakuwa tayari kuhatarisha maisha yao kwaajili ya uchaguzi wa Tanzania.

Mazingira haya ya uchaguzi 2020 October ni rafiki kwa chama kinachopenda kuiba kura,kukandamiza haki za wananchi wake kuchagua viongozi wanaowataka.Ni hakika uchaguzi huu wagombea wa CCM watasaidiwa na tume na vyombo vya dola.

Vyama vya upinzani sijui kama wamejiandaa kukabiliana na hujuma ambazo wakati huu zitakuwa kubwa kuliko kipindi kingine chochote katika uhai wao.Tumesikia kupitia viongozi wa upinzani John Mnyika kwamba mawakala hawatapewa fomu sijui wamejiandaa vipi kukabiliana na hicho kitisho.Kwasababu kama mgombea wa upinzania atashinda halafu akatangazwa mgombea wa CCM mkienda mahakamani mtatakiwa kuleta ushahidi sasa sijui mtepeleka vielelezo gani ?.

Nadhani badala ya vyama vya upinzani kukimbilia kututangazia idadi ya wagombea waliochukua fomu za kugombea uRais ni vyema wakapambana kisheria kwa kuipeleka tume na mwanasheria mkuu wa serekali Mahakamani na si kusubiri kushindwa halafu mkaja na maelezo yasiyokuwa na maana.Sijasikia Katibu Mkuu wa ACT au CDM wakiwaleza wapiga kura namna walivyojiandaa na uchaguzi huu wakati wanaelewa tayari yapo mazingira mabovu.
Utawala wa kidikteta ndivyo unavyokuwa.
 
Kwa mtazamo wangu upinzani wa Tanzania umetetereka sana hasa baada ya KUB kung'ang'ania uenyekiti wa Chama kikuu cha upinzani. Angefanya mabadiliko naamini Upinzani kidoogo ungeweza isumbua CCM. Ila kwa sasa ni CCM NAMBARI WANI
 
Mjotathmini sana kabla watanzania hawajatathmini wao, na yasijewakuta yaliyowakuta kwa kufukuzwa mwanza na wananchi wakati mkizunguka na maiti ya marehemu A,mawazo.
 
Back
Top Bottom