Uchaguzi DRC: Upinzani waandamana kupinga uchaguzi, polisi wafanikiwa kuwazima

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,625
1703749625828.png

Polisi katika mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kinshasa imewazuwia waandamanaji kukusanyika siku ya Jumatano 27/12/2023, baada ya kuandamana dhidi ya uchaguzi wa hivi karibuni katika taifa hilo tete la Afrika ya Kati.

Wanasiasa wakuu wa upinzani katika nchi maskini lakini yenye utajiri wa madini nchini DRC waliitisha maandamano hayo baada ya kukataa kura ya wiki iliyopita, ambayo ilikumbwa na ucheleweshaji mkubwa na mtafaruku wa ukiritimba.

Waziri wa mambo ya ndani wa Kongo Peter Kazadi alisema Jumanne serikali ilipiga marufuku maandamano hayo kwa sababu "yanalenga kuharibu mchakato wa uchaguzi."

Upinzani hata hivyo ulikuwa umewataka wafuasi wake kukusanyika karibu na bunge la kitaifa mjini Kinshasa na kuandamana hadi makao makuu ya tume ya uchaguzi nchini humo.

DW Kiswahili
 
Back
Top Bottom