Maelfu waandamana Serbia kupinga matokeo ya uchaguzi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,502
9,282
Maelfu ya watu wameandamana Jumamosi katika mji mkuu wa Serbia, Belgrade, huku wakipiga zogo kwa kumshutumu rais wa nchi hiyo Aleksandar Vucic kuendesha udanganyifu wakati wa uchaguzi wa bunge na serikali za mitaa.

Kwa karibu wiki mbili sasa, Serbia imekuwa ikishuhudia maandamano makubwa ya kupinga kasoro zilizoshuhudiwa wakati wa uchaguzi huo uliofanyika Desemba 17 mwaka huu, kasoro zilizoainishwa pia na waangalizi wa kimataifa wa uchaguzi.

Chama tawala cha Serbian Progressive Party kilitangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi huo lakini muungano mkuu wa upinzani wa Serbia Against Violence, unadai kuwepo wizi wa kura na wameomba kuwepo tume ya kuchunguza kasoro hizo na ikihitajika uchaguzi huo urudiwe.


DW
 
Back
Top Bottom