Ubora na bei za tecno smartphones

Ubora na bei za tecno smartphones

Nimepata mwanga kwenye P5 na Phantom A. Vipi hizo nyingine?
 
Zinatofautiana kidogo sana hususan ktk grafx na pixel ram na internal storage bt ni poa sn nokia na i phones walibweteka sn wakidhan wao ndo kila kitu.
 
hizo simu ndio kimbilio letu,hatuangalii majina sisi bali specifications,durability na capability,zina kila kitu aisee na ukienda google store ndio kabisaaaaa,cjawahi kujuta kununua hii simu aisee,ni p3 tu,hzo phantom ndio usipime,hata hzo zenye majina zinazidiwa kwa mbali sana

endelea kujidanganya! Simu wala haipo kwenye mtandao wa simu gsmarena... Ipo kwenye ma blog tu!!
 
techno hawana spare.


Spare za nini tena kwenye simu?

Tatizo wabongo wamezoea kukaa na bidhaa hadi inalingana umri na mtoto wake. Maintenance hadi kwenye simu?

Note that, hakuna mtz yoyote anayemzidi akili machina,hata kama mchina huyo ana miaka duniani..
 
endelea kujidanganya! Simu wala haipo kwenye mtandao wa simu gsmarena... Ipo kwenye ma blog tu!!

Sa nijidanganye nn wakati karibia kila kitu kifanywacho na simu zenu zenye majina simu yng pia inafanya na simu ina muda mrefu tokea niinunue na haijawahi kunisumbua, wabongo acheni kukremu,

Mnapigwa kwa misimu yenu mnayoiamini lakini nyie mpo tu,yaani kama mizukule vile aisee, poleni, endeleeni kutapeliwa na muwatajirishe watu kupitia ulimbukeni wenu wa kukariri !
 
Kuna kitu kisichofanyiwa maintenance ni lazima acha ubazazi kama ni promo nenda mkoa kwa akina wasira. Hizo ni sim cheap sana lakin adha yake ni kubwa sana. Ningekupa big up sana walau ungewazungumzia samsung maana kila watu kumi wenye sim watono au zaid watakua na samsung.

Ndo mchina ambae nampa pongezi sio hao wajinga wako.
 
Sa nijidanganye nn wakati karibia kila kitu kifanywacho na simu zenu zenye majina simu yng pia inafanya na simu ina muda mrefu tokea niinunue na haijawahi kunisumbua,wabongo acheni kukremu,

mnapigwa kwa misimu yenu mnayoiamini lakini nyie mpo tu,yaani kama mizukule vile aisee,poleni,endeleeni kutapeliwa na muwatajirishe watu kupitia ulimbukeni wenu wa kukariri!!

Mchna ni mchna tu hata sku moja huwez kusema ni imara hata sku moja. Ni unafuu wa bei na mbwembwe za muonekano wa bidhaa za kchna tu vnawavutia weng wanachkua lakn hamna kila kitu hapo
 
mchna ni mchna tu hata sku moja huwez kusema ni imara hata sku moja. Ni unafuu wa bei na mbwembwe za muonekano wa bidhaa za kchna tu vnawavutia weng wanachkua lakn hamna kila kitu hapo

Duh! kumuelewesha mbongo ni kazi kubwa sana na ndio maana hata kumuelimisha pia ni gharama sana kwani kila mara atarepeat a year kwa kufeli mara kwa mara,itabidi alipiwe ada tena,wakati kuna wengine nao walitakiwa kulipiwa hyo fedha ili wasome,

Mkuu umewahi kutumia tecno za hizi series tunazoziongelea au umekariri tu michina sio simu,unazijua Huawei ascend y300 kaka? nazo ni michina, kama huna taarifa mkuu

hao wenye masimu yenye majina mnaowaaminia wapo matumbojoto kutokana na uwezo wa hizo simu unazozidharau kwani zinawaharibia soko lao,fanya utafiti kwa watumiaji wa michina hyo uone wanakupa ripot zipi kuhusiana na ubora wa hizi simu kaka,upo??
 
steveachi

Wewe ongelea tecno ambayo inayoongelewa kwenye ma blog tuu.. HUAWEI ni mambo mengine. Si kweli simu za kichina ni feki... Hata tecno sio feki.. Ila inatengenezwa na material za low quality. Ukisikia mtu unaweza kupata cancer ya ubongo kwa ajili ta kuongea na simu sana basi hapo tunaongelea simu aina ya tecno na zengine zote zenye low quality hardware.

Halafu kuna jamaa alikuja hapa akasema nyie mnaonunua tecno mnapigwa sana maana kwa low quality phone kama hiyo mlitakiwa TECNO phantom muinunue kwa laki mbili za kibongo. Sio laki 4. Huko china hata watumiaji wa tecno hawapo.. Wapo africa tu. Kule kuna masimu ya kufa mtu.. Xiaomi n.k bei chee!
 
Last edited by a moderator:
kinyoba

Hahahahahahahahahahaaaaa,nimegundua nini ujue mkuu,mliopigwa kwa kununua misimu ya bei kubwa mna wivu sana na tecno kwa kuwa ni durable,capable na zina kila kitu ambacho simu zenu za bei kubwa zilichonacho,

so mnabakia na jealosy,ooooh michina,oooh mionzi n.k,wakati kabla hata michina haijaanza kuingia habari za simu za mikononi kuwa zina madhara yenye mionzi tumeshazisikia,so hyo sio habari mpya,manikoleza tu kutokakana na wivu wenu,teh teh teh teh
 
Last edited by a moderator:
True. Tatizo watu hawaelewi nadhani. Kinachomatter ni unataka nini kwenye simu. Camera ya ukubwa upi? Uwezo wa simu upi? Battery inaweza kaa muda gani nk.

Kusema TECNO haifai ni kosa. Haifai kwako. Mbona unaendesha Vitz badala ya Pollo au Golf kama unajifanya ni mtu wa quality? Na isitoshe TECNO inauwezo mkubwa wa kutunza charge zaidi ya smartphones zingine.

Nunua bro wasikubabaishe. Phantom. Ni zaidi ya simu. WIFI yake ina nguvu balaa.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Oya, oya..., OYA WAKUU! Mbona mmeenda nje ya mada jamani! Niliyeanzisha thread ni mimi na nimeshapata picha kuhusu ubora kutokana na michango yenu japo mmegeneralize tu simu za kichina. Naomba sasa kujua bei ya simu nilizooridhesha katika soko la Tanzania. Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom