Ubobezi katika sheria wa Tulia Ackson ni upi?

Nzi

unapoteza muda wako

article ndeefu kisa unataka kum dis mtu?

unafahamu journals ngapi dunia hii?

unafikiri waalimu wa UDSM ni vilaza? ulizia mkuu

suppose sio au hana elimu au hana ubobezi, unachotaka kusema nini hasa

Ni naibu spika, wewe haujawa, ni PhD holder wewe hauna,ni notable figure wewe ni NZI TU

Punguza jazba.
Nyie ndiyo mmempa promo sasa watafiti wamemgoogle wamepata taatifa zake ghafla fisiemu mnapanic.
 
..mleta uzi umechambua vizuri na emetiririka kimantiki.tatizo hapa kuna ushabiki ambao hauna maana na kuna watu wanahisi wao tu ndio wanaijua sana UD..ni upuuzi na kujilisha upepo.ukweli ni ukweli
 
Mkuu kwa nilivyoona mimi binafsi sikudhani kama msingi wa hoja yako ya KUBOBEA umejikita kwenye "machapisho" sababu kwanza kitendo tu chakuwa na PHd kina maana lazima utakua na machapisho, swala la kuyaweka mtandaoni au la hakufanyi mtu kuwa mbobezi
Lakini pili swala la machapisho kuwa cited bado inategemea na chanzo cha habari yako ambacho kililalia zaidi oline, kwa mazingira yetu ya kibongo

Pengine nikubaliane na wewe kwamba kupitia online Dr Tulia hajafanya vizuri sana, nakushauri jaribu kwenda mbali zaidi kwenye utafiti wako mkuu kutafuta data zingine zaidi ya online naamini utapata kitu na utakua katika kipimo kizuri cha kujua ubobezi wake

Lakini mkuu Kama mpaka karne ya leo utafiti wako hauwezi kuwa online si kuna tatizo hapo? Most of the consultancy for example zinaanzia online, sasa kama hayupo online atakuwa active kweli?
 


Sawa leteni sasa na Machapisho ya Tundu Lisu halafu tulinganishe!


Sasa hii kazi ya Tundu Lissu tumekuchagua wewe ukafanye utafiti ulete hapa tuutazame kiroho safi.
In short burden of proof kuwa Tundu lisu sio mbobezi kwenye sheria iko mikononi mwako.
 
Lakini mkuu Kama mpaka karne ya leo utafiti wako hauwezi kuwa online si kuna tatizo hapo? Most of the consultancy for example zinaanzia online, sasa kama hayupo online atakuwa active kweli?

Uko sahihi mkuu. Journal zote muhimu ziko online na paper zao zote unasema kuzipata ama bure au kwa kununua cash/annual subscription ya mtu binafsi au taasis. Ila journal nyingi za nchi zetu hazipo online na hazina impact factor. Kwa mtaalamu makini utapeleka huko chapisho lako kama limekataliwa na journal makini au kama linafaa kwa matukizi ya ndani.
 
Sasa hii kazi ya Tundu Lissu tumekuchagua wewe ukafanye utafiti ulete hapa tuutazame kiroho safi.
In short burden of proof kuwa Tundu lisu sio mbobezi kwenye sheria iko mikononi mwako.

Ni muhimu watu wakajua kwamba ubobezi mwanataaluma na mtemdaji au practioner unatofautiana. Sina hakika Kama Lisu ni mwanataaluma.
 
Uko sahihi mkuu. Journal zote muhimu ziko online na paper zao zote unasema kuzipata ama bure au kwa kununua cash/annual subscription ya mtu binafsi au taasis. Ila journal nyingi za nchi zetu hazipo online na hazina impact factor. Kwa mtaalamu makini utapeleka huko chapisho lako kama limekataliwa na journal makini au kama linafaa kwa matukizi ya ndani.

Kabisa mkuu. Hiyo ndiyo practice....

Ni muhimu watu wakajua kwamba ubobezi mwanataaluma na mtemdaji au practioner unatofautiana. Sina hakika Kama Lisu ni mwanataaluma.

Mkuu hawa watu wengine ni wa kuwashangaa tu....sasa unajiuliza mtu unaanzaje kuwalinganisha Lissu na Tulia kwa kutumia muktadha wa ubobezi wa kisheria kwenye akademia? Jambo la kuhuzunisha ni kwamba unaweza kukuta hawa wanaoongea hivi ndiyo washauri wa CCM..
 
Mazee, asante kwa hii video. Napenda sana alichokisema kuanzia dakika ya 2.20 hadi 2.44. Amesema:

"...ninajiamini, nina uwezo na kazi ya naibu spika na spika ni kutafsiri kanuni za Bunge, sheria za nchi na pia katiba. Na mimi haya ndiyo maeneo ambayo nimebobea kikazi"

Amebobea kikazi kwenye kutafsiri kanuni za Bunge, sheria za nchi na katiba?!? Haya wanamwona huyu ni mbobezi katika maeneo hayo walete ushahidi. Maana kwenye utafiti huo usio rasmi, sijaona kubobea kwake.

Huyu bidada hajielewi kumbe! Hakika hii ni mbeleko. Angebaki kufundisha tu sheria au kuwa naibu mwanasheria mkuu...maana hapo Bunge kuaibika kwake is bound to happen. Na yeye ni mfano wa 'wabobezi' na 'wasomi' wajanja waliojaa Tanzania chini ya CCM.
Mkuu nzi kwa wenye akili wamekuelewa vizuri sana! Huo ubobezi wa kanuni za bunge alifanyia bunge gani au lile la siki 90? Mbona alikua benchi? Kazi ya ubobezi wa kutafsiri sheria za nchi hua ni kwa mawakili waliohangaika na kesi za mashtaka miaka mingi kama kina Lissu na Change! Sasa huyu binti uwakili wake practical ilikua ya kesi ngapi?
 
Wataalamu wa lugha wangetuambia kuwa neno "kubobea" lina maana gani? Baada ya hapo tusome bango la mkuu Nzi.
Kubobea kwa kiingereza lina maana ya "specialization". Dr. Tulia Akson amebobea "specialized" katika maswala ya sheria. Sioni kuna kosa. "Daktari amebobea kwenye magonjwa ya wanawake", n.k . Labda kama mnataka kuleta siasa, lakini Dr. Tulia amebobea kwenye maswala ya sheria.

bobea - jishughulisha na jambo fulani kupita kiasi/jifunza jambo na kulifahamu barabara: (TUKI) mfano: Tulia amebobea sana katika sheria.
 
Hivi tukimchukua Dr.Tulia tukamlinganisha na Mh.Ndugai na mama Makinda mathalani, hivi hawa kwenye ubobezi wa sheria wapo sawa? Hivi hili neno kubobea nd'o linalotoa mtu roho kujaribu kufanya mjadala usioisha? Basi tufanye DrTulia ni msomi mzamivu wa sheria hajabobea kama ambavyo inaonekana Nzi,Nyani Ngabu and Co hilo linawatesa sana. Manake hata tujadili vipi habari haibadiliki nd'o naibu spika sasa yupo anakula bata sasa. Na si mbobezi.

Ni kiongozi wa Mhimili wa serikali ndo maana tunajiridhisha kwa kinachosemwa na wapambe wake.
Kuchambua ubobezi wake hakutabadili nafasi yake bungeni.
Inaoneka unateseka sana kumjadili kiongozi wetu.
 
Back
Top Bottom