Yote tisa, kumi hii habari ni hearsay. Kwa principle za journalism, huyo mwandishi kapata tip toka kwa mmoja wa wajumbe. Alitakiwa kufanya homework yake vizuri to seek attribution from competant authority, hata kama wasinge ongea. Other wise angetafuta collaboration toka kwa angalau wajumbe wengine wawili.
Hizi news za single source has always leave a room for doubt maana zina hatari kubwa ya exegaration na Tanzania tuna bahati ya kuwa na wanasheria wachache, otherwise magazeti mengi yangeshafilisiwa long ago.
Naombeni wana JF msinishambulie my comments has nothing to do na utetezi wa Mkapa, bali Journalism Professionalism and Ethics.
Pasco,
Hiki ki-habari cha TanzaniaDaima ni udaku mtupu. Mkapa ana soo la kubinafsisha mgodi na partner in crime wake Daniel Yona ana kesi mahakamani kuhusiana na haya haya ma hanky-panky ya dealings za serikali na wawekezaji, hawezi kujitia kitanzi kukiri makosa saa hizi.
Sio principle za journalism tu, hata za stori za mtaani haziendi hivyo. Hivi tukiwa tunamtafuta Juma atujibu kuhusu mali zetu halafu tunakuja kuambiwa kuna fulani kasema Juma kakiri kosa, hatutataka kujua huyo fulani anaesema Juma katubu ni nani, na nani mwingine alisikia wakati anatubu? Halafu alipokubali makosa alisema nini kuhusu mali zetu going forward? You know?
Halafu ki-habari kina misrepresent ukweli kwa kusema pressure ya kumshitaki Mkapa imeongezeka. Kila kukicha tunasikia padri so and so mbunge huyu na yule wanasema let this Mkapa character alone, sasa hiyo pressure iko wapi? Na Pinda keshapayuka kwamba it's a complicated process.
Kinga yenyewe walivyoiongelea ni misrepresentation tupu. Hakuna sehemu kwenye Katiba paliposema Wabunge wanaweza kuondoa kinga. Itabidili Wabunge waandike kipengele hicho cha Katiba upya, na hiyo ndio itahitaji theluthi mbili za wabunge, tena inabidi ipatikane kote Zanzibar na Bara separately.
Halafu Pasco, notice kwamba kwenye misingi journalism, ilibidi pale kwenye paragraph ya kwanza, au ya pili at the latest, waseme kwamba wanaripoti based on stori ya kuambiwa na anonymous source. Walivyoiweka ni kama wao Tanzania Daima ndio wanaripoti wakati hawana uhakika. Wakishitakiwa watasema sisi tumeambiwa na mtu, lakini hapa wameitengeneza kuwa-fool unwary readers kama wana uhakika vile. Wadaku.
Halafu, notice vi-taarifa ambavyo hawana uhakika hawatoi jina la mwandishi, wanavunja cardinal rule of journalism, inayotakiwa kuleta credibility na accontability.
Eti gazeti linaripoti kwa kuambiwa na mjumbe mmoja, udaku, uzushi, vilaza wakutupwa nje ya press room.