Ubinafsi mkubwa wa Serikali za Afrika

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,606
8,744
Kuna ubinafsi mkubwa ambao unashangaza wengi sana kwenye nchi zetu za Afrika na zinazoendelea. Mfano kwenye magari ya Serikali mimi naishi state ya Texas magari mengi ya Serikali ya hili jimbo ni Ford, Toyota, Nissan, Jeep .

Cha ajabu ukienda kuulizia Toyota wenyewe wanakwambia Gari za hapa USA zina viwango vya juu zaidi ya zile VX zinazotumwa Afrika! hata finishing za gari za huku ni mzuri na wa viwango vya juu sana. Bei kwa haya magari mapya ni kati ya $40,000-$50,000 kwa gari jipya toleo la 2021.

Cha ajabu serikali inanunua magari kati ya Tsh 220,000,000 mpaka 400,000,000 ambayo ni $98,000 mpaka $178,000. Hakuna sababu ya msingi kuona mpaka vyama vinanunua magari kwa pesa hii wakati sio yao ni pesa za wananchi.

Hivyo hapa naongelea matumizi ya Serikali sio binafsi. Kibaya zaidi magari mengi hayatumiki vilivyo hayaendi hata mbali!. Mshahara wa mfanyakazi wa Africa kwa wastani ni $200 kama tsh 500,0000 tu hivyo gari moja tu ina uwezo wa kulipa watu 40 laki tano kila mwezi kwa mwaka mzima! hebu jiulize.

Wakati huku unakuta mtu anatengeza $100,000 kwa mwaka na ananunua gari ya $25,000 tena kwa mkopo wa miaka 5. Sasa tutapigana madongo lakini nchi zetu bado zina matumizi mengi sana mabaya na viongozi wengi hawana uchungu na pesa za wananchi kama wanavyodai

1625766757027.png

1625766764821.png



1625766781727.png
 
Pesa ya wananchi Maskini inavyotumika na Wanasiasa unaweza kulia ndugu yangu. Ni UBINAFSI na ROHO MBAYA kupita maelezo.
 
Unajua kuwa TZ ni RHD? Labda Rwanda na nchi nyingine nje ya EAC wanaotumia LHD
 
MKUU Kwani kama Serikali ikiongea na kiwanda hawawezi kuwaweke RHD?
I think inawezekana ila hata zikiletwa hizo mashine from US bado tutalalamika zinakula mafuta sana. Kwa marekani gari kuwa na cc6200 ni kawaida.

Kama tatizo ni bei kubwa tuagize hata china gari tutapata za bei nafuu zaidi ya hapo.

Hizi ni sifa za kiujumla za magari kulingana na nchi/bara (maoni ya yangu tu) uchaguzi utabaki kwetu tu;
US - Unywaji mbovu wa mafuta, japo siku hizi wameeanza kujirudi kwa sababu za kimazingira. Full size SUV ya marekani kupata parking katikati ya miji yetu lazima utembee na panado mfuko kupunguza maumivu ya kichwa.

Ulaya - Over engineered, likipata shuruba ndio utajua hujui, kuletewa invoice ya 5M kwa ajili ya normal repair kama suspension itakuwa ni vitu vya kawaida.

Japan - Uvumilivu wa hali ya juu hasa kwa mazingira yetu ya kiafrika ambayo kuwekewa mafuta machafu yasiyo na viwango ni jambo la kawaida. Pili tayari dealers washajiestablish sana hivyo hata kupata spare ni rahisi sana.
 
Back
Top Bottom