KING MIDAS
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 10,569
- 21,075
WAMEMFANYIA MWENETU UBAYA UBWELA HUKO
SASA WANATAKA KUPELEKANA FIFA
Ishu nzima ilianza pale Captain aliposepa wakamsajili beki mmoja mzawa kutoka hapa hapa Timu za Ligi kuu Huyo beki ni mzuri sana lakini changamoto ni kwamba sio mzoefu wa mechi za kimataifa
sasa coach wao akasema anamtaka mwenetu na sisi Bila Hiyana tukawatajia Bei wakaanza kubembeleza mara watatulipa msimu ujao oooh mara Tuwape kwa mkopo kiufupi maneno yakawa mengi ila Mtee hawatoi Nadhani walitaka kurudia kama ya Jonathan Sowah
sasa baada ya Kuona kununua inakua Ghali wale wahuni wakaona wapite njia ya Uwani wakasema Hawamtaki Tena mwenetu hivyo Dili Limekufa Rasmi tukahamishia Majeshi hapa Ardhi ya Wameru kuweka Kambi
kumbe nyuma ya pazia wale Mawinga wanaendeleza mawasiliano na Mwenetu wakamuambia Avunje mkataba na sisi alafu wao ile pesa waliyokuwa Watupatie sisi kwa kumuuza watampa 75% Alafu mawinga watasepa na hiyo % Nyingine
Ghafla mwana akasema amekosa Furaha na anataka kurudi kwao Tukamuuliza Mbona ghafla sana akajibu hapana mimi nimechoka tu kuishi Tanzania sisi tukaona isiwe Tabu tumuachie Bure yeye akasema hapana anataka kuvunja mkataba wake aondoke kwa amani
tukakubaliana tukamuambia avunje mkataba akalipa nusu tukaachana kuja kushangaa siku 2 mbele tunamuona misri tena na Jersey ya mwafulani sasa wamemfanyia majaribio kocha kasema hapana anamtaka msauzi hivyo hana muda naye
mwenetu na mawinga wake sasa hivi Hazipandi mawinga wanataka kwenda sumbawanga na mwenetu sio haba Nigeria ni mwenyeji Acha Tusubiri tuone itakavyokuwa
View: https://www.facebook.com/100082243600932/posts/pfbid0RW7RgnuD8v3mhHAEiQFbniWqVgCmjgVFWaXgc8PazwQDy5zKFMYD8s2XQXEK4WUvl/?app=fbl