Ubaguzi huu utakoma lini?

Ubaguzi huu utakoma lini?

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
25,995
Reaction score
25,388
Leo nilikuwa nasikiliza redio ya Morning Star nikasikia tangazo hili la nafasi ya kazi ambalo limenishangaza sana:

1. Mwombaji awe ni muumini wa kanisa la Waadiventista wa Sabato (SDA) na aweze kuthibitisha hilo kwa maandishi.

2. Mwombaji awe ni mwenyeji wa Kanda ya Ziwa na hilo lithibitike kwenye cheti chake cha kuzaliwa.

3. Mwombaji awe na shahada ya kwanza ya uboharia (Material Management). Mwenye shahada ya pili ana uwezekano mkubwa wa kuajiriwa.

Kumbe bado kuna ubaguzi mkubwa wa kidini, kikabila na kikanda katika ajira nchini Tanzania? Ni lini hasa huu ubaguzi utakoma?
 
Kumbuka hii ni taasisi ya kidini pengine wameweka sharti hilo kuweza kukidhi mahitajio ya kisabato.
 
Kumbuka hii ni taasisi ya kidini pengine wameweka sharti hilo kuweza kukidhi mahitajio ya kisabato.

sasa usabato unahusikaje kwenye kazi ya kitaaluma (kitaalamu)?
 
nenda kwa bharessa ukaone ubaguzi zaidi

nakubali kwamba hata kwa bakhresa kuna ubaguzi wa hali ya juu lakini sijawahi kusikia ukitangazwa hadharani kama huu wa wasabato.
 
Kumbuka hii ni taasisi ya kidini pengine wameweka sharti hilo kuweza kukidhi mahitajio ya kisabato.
kama ni usabato na kwa maslahi ya usabato ukanda wa ziwa unaingiaje hapa si wangesema awe msabato mtanzania tu. Ukanda wa ziwa ukusini au kaskazini mwa tz una uhusu nini huu ni ubaguzi na si ucha mungu mungu gani huyo anaependa mtu kubaguliwa mpaka anapotoka? Hizi dini nyingine ni majanga tuu
 
Kumbuka hii ni taasisi ya kidini pengine wameweka sharti hilo kuweza kukidhi mahitajio ya kisabato.

Kama ni kazi ya kidini kwa nini watangaze hadharani? Si wangetangaza makanisani mwao na wangepata waombaji humo humo makanisani??? Huu ni ubaguzi na ushindwe kabisa
 
Kama ni kazi ya kidini kwa nini watangaze hadharani? Si wangetangaza makanisani mwao na wangepata waombaji humo humo makanisani??? Huu ni ubaguzi na ushindwe kabisa

umelazimishwa kusikiliza radio Yao?
 
sasa usabato unahusikaje kwenye kazi ya kitaaluma (kitaalamu)?

Wasabato wana itikadi tofauti na madhehebumengine ya kikristo ndio maana wanataka msabato mwenzao ambae si mwizi kama wewe. isitoshe wanataka wa kanda ya ziwa atakae declare utajiri au umaskini wake ili wawe wanammonitor kirahisi. sijawahi kuona mfanyakazi msabato bale bakwata
 
Wasabato ni wabaguzi hadi ktk shule zao wanangalia kwanza watoto wa wasabato hata kama ni manunda wapate kwanza nafasi wengine baadae!

wangekuwa na shule nyingi na bora kama waroma si wengine ambao madhehebu yetu hayana shule tungekoma?:sad:
 
Patrick Kahemele, ambaye ni Mkristo na mwenyeji wa Bukoba alikuwa Meneja wa Azam FC na sasa ni Mkurugenzi wa matangazo wa Azam TV (kama sijakosea).
Kama huna la kufanya kakojoe ukalale...

Hata hivyo Bakheresa ina ubaguzi wa hali ya juu!
 
Leo nilikuwa nasikiliza redio ya Morning Star nikasikia tangazo hili la nafasi ya kazi ambalo limenishangaza sana:

1. Mwombaji awe ni muumini wa kanisa la Waadiventista wa Sabato (SDA) na aweze kuthibitisha hilo kwa maandishi.

2. Mwombaji awe ni mwenyeji wa Kanda ya Ziwa na hilo lithibitike kwenye cheti chake cha kuzaliwa.

3. Mwombaji awe na shahada ya kwanza ya uboharia (Material Management). Mwenye shahada ya pili ana uwezekano mkubwa wa kuajiriwa.

Kumbe bado kuna ubaguzi mkubwa wa kidini, kikabila na kikanda katika ajira nchini Tanzania? Ni lini hasa huu ubaguzi utakoma?


Mkuu unadhani umaskini tulionao ni wa bahati mbaya?
 
Back
Top Bottom