U.S. tells Rwanda to immediately end support for M23 rebels

U.S. tells Rwanda to immediately end support for M23 rebels

Bashar ameua zaidi ya wasyria laki moja,unasema kwanini US wanawapa siraha wapinzani wa Bashar???wewe ulitakaje???aendelee kuua???

Kule kuna vita kati ya magaidi na jeshi la serikali, popote palipo na vita mauaji lazima kutokea! upo hapo dogo? Magaidi wameshika silaha wanataka kupindua nchi alafu wewe ulitaka Serikali ifanyaje? icheze marede?

juhudi nyingi zimefanyika kuleta suluhu lakini Bashar ni jeuri hataki.
Una uhakika na unachozungumza? Marekani na Russia wamefungua uwanja wa majadiliano kati ya serikali ya Syria na wapinzani (waasi), hao waasi unaowashabikia wamekataa ku join madhungumzo uti mpaka wapatiwe silaha za kuweza kupambana na jeshi la serikali ya syria, unafahamu hilo au unaongea tu?

DRC nako unasema tusiunge mkono vikosi kupelekwa huko kwani tatizo la wakongo litamalizwa na wakongo UNAUHAKIKA NA UNACHOSEMA???HOW??nadhani sanasana unanitafutia ban.

wewe unafikiri matatizo ya congo sisi watanzania tutaweza kuyatatua? au unafikiri matatizo yanatatuliwa kwa silaha? hata raisi wako Kikwete kawambia rwanda,burundi,uganda na congo wakae mezani na waasi wayamalize kwa mapatano! au na hili haulifahamu?
 
Maskini Paul Kagame, namfananisha na NOVEL YA CHINUA ACHEBE THINGS FALL APART, mwisho wa utawala wamabavu ni sasa, anaua wapinzania wake wote popote walipo duniani, hata yule prof wetu wa UDSM aliuawa na mafia wa Kagame, hilo la kusaidia waasi wa M23 ni geresha OBAMA anatafuta njia za kuisaidia Tanzania iwapo tutapigana na Rwanda, kumbe JK hakukurupuka kumwambia aongee na waasi wa kihutu alitumwa tu kuongea na wakubwa kwa akili yake ndogo akakurupuka kumtukana JK, sasa atajuta. JWTZ wameanza mafunzo ya DRONS.

Siungi mkono anachofanya kagame na pia siungi mkono wanachofanya USA dhidi ya wananchi wa syria. M23 na waasi wa Syria vyote ni vikundi vya ugaidi
 
Koba tumekukosa kwenye hoja hii.... Njoo unogeshe au maji ya shingo?? Unawaogopa wa marekani??
Mkuu Ndugu KOBA anaishi Merikani kwa hiyo usitegemee anaweza kuchangia chochote kuhusu Merikani, naona kwa hilo tunaweza kumuelewa na kumsamehe hana jinsi.
 
Mkuu haujasikia kuna large reserve ya mafuta imegundulika muambao wa Ziwa Tanganyika kwa upande wa Congo DRC? Whenever there is OIL U.S.A is there, instability ya East CONGO eneo ambalo ndiyo mafuta hayo yamegundulika itamkwaza mmarekani kujivunia mafuta yake kwa urahisi. You just connect the dots, Tanzania ndiyo itakuwa main port ya mafuta ya CONGO yatakayokuwa exported kwenda U.S.A .

Nilikua sifahamu mkuu, anachofanya Rwanda ndio wanachofanyaga USA dhidi ya maifa mengine, USA anapinga waasi wa M23 wasisaidiwe then anaunga mkono waasi wa syria wapewe silaha.
 
Kagame anajiandaa kubadilisha katiba 2014 ili kuondoa term limits.

Asingefanya hivyo ningemshangaa na kumwona kipofu maana usalama/kuishi kwake kwa raha ni kuwa president.
 
Sasa haya uliyoyaandika, ndio ushauri ambao JK aliwapa Rwanda, nao wakamjia juu! Sasa sielewi unaunga mkono au unapinga! Kimsingi, JK yuko sahihi kabisa

mkuu kama umesoma text yangu yote naeleweka vizuri tu, siungi mkono vita ya aina yeyote na wanaofadhili ivyo vita.
 
Mgogoro wa congo ni congolese wenyewe,waache kulaumu Rwanda maana theres no Rwandese single soldier in Congolese land,the only foreign military ndani ya congo ni monusco and genocidal FDLR ambao wanawasaidia congo kupigana na wapinzani wao M23,maimai etc story za majeshi ya Rwanda ndani ya congo kusaidia waasi or kuiba mineral is pure allegations and ridiculous at best,chinese and western companies wako busy kujichotea Congolese wealth huku Congolese wakiwa busy kuchinjana then Rwanda is the problem...kweli wajinga ndio waliwao.
 
USA anaunga mkono waasi wa Syria na anawapatia silaha ili waipindue Serikali ya Syria, mbona hao Human Right Watch sijawasikia waipinge USA silaha zake zinamwaga damu za wasyria, nyani haoni kundule?
Wana JF sio kama wanaunga mkono M23/Rwanda, sipendi unafiki wa USA hasa maslahi yake yanapoguswa.
Vile vile sisi wa-Tz hatutakiwi kuunga mkono vikosi kwenda Congo, mzozo wa Congo hauwez kutatuliwa kwa bunduki hata Yesu atakapo rudi, mzozo wa Congo utatatiliwa na wacongo wenyewe kukaa mezani na kujadili namna wote watakavyonufaika na raslimali za ile nchi, tusiwe mashabiki maandazi.
Masawe unajua waCongo (DRC)? Aau unasema tu kwa kutumia hasira za maandazi
  • huyo Paul kagame ni Mkongo?
  • leo Watutsi ni waCongo?
  • hao M23 ni WaCongo?
Hizo rasilimali wanazochuma kuendeshea Serikali ya rwanda na uganda ndio za kukaa pamoja mezani kuzungumza?
Huyu Kagame mwache achapwe sasa maana kaona nwote wa Maziwa Mkuu ni wapuuzi
 
Masawe unajua waCongo (DRC)? Aau unasema tu kwa kutumia hasira za maandazi
  • huyo Paul kagame ni Mkongo?
  • leo Watutsi ni waCongo?
  • hao M23 ni WaCongo?
Hizo rasilimali wanazochuma kuendeshea Serikali ya rwanda na uganda ndio za kukaa pamoja mezani kuzungumza?
Huyu Kagame mwache achapwe sasa maana kaona nwote wa Maziwa Mkuu ni wapuuzi
M23 are legit Congolese wengi wao known as banyamulenge na wapo pale for hundrels of yrs na wameishi bila matatizo mpaka genocidals FDLR walipoingia Congo na kutaka kuwamaliza kwa sababu wana asili ya kitutsi,na acha fantasy zako za kufikiria Rwanda inaendeshwa kwa raslimali za Congo,wapi walikamatwa Rwanda wanaiba madini ya Congo ni story za vijiweni tuu
 
Leo sijasikia matangazao kutoka Goma,labda John Kerry amepiga marufuku mpaka atakapoamua jambo gani litangazwe. Nilisika tu katika gazeti asubuhi kwamba M23 wamemwachia huru yule mtanzania waliyemkamata kwa heshima ya Nyerere,halafu imekuwa news blackout.
 
Kagame anajichimbia shimo ambalo lazima ataliingia. Abadilike kabla wakati haujamtupa mkono.
 
Kinachotakiwa ni kusimamia haki. Kagame na M7 wamekuwa wakitumia genocide kama sababu ya kuonewa huruma, wakati wanajinufaisha binafsi na rasilimali za Congo. Leo hii kama madini yanayouzwa kutoka Congo yakisitishwa uchumi wa dunia utapata mtikisiko ambao haujawahi kutokea. (Hapa ni katika kuweza kuweka memory kwenye technologia tunayojivunia).

Vile vile ikumbukwe geological features za Congo zinashabihiana na zile za nchi za Afrika mashariki na kati, Marekani hawawezi kupuuza swala hili katu. Kagame aombe ushauri sasa kutoka kwa M7 yeye anafikiri nchi jirani wamelala fofofo kumbe wako macho. Wasubiri sasa hilo kombora kutoka UN.

Tanzania itaendelea kuchukua leading role katika Afrika kutokana na mchango mkubwa alioufanya Kambarage RIP. Matunda yake yanaonekana wakati yeye hatunaye tena.
 
M23 are legit Congolese wengi wao known as banyamulenge na wapo pale for hundrels of yrs na wameishi bila matatizo mpaka genocidals FDLR walipoingia Congo na kutaka kuwamaliza kwa sababu wana asili ya kitutsi,na acha fantasy zako za kufikiria Rwanda inaendeshwa kwa raslimali za Congo,wapi walikamatwa Rwanda wanaiba madini ya Congo ni story za vijiweni tuu

Utasema sana ni story za vijiweni lkn ukweli nyie watutsi (tena nyie wa rwanda na uganda)mnaiba mali ya drc. Ulisema eti M23 ni wakongo..guy you are dreaming. Hao ni watutsi na walishiriki kuvamia rwanda kutokea uganda mkijiita rpf. Usidhani tabia zenu na yote mnayofanya huko DRC hayajulikani. Ngoja siku tuanze kuwasaka huku nchini kwetu tuwarudishe kwenu kwa sababu mshaanza vurugu huko karagwe na ngara. Na hivi kagame ameanza ujinga wa kumtukana Rais wetu Mh Kikwete, ile huruma tuliyo waonyesha miaka yote sasa hamna! Nyie sio watu kabisaaa..mrudi kwenu mkauane wenyewe maana ndo raha yenu watutsi kuona damu za watu zikimwagika..
 
Thats the end of the Game to P.Kagame...yani JWTZ inaita last Card...tena mavi ya mbuzi ya tripple7,wakati Kagame bado ana Joker na bwana na bibi....Kumbe kelele zote zile n sbb tumetekenya masabuli ya Kigali...Dah kweli Ziara ya Obama inajibu

Hahahahaha hii ya leo ndo naenda kulalia
 
Utasema sana ni story za vijiweni lkn ukweli nyie watutsi (tena nyie wa rwanda na uganda)mnaiba mali ya drc. Ulisema eti M23 ni wakongo..guy you are dreaming. Hao ni watutsi na walishiriki kuvamia rwanda kutokea uganda mkijiita rpf. Usidhani tabia zenu na yote mnayofanya huko DRC hayajulikani. Ngoja siku tuanze kuwasaka huku nchini kwetu tuwarudishe kwenu kwa sababu mshaanza vurugu huko karagwe na ngara. Na hivi kagame ameanza ujinga wa kumtukana Rais wetu Mh Kikwete, ile huruma tuliyo waonyesha miaka yote sasa hamna! Nyie sio watu kabisaaa..mrudi kwenu mkauane wenyewe maana ndo raha yenu watutsi kuona damu za watu zikimwagika..
Not worth debating na mwendawazimu kama wewe,waulize wenzako waliokuwa na mawazo kama yako labda utajifunza kitu.
 
Being patient and calm with maximum determination philosophy responses to any matter is only required than insult eruption that been shown out by our neighbor....how can we rate this?....:disapointed🙁over maximum confidence...)
What's behind...???
 
Haya sasa. Rais wa dunia keshasema. Tusubiri utekelezaji. Kama kuna rafiki mkubwa Rwanda ilitakiwa ibaki naye ni Tanzania. Ukiichokoza Tanzania kila nchi duniani itakushangaa!. Wanaojua kama Kenya na Uganda siku zote huwa hawajaribu na tunakaa nao vizuri. Huyu inaonekana alikuwa amelala fofofo!

si unajua tena ushamba mkuu, kutokea ukimbizini mpaka kuwa raisi wa nchi sawa na kikwete siyo mchezo, pia kajipumbaza na kudeki barabara na kufikiri ni bonge la dili na kuanza kuwadharau hata majirani wenye nia njema na taifa lake bila kusahau uhalifu mkubwa dhidi ya raia wasiokuwa na hatia huko rwanda na DRC.
 
Jasusi JokaKuu Kagame amejiweka katika wakati mgumu. Kama UN sec council imemtupia macho ajue siku zinakaribia.
Mwisho wa Kagame ni mbaya sana. Sasa hivi atakuwa bize na usalama wake kuliko kuivuruga EAC.
This is just the beginning of, kila uovu wa DRC atahusishwa nao. Kagame ipo siku ataungana na Charles Taylor the Hague.
 
Godlisten i support u.....nashangaa baada ya kutoa pendekezo mhe Rais wa TZ kuwa waasi wa maziwa makuu wasikilizwe kwenye meza moja na govts zao....kesho yake Membe akatuma kikosi DRC sijaelewa mhe JK anahubiri Maji huku akinywa wine?tuache unafki kama kweli bwana mkubwa ulimaanisha kwanini utume jeshi Congo?
 
Back
Top Bottom