TV flat Samsung na ulaji wa umeme

TV flat Samsung na ulaji wa umeme

samuel faraj

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
1,326
Reaction score
1,266
Wakuu Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu Nyumbani nimenunua flat TV ya 50" tangu ninunue matumizi ya umeme yameongezeka maradufu yaani unit 5-6 kila siku zimeongezeka kwenye matumizi. Tatizo nini Wakuu wenye uelewa msaada tafadhali.

NB:wenye Povu hapa sio Mahala pake
 
Tatizo ni ww,unatumia mda mwingi kuangalia hiyo tv maana ni mpya.Pia Unaonekana unaishi ktk nyumba za kupanga so ushindani wa matumizi ya umeme ni wa Kasi zaidi
Kumjibu mjinga Mara zote kunahitaji busara sana Ngoja Nitumie busara
 
Mkuu model yake ni PS50A456P2D
Dah kama nilivyofikiria ni kitu cha plasma, hazitengenezwi tena hizo mkuu na wamekukamata. Ukiiwasha matumizi ya kawaida inakula 330 watts hivyo haifiki hata masaa 3 unit moja imekata.

Ushauri wangu irudishe ikiwezekana ongeza hela tafuta tv ya led,

Pia hizo tv ni bei rahisi sana, zinakuwa hadi laki 6 hadi 8 kwa hio 50 inch, na kioo chake ni 720p ambacho sio kizuri kwa ukubwa huo,
 
Ulitakiwa uangalie itakula umeme kiasi gani kwa saa kabla ya kununua!
 
Dah kama nilivyofikiria ni kitu cha plasma, hazitengenezwi tena hizo mkuu na wamekukamata. Ukiiwasha matumizi ya kawaida inakula 330 watts hivyo haifiki hata masaa 3 unit moja imekata.

Ushauri wangu irudishe ikiwezekana ongeza hela tafuta tv ya led,

Pia hizo tv ni bei rahisi sana, zinakuwa hadi laki 6 hadi 8 kwa hio 50 inch, na kioo chake ni 720p ambacho sio kizuri kwa ukubwa huo,
Ahsanteni mkuu be blessed!
 
mkuu mkwawa miye pia nina mdubwasha THOMSON (TV) HAUNA CHOGO wenyewe pekee ukiuwasha kwa siku ynakula hadi unit 6 kwa muda wa masaa 2tu
 
Wakuu kwa flat mi naona Rising wako vzur umeme unatumia kdogo sana, display iko vizur picha iko quality vizur mi naona
 
Wakuu kwa flat mi naona Rising wako vzur umeme unatumia kdogo sana, display iko vizur picha iko quality vizur mi naona
umeme hauhusiani na brand bali technology iliotumika hasa hasa aina ya kioo, unafkiri TV ya rising ya plasma itatumia umeme mdogo kushinda LED ya samsung? vitu vyengine kama wifi, speaker kubwa, smart features mbali mbali, 3D, etc vinaweza sababisha tv ile zaidi umeme
 
umeme hauhusiani na brand bali technology iliotumika hasa hasa aina ya kioo, unafkiri TV ya rising ya plasma itatumia umeme mdogo kushinda LED ya samsung? vitu vyengine kama wifi, speaker kubwa, smart features mbali mbali, 3D, etc vinaweza sababisha tv ile zaidi umeme
so unamaanisha watu kwa ulimwengu wa sasa ni vizuri watumie led na si lcd?
 
Back
Top Bottom