Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Naomba leo niwarudishe nyuma kidogo tulikotoka hadi leo nimepata Tuzo ya Mwandishi Bora wa Vitabu Afrika.
Nawakumbusha tu kwamba December 2017, kitabu cha Ujasusi kikiwa na mwaka mmoja hivi tangu kichapishwe, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dkt. Athumani S. Ponera (Akiwa ni Mhadhiri wa Taaluma za Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma) alinunua kitabu na kukisoma, baada ya Kusoma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi alitoa mapendekezo/maoni yake kwamba Mwandishi wa Kitabu cha Ujasusi Bwana Yericko Nyerere anastahili kutunukiwa shahada mbili za "heshima" za udaktari.
Daktari Ponera katika maoni ama mapendekezo yake huru yanayosikika katika video hii, alisema,
"Yericko Nyerere kupitia kitabu hiki unastahili kupata PhD mbili, anafafanua zaidi kwakusema, PhD ni uzamivu wa mtu ktk Eneo/uga fulani. Mtu akisoma andiko lako anapata maeneo mawili au matatu yaliyofanyiwa kazi kwa kina. Kwa maoni yangu, Nyuga hizo ni pamoja na:
"1. Usalama, 2. Histo-tamaduni (maelezo ya kihistoria, matukio na utamaduni kuhusu jamii/maeneo mbalimbali), 3. (utamaduni wa)Siasa za maeneo mbalimbali. Any of the above fields zimeelezwa Kwa kina, na zinaweza kumegwa na kujaziwa kidogo kisha mtu anapata PhD....hongera sana Yericko Nyerere".
Mwisho wa kunukuu.
Baada ya maoni hayo, kwasababu ya siasa chafu za nchi yetu, alishughulikiwa kisawasawa, alinyanyaswa sana akitakiwa kujieleza kwanini ametoa maoni hayo kwa mtu ambae ni mpinzani nchini, baadae aliondolewa pale chuoni akapelekwa chuo cha Mwalimu Nyerere, kisha akapelekwa Zanzibar ambako aliendelea na utumishi wake kwa uaminifu mkubwa.
Miaka 6 baadae yaani 2023, Yericko Nyerere ametukiwa tuzo ya Mwandishi Bora wa Vitabu Barani Afrika. Sijui tunajifunza nini? Pengine wale maprofesa pale UDOM na wale viongozi wa kiserikali waliomshughulikia Dr. Ponera wanaweza kuwa na maoni tofauti leo wakisikia kuwa yule mtu waliyemchukia ilipopendekezwa apewe tuzo ya heshima ya PhD za Dar, Sasa amepewa tuzo ya Afrika ya uandishi Bora wa Vitabu.
Nakufahamisha incase umesahau au ulikuwa hujui, Mshindi wa Tuzo ya Mwandishi Bora wa Vitabu Barani Afrika ni YERICKO YOHANESY NYERERE kutoka TANZANIA.
Sifa na heshima ni za Watanzania!
Idumu Mizimu!
Na Yericko Nyerere
Nawakumbusha tu kwamba December 2017, kitabu cha Ujasusi kikiwa na mwaka mmoja hivi tangu kichapishwe, Mhadhiri wa Chuo Kikuu Dkt. Athumani S. Ponera (Akiwa ni Mhadhiri wa Taaluma za Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dodoma) alinunua kitabu na kukisoma, baada ya Kusoma kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi alitoa mapendekezo/maoni yake kwamba Mwandishi wa Kitabu cha Ujasusi Bwana Yericko Nyerere anastahili kutunukiwa shahada mbili za "heshima" za udaktari.
Daktari Ponera katika maoni ama mapendekezo yake huru yanayosikika katika video hii, alisema,
"Yericko Nyerere kupitia kitabu hiki unastahili kupata PhD mbili, anafafanua zaidi kwakusema, PhD ni uzamivu wa mtu ktk Eneo/uga fulani. Mtu akisoma andiko lako anapata maeneo mawili au matatu yaliyofanyiwa kazi kwa kina. Kwa maoni yangu, Nyuga hizo ni pamoja na:
"1. Usalama, 2. Histo-tamaduni (maelezo ya kihistoria, matukio na utamaduni kuhusu jamii/maeneo mbalimbali), 3. (utamaduni wa)Siasa za maeneo mbalimbali. Any of the above fields zimeelezwa Kwa kina, na zinaweza kumegwa na kujaziwa kidogo kisha mtu anapata PhD....hongera sana Yericko Nyerere".
Mwisho wa kunukuu.
Baada ya maoni hayo, kwasababu ya siasa chafu za nchi yetu, alishughulikiwa kisawasawa, alinyanyaswa sana akitakiwa kujieleza kwanini ametoa maoni hayo kwa mtu ambae ni mpinzani nchini, baadae aliondolewa pale chuoni akapelekwa chuo cha Mwalimu Nyerere, kisha akapelekwa Zanzibar ambako aliendelea na utumishi wake kwa uaminifu mkubwa.
Miaka 6 baadae yaani 2023, Yericko Nyerere ametukiwa tuzo ya Mwandishi Bora wa Vitabu Barani Afrika. Sijui tunajifunza nini? Pengine wale maprofesa pale UDOM na wale viongozi wa kiserikali waliomshughulikia Dr. Ponera wanaweza kuwa na maoni tofauti leo wakisikia kuwa yule mtu waliyemchukia ilipopendekezwa apewe tuzo ya heshima ya PhD za Dar, Sasa amepewa tuzo ya Afrika ya uandishi Bora wa Vitabu.
Nakufahamisha incase umesahau au ulikuwa hujui, Mshindi wa Tuzo ya Mwandishi Bora wa Vitabu Barani Afrika ni YERICKO YOHANESY NYERERE kutoka TANZANIA.
Sifa na heshima ni za Watanzania!
Idumu Mizimu!
Na Yericko Nyerere