Kuna watu hawapendi ujirani wa amani kabisa. Na kundi hili la majirani wagomvi ni kubwa sana kuliko tudhaniavyo!
Binafsi ugomvi mkubwa na jirani yangu ilikuwa ni kwenye kununua Umeme. Huyo umeme ukiisha tu alikuwa hawashi taa na hapandishi mapazia anajifungia kimya!
Tulikalishwa vikao hadi vya mjumbe lakini wapi! Ikabidi nihamie nyumba nyingine! Huku nako nilikutana na mama mmoja jirani mchafu hatari, watoto wake walikuwa wanajisaidia kwenye corridor! Halafu hajali wala nini, ukiweka kanyagio la kufutia miguu ukitoka baadae unarudi unakuta wamelichukua wao kufutia miguu!
Nikadhani mtu aliyejenga hana kero ya ugomvi na majirani kumbe huku ndiko kuna balaa zaidi! Huku nako kuna watata vilevile, usipoangalia unaweza pata presha. Wapo majirani mabingwa wa kusogeza mipaka ya viwanja! Huu ugomvi ni mwingi sana umeharibu mahusiano ya majirani wengi sana!
Wapo pia majirani wanaojenga hadi kiwanja wanamaliza halafu paa la nyumba linamwaga maji kwa jirani ilimradi tu wawakere!
Yote tisa, wapo majirani wafugaji wenye mifugo inayoharibu mali za jirani yake na wala hawajali.
Nisiseme mengi. Leo Naomba tushirikishane, ni mgogoro gani hasa ulionao wewe na jirani yako hapo?
Binafsi ugomvi mkubwa na jirani yangu ilikuwa ni kwenye kununua Umeme. Huyo umeme ukiisha tu alikuwa hawashi taa na hapandishi mapazia anajifungia kimya!
Tulikalishwa vikao hadi vya mjumbe lakini wapi! Ikabidi nihamie nyumba nyingine! Huku nako nilikutana na mama mmoja jirani mchafu hatari, watoto wake walikuwa wanajisaidia kwenye corridor! Halafu hajali wala nini, ukiweka kanyagio la kufutia miguu ukitoka baadae unarudi unakuta wamelichukua wao kufutia miguu!
Nikadhani mtu aliyejenga hana kero ya ugomvi na majirani kumbe huku ndiko kuna balaa zaidi! Huku nako kuna watata vilevile, usipoangalia unaweza pata presha. Wapo majirani mabingwa wa kusogeza mipaka ya viwanja! Huu ugomvi ni mwingi sana umeharibu mahusiano ya majirani wengi sana!
Wapo pia majirani wanaojenga hadi kiwanja wanamaliza halafu paa la nyumba linamwaga maji kwa jirani ilimradi tu wawakere!
Yote tisa, wapo majirani wafugaji wenye mifugo inayoharibu mali za jirani yake na wala hawajali.
Nisiseme mengi. Leo Naomba tushirikishane, ni mgogoro gani hasa ulionao wewe na jirani yako hapo?