Tuwaenzi walimu wa somo la Mwandiko

Tuwaenzi walimu wa somo la Mwandiko

MOORIINGEE

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2013
Posts
381
Reaction score
190
Uwezo wa kubadilishana mawazo hapa JF ni kutokana na walimu waliyotufundisha somo la mwandiko tukiwa darasa la kwanza!

Kwa kuwaenzi nawaomba kila mmoja amtaje mwalimu wake kwa kumuenzi hata kama aliwahi kukuchapa.

Najua ulianza kuandika kwenye kibao kabla ya daftari.

Karibuni wana JF.
 
namkumbuka mwalimu ester jamani alikuwa mkali mpaka kero
 
mwalimu mwakabonga la kwanza A ubungo pr enzi hizo ubungo plaza pori pale, mihogo twala kwa ali kikono long tym.
 
Mwalimu Matee Shia P/r school- Moshi, Mungu amzidishie siku za kuishi wafaidi na wengine.
 
Mwl Ethel Msemwa ndio chanzo cha hata kuadika hivi.
 
Mwal. Ngitiri Olkokola Pr school Enzi za 1984 nyinyi wanajamvi hakuna aliyekuwa amezaliwa
 
Mwalimu Mtaki, Lionness Miburani primary school. Temeke. nasikia alikufa Mwenyezi Mungu amuweke mahala panapostahili. ameeen
 
Mwalimu Baruan mzingani primary school alikuwa anachapa na ruler mkononi hahaha
 
Mwalimu Muhima- Mwananyamala Primary School drs 1.
 
Mwl Mbaruku enzi hizo soni p/r school daa kitambo sana
 
Mama yangu mzazi! najivunia mpaka mwisho wa dunia, nilianza darasa la kwanza najua kusoma na kuandika..... chakushangaza zaidi yeye kaishia darasa la tatu.......
 
Mwalim Mzava, mazengo Pri. Dodomaaa.
Halaf alikuwa anatupenda huyo, acha tu
 
Mwl Jekera, Mtoni Pr.sch. Dar. std I 1984 Nilikuwa namzimia sana huyu ticha, hasa alivokuwa mpole na jinsi alivyokuwa anauza ufuta mzuri wa motomoto. we acha tu.
 
Bi mkubwa to alinfundsha la kwanza,la pili na la 3 ndo nilianza kuandikia peni!! Nashukuru nilikua na mwandko mzuri kimtndo na nilpokua nawaandikia barua kwa penseli kina esta na mwajuma wakawa wanaelewa!!!
 
Mwl Zungiza,Mugabe pr. Schl,Sinza Dar.kwa kweli namshukuru sana.Mapumziko darasa linafungwa,hutoki bila kununua vibagia na ubuyu wa urojo,kama huna hela unalazishwa kukopa.Tehe tehe.
 
Mwl.F.Chone!Alikua mpole na mnyenyekevu sana.Nampenda sana mwl huyu!Kanifundisha drs la kwanza 1993 na drs la pili 1994 mwl.H.Mwakisinini kanifunza vema!Mungu awape maisha mema na marefu!
 
Back
Top Bottom