TuntemekeSanga
JF-Expert Member
- Jan 15, 2015
- 1,346
- 863
- Thread starter
- #21
Kasumba ya kuwa "dawa ya moto ni moto" inapotosha. Wakati mwingine dawa ya moto ni baridi. Aliyetudanganya kuwa kila inapotokea wananchi wamechachama kwa sababu yeyote tutumie nguvu za ziada hususani mabamu ya machozi, risasi au kuwakamata.. huyu alitupotosha. Uzoefu labda kama lengo ni kujenga hofu ndani ya wananchi, lakini nafikiri tulipofikia, ni vema kutumia busara, psychology na hekima katika kutatua na kudhibiti hali kama hii kila inmapojitokeza. Na tukumbuke kuwa dawa ya moto si kila wakati iwe ni moto.
Mbona wananchi wamekiuka miiko na kuondokana na maadili ya mababu zetu? Polisi au vazi la polisi lilikuwa na heshima yake enzi zetu. Vazi la polisi lilibeba miiko kwa wananchi: palipo na ishara ya polisi ilimaanisha AMANI, UTULIVU, KIMBILIO, HAKUNA GHASIA... hata kama kungelikuwepo na vurugu, kitendo cha kuona mtu aliyevalia kama polisi,... wangelikimbilia huko... iweje siku hizi, wananchi wamechoka kuona "polisi"
Mkuu; Dunia ya leo si ya kale! We people have changed. We have grown a sortie of aggression.
Ushauri wako ni bora na umetoa mchango ulioutukuka ktk mada hii. Bravo!
Hope Polisi na wakubwa wao wangezingatia dhana hiyo. Si kila purukushani hutulizwa na Purukushani. Wanapaswa kuongeza weledi na maarifa zaid.
Pia, ni vyema nasie wananchi kujitahidi kuwa na simile. Kuna matukio au visa tunavifanya sometimes kwa namna ambayo haipendezi. Tujitahidi kuheshimu Mamlaka na kuwa watulivu ktk nyakati fulanifulani za matukio na visa. Sio kuwa aggressive na ushabiki usio na msingi.