'Tusivifokee' vyombo vya habari vya nje kuripoti taarifa kuhusu hali ya Rais Magufuli!

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,015
Usiku huu, Aloyce Nyanda (Mtozi) amekuwa na kipindi muhimu katika Star TV usiku huu. Agenda Kuu ilikuwa ni Maadili ya Uandishi wa Habari kufuatia Vyombo vya Habari vya mataifa mengine kuripoti taarifa kuhusu Rais Magufuli pasipo kupata uthibitisho kutoka kwa wahusika yaani Serikali ya Tanzania.

Kwanza kabisa, ninataka kutangaza maslahi kabla ya kujadili hoja hii hapa. Nimesomea 'Sociology of Mass Media' na nilitafiti kidogo kuhusu namna Vyombo vya Habari vya Nchi zinazozungumza Kiingereza vilivyoripoti taarifa za Vita vya Ghuba vilivyomwangusha Rais Saddam Hussain wa Iraq. Niliangazia zaidi Magazeti katika nchi za Afrika Kusini, Kenya, Uganda, Ghana, Malawi, Zambia, Nigeria, Tanzania, Zimbabwe, Botswana, New Zealand, Australia na Uingereza yenyewe. Niliangazia pia mashirika makubwa pia ya Reuters, CNN, BBC nk.

Baadhi ya niliyogundua ni kuwa kulikuwa na taarifa ambayo ilikuwa inaripotiwa na vyombo vyote kwa mtindo uleule hii ikiwa na maana kuwa kulikuwa na chanzo kimoja Kikuu cha Habari! Hii ina maana kuwa taarifa nyingi za Kimataifa ambazo hata Vyombo vyetu vya Habari hutangaza 'humegewa' na Mashirika Makubwa ya Habari Duniani!

Ninachoweza kusema ni kuwa Mashirika Makubwa ya Habari Duniani yanakuwa na vyanzo vya Habari ndani ya nchi kadhaa ambavyo vinaaminika hata kuliko nchi husika ambamo mashirika hayo huangazia. Kuna wakati ambapo nchi husika inaweza isijue taarifa kamili hadi itakapoambiwa na mashirika hayo. Hata hivyo, kama kuna urafiki na mahusiano mazuri kati ya mashirika hayo na nchi husika, Vyombo hivyo hutafuta uthibitisho kutoka mamlaka hata kama vinakuwa na taarifa kamili. Pale ambapo taarifa au habari zinahusiana na mambo ya kijasusi au katika nchi isiyo rafiki (closed countries) katika masuala ya Habari nk basi media au mashirika ya nje yanaweza kutangaza Habari pasipo kupata uthibitisho kutoka katika mamlaka husika. Nawarejeza wasomaji wangu jinsi ambavyo BBC inavyotoa taarifa zinazohusu nchi za Urusi, Korea Kaskazini nk.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini Deodatus Balile amejitokeza na kusema kuwa wao walijatahidi kutaka kupata taarifa kutoka Serikalini lakini hawakufanikiwa. Kama watu walioko nchini wanashindwa kupata taarifa kutoka Serikalini inakuwaje kwa Vyombo vya nje? Tunachotakiwa kujua hapa ni kuwa kama baadhi ya Vyombo vya Habari vya nje vinaichukulia Tanzania kama 'closed country' kwa masuala ya Habari, basi vinaweza kutoa pasipo kusubiri uthibitisho kutoka katika mamlaka za Tanzania.

Ni vizuri tukatofautisha kati ya media ya Tanzania ambayo kwa kiasi kikubwa ni 'pro government' na media za nje ambazo ni huru! Media za nje nyingi huuza habari kwa hiyo utoaji wake wa Habari utakuwa tofauti sana na media zetu ambazo wasikilizaji hawana mamlaka ya kuamua nini wasikilize.

Mtazamo wangu ni kuwa Tanzania siyo kisiwa katika ulimwengu huu. Sisi tusipokuwa tayari kutoa taarifa kwa wanahabari tujue kuwa media za nje zitachokonoa tu kwa kuwa na wao wana maslahi ya kiuchumi, kiusalama na nchi yetu.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
 
Uhuru wa kuku wa kienyeji ni tofauti kabisa na kuku wa kufugwa bandani.

Wa kienyeji hula atakacho , huenda atakako. Huyu wa kufugwa bandani yuko chini ya uangalizi 24/7 na ana limitations kwenye kila kitu.

Ni ajabu ya mwaka kama kuku wa bandani hatamuonea wivu kuku wa kienyeji.. Waandishi wa bongo wamekuwa kama yale makuku ya kufugwa.

Tunayaita MAZEZETA.
 
Acha ujinga, kama hivyo vyombo vina ukweli , mbona viliripoti kuwa Rais wa Korea Kaskazini amefanyiwa upasuaji na kupoteza maisha je huo ukweli waliutoa wapi?

Hata wao wanategemea waongo kama ndugu yenu Lissu
 
Kwa hiyo unaamini taarifa ya vyombo vya nje? Hivi si hao akina BBC, CNN et al waliripoti Kiduku wa NK amedanja, taarifa ambayo walipika au kukurupuka bila uthibitisho. Ninachofahamu hao mabeberu kama uko kinyume na maslahi yao lazima wakuchafue kwa njia yoyote ile, ikiwemo taarifa kama hizo za uzushi ili kuleta taharuki katika jamii.
 
Uhuru wa kuku wa kienyeji ni tofauti kabisa na kuku wa kufugwa bandani.

Wa kienyeji hula atakacho , huenda atakako... Huyu wa kufugwa bandani yuko chini ya uangalizi 24/7 na ana limitations kwenye kila kitu.

Ni ajabu ya mwaka kama kuku wa bandani hatamuonea wivu kuku wa kienyeji.. Waandishi wa bongo wamekuwa kama yale makuku ya kufugwa.

Tunayaita MAZEZETA
Ndio Maana Wistonchurchil alipowaita waengera akasema je waingereza mutapenda muwe na matumbo makubwa na huku mumetawaliwa au mutapenda muwe na matumbo madogo lkn muko huru .Naam waingereza wakasema tunataka tuwe HURU basi akawambiya lazima tupigane tumuondoshe Hitler.Hapa nyumbani habari ni criminal case itabidi ufuate upepo maana weye bendera tu.
 
Kwa hiyo unaamini taarifa ya vyombo vya nje? Hivi si hao akina BBC, CNN et al waliripoti Kiduku wa NK amedanja, taarifa ambayo walipika au kukurupuka bila uthibitisho. Ninachofahamu hao mabeberu kama uko kinyume na maslahi yao lazima wakuchafue kwa njia yoyote ile, ikiwemo taarifa kama hizo za uzushi ili kuleta taharuki katika jamii.
Mkuu usipotoshe uma

Hakuna source yoyote kutoka BBC, neither CNN iliyowahi kusema Kim amefariki.

Walicho report wao ni kuhusu Kim kuwa mgonjwa, vinginevyo thibitisha kwa kuweka link hapa
 
Mkuu usipotoshe uma

Hakuna source yoyote kutoka BBC, neither CNN iliyowahi kusema Kim amefariki.

Walicho report wao ni kuhusu Kim kuwa mgonjwa, vinginevyo thibitisha kwa kuweka link hapa
Fauatilia walichoripoti, usiwe mvivu wa kufanya ufuatiliaji.
 

Attachments

  • Screenshot_20210316-082037_Samsung Internet.jpg
    Screenshot_20210316-082037_Samsung Internet.jpg
    107.4 KB · Views: 1
Fauatilia walichoripoti, usiwe mvivu wa kufanya ufuatiliaji.
Hili halijadhibitisha kauli yako kwamba 'BBC na CNN wali report Kim amefariki'

Weka source/s hapa zinazoonesha bila bila kona yoyote kwamba BBC na CNN wali report Kim amefariki
 
Askofu Mwamakula ANA ULIMI WA HATARI KAMA NYOKA NA MDOMONI MWAKE MNA MANENO YA SUMU YA FIRA (Zaburi 140:3).

Mungu mwenyewe ataenda kukifunga kinywa hicho maana maana Mungu hadhihakiwi. Yeye na hivyo vyombo anavyovisifia kwa kutoa habari zisizo sahihi wajitathmini:-
  • Yupo Nairobi mahututi...(ikakanushwa)
  • Ulinzi umeimarishwa.. (Ikakanushwa)
  • Hali mbaya amehamishiwa India
  • Amefia Nairobi Hosp
  • Amefia India
  • Anaumwa ameparalize... Nk
Sasa hivi kama kusoma hawezi amevaa miwani ya mbao, hata picha haoni kwa huu mtiririko wa maneno yasio na chembe ya ukweli au ushahidi.

Zaidi ya kauli ya Makamu wa Rais na Waziri Mkuu anataka nini tena.

Nimkumbushe habari ya kifo cha tajiri na masikini aitwaye Lazaro. Mungu alimwambia kuhusu kuamini wasipowaamini hao hata nikituma Malaika hawatamuamini. Sifa ya mtumishi wa Mungu ni uvumilivu, si asubiri aone kama hatajitokeza?

Ask Mwamakula jikite kwenye kutafuta kondoo waliopotea, huo ndio wito wako. Siasa za maji taka ZINAMDHALILISHA KRISTO!!
 
Uhuru wa kuku wa kienyeji ni tofauti kabisa na kuku wa kufugwa bandani.

Wa kienyeji hula atakacho , huenda atakako. Huyu wa kufugwa bandani yuko chini ya uangalizi 24/7 na ana limitations kwenye kila kitu.

Ni ajabu ya mwaka kama kuku wa bandani hatamuonea wivu kuku wa kienyeji.. Waandishi wa bongo wamekuwa kama yale makuku ya kufugwa.

Tunayaita MAZEZETA
Mzee Mshana ni tasnia gani au kundi gani,au ni nani ambaye si mhanga wa "dicteta uchwara" ??
 
Ha
Mkuu usipotoshe uma

Hakuna source yoyote kutoka BBC, neither CNN iliyowahi kusema Kim amefariki.

Walicho report wao ni kuhusu Kim kuwa mgonjwa, vinginevyo thibitisha kwa kuweka link hapa
Pengine hujui ila walilipoti ingawa hawakuwa na uhakika, na ndo maana trumpu aliwaambia hategemei kama kim amefariki na akasema hawezi kuiamini CCN
 
Uhuru wa kuku wa kienyeji ni tofauti kabisa na kuku wa kufugwa bandani.

Wa kienyeji hula atakacho , huenda atakako. Huyu wa kufugwa bandani yuko chini ya uangalizi 24/7 na ana limitations kwenye kila kitu.

Ni ajabu ya mwaka kama kuku wa bandani hatamuonea wivu kuku wa kienyeji.. Waandishi wa bongo wamekuwa kama yale makuku ya kufugwa.

Tunayaita MAZEZETA.
Mkuu hawa waandishi wetu wako makini ila wanafanywa kuwa mazezeta.hasa na mamlaka husika.
Si
 
Mzee Mshana ni tasnia gani au kundi gani,au ni nani ambaye si mhanga wa "dicteta uchwara" ??
Mimi siyo muhanga. Hyu dikteta yuko india kimatibabu
Baada ya Nairobi kushindwa kumtibu waka mrefaaa india.
Katiba yetu inasema rais asipofanya kazi week moja nzima . Ajiuzulu kiti achukue makamu wake
 
Back
Top Bottom