Tusikufuru CAG ni binadamu siyo Mungu!

Tusikufuru CAG ni binadamu siyo Mungu!

Mkuu matusi ya nn ? Haikupaswa utoe lugha kali. Kiranga kajenga hoja na kuuliza maswali, ulitakiwa ujibu hoja zake na kumtwanga maswali. Ndo mijadala ilivo. Uzuri wa Jf no one sided thread/topic
Nimemuuliza swali rahisi sana kujibu..

Hiyo kanuni ya kusema kwamba mtu (CAG) asifanywe kama "Mungu", kwani anakosea tu, anaiweka kwa watu wote, akiwamo na Magufuli?

Jibu ni ndiyo au hapana.

Mpaka sasa kapata kigugumizi hajajibu.

Kwa nini?

Kwa sababu, nia yake si kusema mtu asifanywe kama Mungu, angekuwa na nia hiyo angekubali kwamba hata Magufuli naye kwa kuwa si Mungu, hili linamhusu.

Nia yake ni kuleta siasa za majitaka dhidi ya CAG.

Tumemstukia ujanja mwingi mbele kiza.
 
Kinachopelekea CAG kutendewa haya tofauti na kawaida sote tunakijua na hatuhitaji kulitaja jina lake baba aliye juu buuure kisa kutetea hila chafu. Chuma dhambi na wakwenu... mmezoea hata kutesa na kupoteza watu kisa mdumu madarakani. shame!!
 
Nimemuuliza swali rahisi sana kujibu..

Hiyo kanuni ya kusema kwamba mtu (CAG) asifanywe kama "Mungu", kwani anakosea tu, anaiweka kwa watu wote, akiwamo na Magufuli?

Jibu ni ndiyo au hapana.

Mpaka sasa kapata kigugumizi hajajibu.

Kwa nini?

Kwa sababu, nia yake si kusema mtu asifanywe kama Mungu, angekuwa na nia hiyo angekubali kwamba hata Magufuli naye kwa kuwa si Mungu, hili linamhusu.

Nia yake ni kuleta siasa za majitaka dhidi ya CAG.

Tumemstukia ujanja mwingi mbele kiza.

Kwa johnthebaptist Hili swali jepesi tu sema hakupenda tu kulijibu huenda hakuliona maana watu wengi wali comment.

Kwa sasa natumai atalijibu mjadala uendelee. Hii ndo raha ya JF.
 
Nimemuuliza swali rahisi sana kujibu..

Hiyo kanuni ya kusema kwamba mtu (CAG) asifanywe kama "Mungu", kwani anakosea tu, anaiweka kwa watu wote, akiwamo na Magufuli?

Jibu ni ndiyo au hapana.

Mpaka sasa kapata kigugumizi hajajibu.

Kwa nini?

Kwa sababu, nia yake si kusema mtu asifanywe kama Mungu, angekuwa na nia hiyo angekubali kwamba hata Magufuli naye kwa kuwa si Mungu, hili linamhusu.

Nia yake ni kuleta siasa za majitaka dhidi ya CAG.

Tumemstukia ujanja mwingi mbele kiza.
Mbona humwambii kwamba wewe ndio uliyeleta lugha ya " kujamba"?

Unaweza ukajidanganya kuwa wewe unajua matusi kuliko wanajf wote.

Swali kama lako limeulizwa na wengi akiwemo kamanda Retired kwa ustaarabu kabisa nimewajibu na hawajatokwa povu.

Huko uliko le mutuz aka kubwa jinga anaita " zilipendwa"!!!
 
Mbona humwambii kwamba wewe ndio uliyeleta lugha ya " kujamba"?

Unaweza ukajidanganya kuwa wewe unajua matusi kuliko wanajf wote.

Swali kama lako limeulizwa na wengi akiwemo kamanda Retired kwa ustaarabu kabisa nimewajibu na hawajatokwa povu.

Huko uliko le mutuz aka kubwa jinga anaita " zilipendwa"!!!
Hujajibu swali langu. Huko kwingine hakunihusu.

Na nilishakupa kikombe cha viroja, nikakwambia kwa viroja utanishinda, ila hoja huna.

Umeshindwa kujibu swali rahisi tu.
 
Natoa tu angalizo maana kuna watu hapa wanatamani Controller and Auditor General asiguswe kwa lolote.

Nasema hilo haliwezekani maana CAG ni cheo kinachobebwa na mtu na wala siyo Mungu kwahiyo yeye mwenyewe anaweza kuwa na mapungufu au wasaidizi wake tena ya kibinaadamu kabisa.

Kwa mfano kuna wizara, idara na taasisi nyingi za serikali ambazo zimepewa bajeti kidogo ukilinganisha na mwaka jana lakini watu wanamuona CAG pekee. Tena wengi wanaona ama ameonewa au anafanyiwa figisu za hujuma.

Watanzania tunaelekea wapi jamani, binafsi namkubali sana CAG wa sasa Alhaj Prof Assad lakini hiyo hainifanyi nimuone ni zaidi ya binadamu wengine.
Ni ukweli anaitendea haki dhamana yake lakini ni lazima tukubali kuwa ofisi yake ni ya kawaida tu kama zilivyo ofisi nyingine za serikali.

Niishie hapo
Maendeleo hayana vyama!
mkuu, ingependeza pia ungeanzisha thread nyengine kama hii kuwakumbusha watu kuwa jiwe si Mungu!
 
mkuu, ingependeza pia ungeanzisha thread nyengine kama hii kuwakumbusha watu kuwa jiwe si Mungu!
Huyu kwa kukataa kujibu swali langu kashakubali kwamba kwake Jiwe ni Mungu.
 
Hujajibu swali langu. Huko kwingine hakunihusu.

Na nilishakupa kikombe cha viroja, nikakwambia kwa viroja utanishinda, ila hoja huna.

Umeshindwa kujibu swali rahisi tu.
Silazimiki kukujibu utakavyo wewe huu siyo mtihani na wewe siyo mwalimu.

Kama " unaumia" anzisha thread tutachangia hapa tuko na CAG.

Hahahaa...... Kamanda kiranga unateseka na Dr Magufuli....... Rudi nyumbani kumenoga utalea vibabu hadi lini na uzee umeshakupigia hodi!
 
Huyu kwa kukataa kujibu swali langu kashakubali kwamba kwake Jiwe ni Mungu.
Hahahaa..... Mimi na Dr Magufuli tunamwabudu Mungu wa mbinguni pale St Peters!!!
Tunaamini katika Mungu wa mbinguni anayeishi katika utatu mtakatifu!
 
Hahahaa........ Hiyo thread ataanzisha kamanda kiranga japo anaogopa kweli kweli!
Ila mkuu unamtukuza sana jiwe,. Uongo?!

Ila kawaida, komaa ....kitaa kigum mtu asikwambie. Si unawaona akina kibajaji, mura, na yule prof idara ya maji?
 
Silazimiki kukujibu utakavyo wewe huu siyo mtihani na wewe siyo mwalimu.

Kama " unaumia" anzisha thread tutachangia hapa tuko na CAG.

Hahahaa...... Kamanda kiranga unateseka na Dr Magufuli....... Rudi nyumbani kumenoga utalea vibabu hadi lini na uzee umeshakupigia hodi!
Sijasema unalazimika kunijibu nitakavyo mimi.

Ninasema thread yako haina mantiki na ni ya kinafiki.
 
Ila mkuu ugali umekufanya ufumbe macho. Unasema chadema inamshambulia jiwe, akina Nnape, Bashe, Serukamba etc nao ni CHADEMA?
Nimetoa mfano tu lakini nakushukuru kwa kuongeza nyama kumbe hata wanaccm wanamkosoa Rais Magufuli.
Hiyo ndio CCM bhana baba wa demokrasia!
 
Back
Top Bottom