Kwa hali jinsi inavyoendelea ni dhahiri kabisa ccm inakwenda kupasuka ata kama sio yote lakini asilimia fulani itaathirika.
Nayakumbuka maneno ya Mzee Kingunge juzi alipoongea kwamba ili CCM ishinde yanaitajika maridhiano pia kwa kiasi kikubwa inahitajika Lowasa ashirikishwe katika mchakato wa kampeni za Magufuli.
Hakika nawaambia maneno yale ya Kingunge ni busara na ya muhimu sana japo wako watu wanayakejeli.
Na kwa tetesi zilizopo Ngorongoro,Singida,Kigoma na Tanga wako mbioni kufanya kama walivyofanya leo Monduli.
Dhambi nyingine wanayoifanya CCM ni kutaka kuwakata watu wote wanaowania Ubunge na Udiwani ambao walimsapoti Lowasa.
Hili nmelisikia mwenyewe kwa mtu mkubwa kabisa akiwaambia vijana mkakati huo uliopangwa.
Kwa hakika CCM sasa iko vipande vipande tusifarijiane na kujipa moyo ukweli ndio huo.