Tusidharau vijana. Haya matamko ya kuwasema vibaya na kuwakatisha tamaa yazuiwe

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,250
22,320
Ninaandika kwa masikitiko makubwa kufuatia kuona watu mbalimbali maarufu (Public figures) wakitoa matamko yanayokatisha tamaa na kuwakera vijana. Siwezi kurudia yaliyosemwa ila mengi yana ukakasi. Ifike hatua serikali, CCM na upinzani wawe makini sana na watu wote hasa viongozi wanaotoa kauli za kulisema kundi la vijana kwa kukurupuka.

Vijana wa nchi hii ni wazalendo mno na wanaipenda nchi yao. Na wamekuwa watiifu hata kwa maagizo wasiyoyapenda. Wote tunajua vikwazo vilivyopo kwa vijana kwenye ishu za biashara hasa kuaminika na Taasisi za fedha. Tunajua changamoto kubwa ya ajira. Tunajua changamoto za kiafya hasa ya akili kutokana na msongo wa mawazo. Halafu anatokea mjinga mmoja na kuropokea vijana. HII SIO SAWA.

Ninakisihi sana chama changu CCM kushughulika na watu wa aina hii wanaoibua taharuki zisizo za lazima kwa vijana. Ikumbukwe mabadiliko ya kweli ya kisiasa huletwa na vijana kwenye nchi. Vijana wanaweza kubadili mwelekeo mzima wa siasa za nchi wakiamua. Mwaka 2015 tuliona CHADEMA ikibebwa na vijana na wakatutoa jasho. Mwaka 2021 vijana wa Zambia hawakutaka kujua chama tawala cha PF kilijenga barabara ngapi, vituo vya afya na mambo mengine makubwa bali waliamua kuchagua chama cha upinzani UPND na kuwaingiza Ikulu. Vijana wa Zambia walikuwa wakighasiwa na makada wa chama cha PF kwenye shughuli zao. Charles Taylor aliua watu wengi nchini kwake ila baada ya kucheza karata zake vizuri kwa vijana wakamchagua.

Ninashauri viongozi na Public figures watafakari sana kabla ya kuongea lolote kuhusu vijana kwenye media. Vijana wa Tanzania sio wajinga wala wavivu bali wamechagua kuwa wazalendo kwa nchi yao. Wanaipenda Tanzania kuliko inavyodhaniwa.
 
Ninaandika kwa masikitiko makubwa kufuatia kuona watu mbalimbali maarufu (Public figures) wakitoa matamko yanayokatisha tamaa na kuwakera vijana. Siwezi kurudia yaliyosemwa ila mengi yana ukakasi. Ifike hatua serikali, CCM na upinzani wawe makini sana na watu wote hasa viongozi wanaotoa kauli za kulisema kundi la vijana kwa kukurupuka.

Vijana wa nchi hii ni wazalendo mno na wanaipenda nchi yao. Na wamekuwa watiifu hata kwa maagizo wasiyoyapenda. Wote tunajua vikwazo vilivyopo kwa vijana kwenye ishu za biashara hasa kuaminika na Taasisi za fedha. Tunajua changamoto kubwa ya ajira. Tunajua changamoto za kiafya hasa ya akili kutokana na msongo wa mawazo. Halafu anatokea mjinga mmoja na kuropokea vijana. HII SIO SAWA.

Ninakisihi sana chama changu CCM kushughulika na watu wa aina hii wanaoibua taharuki zisizo za lazima kwa vijana. Ikumbukwe mabadiliko ya kweli ya kisiasa huletwa na vijana kwenye nchi. Vijana wanaweza kubadili mwelekeo mzima wa siasa za nchi wakiamua. Mwaka 2015 tuliona CHADEMA ikibebwa na vijana na wakatutoa jasho. Mwaka 2021 vijana wa Zambia hawakutaka kujua chama tawala cha PF kilijenga barabara ngapi, vituo vya afya na mambo mengine makubwa bali waliamua kuchagua chama cha upinzani UPND na kuwaingiza Ikulu. Vijana wa Zambia walikuwa wakighasiwa na makada wa chama cha PF kwenye shughuli zao. Charles Taylor aliua watu wengi nchini kwake ila baada ya kucheza karata zake vizuri kwa vijana wakamchagua.

Ninashauri viongozi na Public figures watafakari sana kabla ya kuongea lolote kuhusu vijana kwenye media. Vijana wa Tanzania sio wajinga wala wavivu bali wamechagua kuwa wazalendo kwa nchi yao. Wanaipenda Tanzania kuliko inavyodhaniwa.
Kweli kabisa,wawakopeshe kama wanavyowakopesha vyuoni kila mtu kwa anachotaka kufanya,kilimo,ufugaji,ufundi,nk
 
Ninaandika kwa masikitiko makubwa kufuatia kuona watu mbalimbali maarufu (Public figures) wakitoa matamko yanayokatisha tamaa na kuwakera vijana. Siwezi kurudia yaliyosemwa ila mengi yana ukakasi. Ifike hatua serikali, CCM na upinzani wawe makini sana na watu wote hasa viongozi wanaotoa kauli za kulisema kundi la vijana kwa kukurupuka.

Vijana wa nchi hii ni wazalendo mno na wanaipenda nchi yao. Na wamekuwa watiifu hata kwa maagizo wasiyoyapenda. Wote tunajua vikwazo vilivyopo kwa vijana kwenye ishu za biashara hasa kuaminika na Taasisi za fedha. Tunajua changamoto kubwa ya ajira. Tunajua changamoto za kiafya hasa ya akili kutokana na msongo wa mawazo. Halafu anatokea mjinga mmoja na kuropokea vijana. HII SIO SAWA.

Ninakisihi sana chama changu CCM kushughulika na watu wa aina hii wanaoibua taharuki zisizo za lazima kwa vijana. Ikumbukwe mabadiliko ya kweli ya kisiasa huletwa na vijana kwenye nchi. Vijana wanaweza kubadili mwelekeo mzima wa siasa za nchi wakiamua. Mwaka 2015 tuliona CHADEMA ikibebwa na vijana na wakatutoa jasho. Mwaka 2021 vijana wa Zambia hawakutaka kujua chama tawala cha PF kilijenga barabara ngapi, vituo vya afya na mambo mengine makubwa bali waliamua kuchagua chama cha upinzani UPND na kuwaingiza Ikulu. Vijana wa Zambia walikuwa wakighasiwa na makada wa chama cha PF kwenye shughuli zao. Charles Taylor aliua watu wengi nchini kwake ila baada ya kucheza karata zake vizuri kwa vijana wakamchagua.

Ninashauri viongozi na Public figures watafakari sana kabla ya kuongea lolote kuhusu vijana kwenye media. Vijana wa Tanzania sio wajinga wala wavivu bali wamechagua kuwa wazalendo kwa nchi yao. Wanaipenda Tanzania kuliko inavyodhaniwa.
Wapumbavu hao wanadhani idadi ya panya road ikiongezeia Tena panya roads wasomi watakua salama na watoto wao kisa eti Wana mali!!

Ccm chama changu kimeacha misingi ya kuwa chama Cha wafanyakazi na wakulima na kua chama Cha mafisadi na machawa au mashoga wa kifikra!!na sasa kinaenda kusababisha tatizo kubwa la amani kutoweka nchini hapo mbeleni coz mwenye njaa haogopi chochote Tena hata kufa atakuwa tayari!!

Muda sio mrefu vijana hawataogopa Tena risasi hasa wenye njaa na watakua tayari kufa,vyombo vya usalama vijiandae miaka michache ijayo kupambana na vijana walio tayari kufa kwa ujinga wa VIONGOZI wanaowalinda!!
 
Wapumbavu hao wanadhani idadi ya panya road ikiongezeia Tena panya roads wasomi watakua salama na watoto wao kisa eti Wana mali!!

Ccm chama changu kimeacha misingi ya kuwa chama Cha wafanyakazi na wakulima na kua chama Cha mafisadi na machawa au mashoga wa kifikra!!na sasa kinaenda kusababisha tatizo kubwa la amani kutoweka nchini hapo mbeleni coz mwenye njaa haogopi chochote Tena hata kufa atakuwa tayari!!

Muda sio mrefu vijana hawataogopa Tena risasi hasa wenye njaa na watakua tayari kufa,vyombo vya usalama vijiandae miaka michache ijayo kupambana na vijana walio tayari kufa kwa ujinga wa VIONGOZI wanaowalinda!!
Njaa noma sana na umaskini ni janga!
 
Natamani kungekua na muongozo ulionyooka unaofundisha jinsi ya kupata hela, vijana wanachanganyikiwa mara uambiwe ongeza elimu, lima, nenda nje, sali sana.... kila mtu ana lake

Kujipata ni ngumu sana wakati huu
 
Vijana wenyewe ndiyo hawa wanaimba sisi niwalevi tunalewa kwa mnyweso
Tatizo wakipata hela kidogo tuu ni pombe na mademu
Kwa style hii sisi wazee ngoja tule hii nchi kwanza siku mkipata akili tutawapisha na nyie mlambe asali
Usidharau nguvu ya walevi wakiamua kuungana. Ndo maana polisi wakiendaga kufanya msako wa wauza gongo huwa wanaingia kwa mkwara mkali mno ili kutowapa walevi muda wa kujipanga.
 
Usidharau nguvu ya walevi wakiamua kuungana. Ndo maana polisi wakiendaga kufanya msako wa wauza gongo huwa wanaingia kwa mkwara mkali mno ili kutowapa walevi muda wa kujipanga.
Duuuh ila wale washenzi wana umoja na ushirikiano sanaaa kuna kipind wametusumbua sana ikabidi tukune vichwa kutafuta plan B hakika tuliwanyoosha wakahama mtaa
 
Vijana wenyewe ndiyo hawa wanaimba sisi niwalevi

Screenshot_20231025-211457_Instagram Lite.jpg
 
Sahihi kabisa, MAZEE YA NCHI HII ndiyo yaliyoharibu mustakabali mzima wa taifa.

JITU ZEE kama WASSIRA lipo tu toka enzi za mkoloni lakini halina tija yoyote.

Dawa ni kuwatandika makofi tu.
Wanadai siye vijana ni wahuni tu.
 
Natamani kungekua na muongozo ulionyooka unaofundisha jinsi ya kupata hela, vijana wanachanganyikiwa mara uambiwe ongeza elimu, lima, nenda nje, sali sana.... kila mtu ana lake

Kujipata ni ngumu sana wakati huu
Jiwekee mkakati maskini wa chini ya b moja hapaswi kukushauri chochote.
 
Tutafika tu, mbona hawa viongozi wastaarabu sana ngoja mi nishike madaraka ntawatukana kama dharau zilizooneshwa kipindi chote mlivumilia naamini hata matusi yangu mtayavumilia
 
Back
Top Bottom