Tusemezane: Waziri wetu wa Mambo ya Nje,Prof.Kabudi amekosea nini na wapi kwenye hotuba yake kule Kenya? 'Washika bango' mnajijengea mazoea mabaya

Naunga mkono hoja. Kuna watu humu ni pinga pinga, wao kazi yao ni kukosoa tuu kila kitu na kupinga kila kitu, ukiwasahihisha, hawachelewi kukuita gamba, na ukisifia jema lolote la awamu hii, huchelewi kunyooshewa kidole kuwa unatafuta uteuzi.

P.

Nasi tumekuwa na allergy ya kukosolewa kiasi kwamba hata neno "kukosoa" tunajitahidi sana kubadilisha maana yake ili lifanane na kupinga! Maoni tofauti sasa tunaita " kupinga"! Kukosoa ndiyo nguzo ya siasa za ushindani; mtu anayehofu kukosolewa atakuwa na matatizo makubwa sana na hususan hawezi kuwa kiongozi wa kisiasa.
 
kama kusema tu na kuvuta hadhira alifanikiwa! hajakosea Magu hakukosea amwakilishe he is Good!
shida je na huku kwetu tukoje? leo neneo ndugu halipo ni mheshimiwa !!
 
Naunga mkono hoja. Kuna watu humu ni pinga pinga, wao kazi yao ni kukosoa tuu kila kitu na kupinga kila kitu, ukiwasahihisha, hawachelewi kukuita gamba, na ukisifia jema lolote la awamu hii, huchelewi kunyooshewa kidole kuwa unatafuta uteuzi.

P.
Na kuna watu humu humu JF kazi yao ni kusifia tu hata kama katiba inavunjwa! so equation is balanced.
 
Na kuna watu humu humu JF kazi yao ni kusifia tu hata kama katiba inavunjwa! so equation is balanced.
Yes hawa wa aina zote mbili, niliishawahi kuwazungumzia humu.
P
 
Niliposoma humu kuwa eti Waziri wetu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba J.A.M. Kabudi ' ametia aibu' nchi kule Kenya, nikasita kuamini au kutoamini kwakuwa sikuwa nimeiona au kuisikia hotuba yenyewe. Baada ya kuiona na kuisikia hotuba husika, sioni hoja za wasema-hivyo.

Katika hafla hiyo ya Uwasilishaji wa Ripoti ya BBI pale Bomas Kenya, Prof. Kabudi, kama Mwakilishi Maalum wa Rais Magufuli alipata nafasi ya kutoa neno mbele ya halaiki iliyokuwepo pale ikiongozwa na Rais wa Kenya, Makamu wa Rais wa Kenya na Kiongozi wa Upinzani wa Kenya.

Kwanza, Prof. Kabudi alianza kumshukuru Mwenyezi Mungu; kumshukuru Rais wa Kenya na hata Rais Magufuli kwa uwepo wake pale kwenye jambo muhimu kwa Kenya, Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Pili, alionyesha kwa mifano uhusiano wa kindugu uliopo kati ya Kenya na Tanzania.

Tatu, Prof. Kabudi aliwafikishia Wakenya salamu za Rais Magufuli hasa kuwaunga mkono Umoja wa Mataifa na kuwafikishia ujumbe wake ambao ulijikita katika kuwataka wajirekebishe na kusonga mbele pamoja wakiwa wamoja. Akawasihi waweke mbele maslahi ya nchi yao badala ya wao mwenyewe kwakuwa nchi huanza.

Prof. Kabudi, pamoja na mambo mengine, alionesha tofauti kati ya Tanzania na Kenya kuhusu makabila na ukabila ambao huathiri pakubwa siasa na utengemano wa kitaifa nchini Kenya. Akawasihi kutoyaweka makabila mbele na juu ya Kenya. Wakati wote wa neno lake, alishangiliwa na meza Kuu pamoja na kaumu mzima iliyokuwepo. Alishangiliwa kwa ukweli wake ambao hakuwa anapepesa kuutoa.

Hafla ile haikuwa ya kuzungumzia mikataba ya kimataifa na hivyo kuzungumzia mikataba hakukuwa mahala pake. Hafla ile haikuwa kuzungumzia uchaguzi na hakufanya hivyo. Sasa amekosea nini na amekosea wapi? Hata mwishoni alifikisha ujumbe wa wazi wa moja kwa moja kwa Rais Kenyatta, Makamu wa Rais Ruto na Mzee Raila Odinga na wote waliukubali na kuufurahia wakichagizwa na shangwe za wananchi wao.

Prof. Kabudi hapaswi kuponzwa na ukweli wake kwa ndugu zetu Wakenya. Hapaswi kuponzwa na uwazi wake wa kuufikisha ukweli. Hafla ile ililenga kupata maridhiano na umoja ili kusonga mbele kama Wakenya. Ndiyo maana kaumu nzima ilishikana mikono na kumfuatilia Prof. Kabudi aliyewaongoza katika kauli na ahadi za kujenga Kenya mpya.

Tabia ya kuona kila kauli ina makosa ni kujenga tabia mbaya na inayotesa. Washika-bango muwe makini na mjiepushe na tabia zisizojenga!


Pia soma
Nadhani wewe ndio umeelewa vibaya aliyoyazungumza huko Kenya.
Angalia mahojiano yake na BBC leo ndio utajua.
Ukiwa mkweli kwa kila jambo basi utakuwa msikivu mnyenyekevu na confident
Ni mbishi unprofessiona si msikivu hata kidogo amekuwa sawa na mwanamke wa msuto


** Huwezi kusifia mke wa jirani anajua kuvaa wakati wa kwako unamvalisha magunia


** Ndugu '"msomi" ni hivi watu hawapingi alichokizungumza wanamshangaa hayo yote mbona serikali iliyopo madarakani inaenda kinyume na mahubiri yao kwa nchi jirani! Sasa wapi pagumu kuelewa!
 
Niliposoma humu kuwa eti Waziri wetu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba J.A.M. Kabudi ' ametia aibu' nchi kule Kenya, nikasita kuamini au kutoamini kwakuwa sikuwa nimeiona au kuisikia hotuba yenyewe. Baada ya kuiona na kuisikia hotuba husika, sioni hoja za wasema-hivyo.

Katika hafla hiyo ya Uwasilishaji wa Ripoti ya BBI pale Bomas Kenya, Prof. Kabudi, kama Mwakilishi Maalum wa Rais Magufuli alipata nafasi ya kutoa neno mbele ya halaiki iliyokuwepo pale ikiongozwa na Rais wa Kenya, Makamu wa Rais wa Kenya na Kiongozi wa Upinzani wa Kenya.

Kwanza, Prof. Kabudi alianza kumshukuru Mwenyezi Mungu; kumshukuru Rais wa Kenya na hata Rais Magufuli kwa uwepo wake pale kwenye jambo muhimu kwa Kenya, Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Pili, alionyesha kwa mifano uhusiano wa kindugu uliopo kati ya Kenya na Tanzania.

Tatu, Prof. Kabudi aliwafikishia Wakenya salamu za Rais Magufuli hasa kuwaunga mkono Umoja wa Mataifa na kuwafikishia ujumbe wake ambao ulijikita katika kuwataka wajirekebishe na kusonga mbele pamoja wakiwa wamoja. Akawasihi waweke mbele maslahi ya nchi yao badala ya wao mwenyewe kwakuwa nchi huanza.

Prof. Kabudi, pamoja na mambo mengine, alionesha tofauti kati ya Tanzania na Kenya kuhusu makabila na ukabila ambao huathiri pakubwa siasa na utengemano wa kitaifa nchini Kenya. Akawasihi kutoyaweka makabila mbele na juu ya Kenya. Wakati wote wa neno lake, alishangiliwa na meza Kuu pamoja na kaumu mzima iliyokuwepo. Alishangiliwa kwa ukweli wake ambao hakuwa anapepesa kuutoa.

Hafla ile haikuwa ya kuzungumzia mikataba ya kimataifa na hivyo kuzungumzia mikataba hakukuwa mahala pake. Hafla ile haikuwa kuzungumzia uchaguzi na hakufanya hivyo. Sasa amekosea nini na amekosea wapi? Hata mwishoni alifikisha ujumbe wa wazi wa moja kwa moja kwa Rais Kenyatta, Makamu wa Rais Ruto na Mzee Raila Odinga na wote waliukubali na kuufurahia wakichagizwa na shangwe za wananchi wao.

Prof. Kabudi hapaswi kuponzwa na ukweli wake kwa ndugu zetu Wakenya. Hapaswi kuponzwa na uwazi wake wa kuufikisha ukweli. Hafla ile ililenga kupata maridhiano na umoja ili kusonga mbele kama Wakenya. Ndiyo maana kaumu nzima ilishikana mikono na kumfuatilia Prof. Kabudi aliyewaongoza katika kauli na ahadi za kujenga Kenya mpya.

Tabia ya kuona kila kauli ina makosa ni kujenga tabia mbaya na inayotesa. Washika-bango muwe makini na mjiepushe na tabia zisizojenga!


Pia soma
Wakenya wenyewe wanasema hizo "lecture" zake azitoe Tz kwenye ukosefu wa press freedom na freedom of speech.
Tz ambako wapinzani wananyanyaswa na kupigwa risasi.
 
Naunga mkono hoja. Kuna watu humu ni pinga pinga, wao kazi yao ni kukosoa tuu kila kitu na kupinga kila kitu, ukiwasahihisha, hawachelewi kukuita gamba, na ukisifia jema lolote la awamu hii, huchelewi kunyooshewa kidole kuwa unatafuta uteuzi.

P.
Pasco umeona utoe ya moyoni
 
Kuna tatizo au ?
wanakuw awamevunja sheria gani wanapo pinga?
Hakuna tatizo lolote la kisheria bali ni issues za morality. Ilivyo uaminifu kwenye mapenzi, ukiwa married, na ukawa promiscuous, hakuna kosa lolote kisheria, hata kutoka na mke wa mtu, hakuna kosa lolote kisheria.
P
 
Niliposoma humu kuwa eti Waziri wetu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba J.A.M. Kabudi ' ametia aibu' nchi kule Kenya, nikasita kuamini au kutoamini kwakuwa sikuwa nimeiona au kuisikia hotuba yenyewe. Baada ya kuiona na kuisikia hotuba husika, sioni hoja za wasema-hivyo.

Katika hafla hiyo ya Uwasilishaji wa Ripoti ya BBI pale Bomas Kenya, Prof. Kabudi, kama Mwakilishi Maalum wa Rais Magufuli alipata nafasi ya kutoa neno mbele ya halaiki iliyokuwepo pale ikiongozwa na Rais wa Kenya, Makamu wa Rais wa Kenya na Kiongozi wa Upinzani wa Kenya.

Kwanza, Prof. Kabudi alianza kumshukuru Mwenyezi Mungu; kumshukuru Rais wa Kenya na hata Rais Magufuli kwa uwepo wake pale kwenye jambo muhimu kwa Kenya, Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla. Pili, alionyesha kwa mifano uhusiano wa kindugu uliopo kati ya Kenya na Tanzania.

Tatu, Prof. Kabudi aliwafikishia Wakenya salamu za Rais Magufuli hasa kuwaunga mkono Umoja wa Mataifa na kuwafikishia ujumbe wake ambao ulijikita katika kuwataka wajirekebishe na kusonga mbele pamoja wakiwa wamoja. Akawasihi waweke mbele maslahi ya nchi yao badala ya wao mwenyewe kwakuwa nchi huanza.

Prof. Kabudi, pamoja na mambo mengine, alionesha tofauti kati ya Tanzania na Kenya kuhusu makabila na ukabila ambao huathiri pakubwa siasa na utengemano wa kitaifa nchini Kenya. Akawasihi kutoyaweka makabila mbele na juu ya Kenya. Wakati wote wa neno lake, alishangiliwa na meza Kuu pamoja na kaumu mzima iliyokuwepo. Alishangiliwa kwa ukweli wake ambao hakuwa anapepesa kuutoa.

Hafla ile haikuwa ya kuzungumzia mikataba ya kimataifa na hivyo kuzungumzia mikataba hakukuwa mahala pake. Hafla ile haikuwa kuzungumzia uchaguzi na hakufanya hivyo. Sasa amekosea nini na amekosea wapi? Hata mwishoni alifikisha ujumbe wa wazi wa moja kwa moja kwa Rais Kenyatta, Makamu wa Rais Ruto na Mzee Raila Odinga na wote waliukubali na kuufurahia wakichagizwa na shangwe za wananchi wao.

Prof. Kabudi hapaswi kuponzwa na ukweli wake kwa ndugu zetu Wakenya. Hapaswi kuponzwa na uwazi wake wa kuufikisha ukweli. Hafla ile ililenga kupata maridhiano na umoja ili kusonga mbele kama Wakenya. Ndiyo maana kaumu nzima ilishikana mikono na kumfuatilia Prof. Kabudi aliyewaongoza katika kauli na ahadi za kujenga Kenya mpya.

Tabia ya kuona kila kauli ina makosa ni kujenga tabia mbaya na inayotesa. Washika-bango muwe makini na mjiepushe na tabia zisizojenga!


Pia soma
Alichokosea ni kuizungumzia demokrasia jumuishi ambayo haifanyiki Tanzania.
Ebu tupe mfano mmoja wa Demokrasia jumuishi na ushirikishwaji wa wananchi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ya juzi juzi.
Nitakupa mifano ya ukabila ufarakanishi ubaguzi wa kiitikadi ulivyo shamiri awamu hii.
Ubaya zaidi anazungumzia asicho kiamini na ndiyo asili yake.
 
anaposema Kenya waache siasa za chuki na wawe na mshikamano at the same time tunamuona Raila na Uhuru wameketi kwenye meza moja.

Je kwa tanzania ameshawahi kuhubiri upendo huo dhidi ya rais kukaa na wapinzani???
Kwa hali inavyoonekana kwa Tanzania rais kukaa na wapinzani labda ni mpaka YESU atakaporudi mara ya pili kwa sababu upinzani umezidi kunyimwa pumzi kwa lengo ovu la kuuulia mbali
 
Nilichoona mimi kwenye mitandao ya kijamii na kinacho lalanikiwa sio hutuba mbovu ya Prof Kabudi, watu wengi wanalalamikia prof kwenda ku advocate demokrasia among Kenyan wakati nchi yake imebana demokrasia.
Hata hotuba ilikuwa mbovu,kabudi kila sehemu anayosimama kuhutubia huwa anajiona kama bado ni mwalimu wa chuo kikuu na anafundisha wanafunzi wake,anatakiwa abadilike.yani watu wanapambana kufikia pazuri yeye anaenda kuwananga tena ooh nyie mna ukabila,muache siasa za kujinufaisha kanakwamba huku kwetu hayo anayoyasema hayapo,huwezi kupata sababu ya kuwananga wakati wao wameshaliona tatizo lao na wameshakaa chini kulitatua wakati sisi ndio tunaanza kulikimbilia tatizo walilokuwa nalo.
 
Naunga mkono hoja. Kuna watu humu ni pinga pinga, wao kazi yao ni kukosoa tuu kila kitu na kupinga kila kitu, ukiwasahihisha, hawachelewi kukuita gamba, na ukisifia jema lolote la awamu hii, huchelewi kunyooshewa kidole kuwa unatafuta uteuzi.

P.
Wewe babu kwa sasa totally ni gamba ambalo halifai kusomwa humu ndani
 
Recently umekua ukiunga hoja mkono kila kitu.....
Naunga mkono hoja. Kuna watu humu ni pinga pinga, wao kazi yao ni kukosoa tuu kila kitu na kupinga kila kitu, ukiwasahihisha, hawachelewi kukuita gamba, na ukisifia jema lolote la awamu hii, huchelewi kunyooshewa kidole kuwa unatafuta uteuzi.

P.
 
Back
Top Bottom