Tupunguze Siri Wakuu

Tupunguze Siri Wakuu

Habari wana JF.
Tuache Siri kwenye vitu muhimu wakuu hasa kwenye family issues. Kuna partner wangu mmoja hapa kariakoo wiki mbili zilizo pita tulikuwa tunazungumzia kuhusu usiri wa pesa tunazo weka Bank . Jamaa akanambia kahifadhi milioni 28 bank na mke wake hajamwambia hivyo katika familia yake hakuna mwenye taarifa hizo zaidi yake. Tugapipiga story pale na kushauriana mambo mengi ikiwa pia inatakiwa kuweka wazi baadhi ya mambo muhimu Kwa familia. Sasa juzi suddenly mshikaji kapata ajari na tumesha mpoteza(kafariki). Niliwaza vitu vingi Sana hivyo nimeleta hii thread hapa ili tujifunze kitu bank wananufaika na pesa na sio mke au watoto.

So the moral of this story is Let's not keep important family matters a secret. Imagine umejenga hakuna uliye mshirikisha, una pesa bank hakuna uliyemshirikisha, una MTOTO njee hakuna uliyemshirikisha, unabiashara hakuna uliyemshirikisha ukipotea suddenly it's worthless. TUPUNGUZE AU KUACHA KABISA SIRI kwenye mambo ya FAMILIA.
Kawaambie familia yake.Hata hivyo unaweza omba kibali Cha Mahakama kufuatilia accounts zote za marehemu.

Vitu ambavyo ni rahisi kupotea ni Mali zisizohamishika kama Hazina Majina yake.
 
Yuko sahihi 100%
Kwa sababu

Katika uendeshaji wa fedha +Familia ni jambo gumu sana hasa katika zama hizi za watu wasio na utu.
Anaweza kuwa mtoto ama Mke wako pesa ikawa na Thamani kwake kuliko wewe mwenye pesa.

Katika mazingira kama hayo unapaswa kutumia akili kuendesha familia ya dizaini hiyo.

Tunakuwa na marafiki na Ndugu Pia,Katika has kuna watu mtu anakuwa anamuamini ambaye Anakuwa anajua siri zake ambazo hata familia Haijui. Inapotokea shida kama hiyo watasaidia walio baki.

Kuwa msiri kuna muda inatusaidia Sana.
Walio wasiri wengi wamefanikiwa.
 
Kuna thread jamaa mmoja alileta, alilalamika hela yake haitoshi matumizi.

Wanaume wengi wakamshauri amfiche mweke mshahara wake, ili asiwe na mategemeo makubwa.

Watu wengi walionekana kukubaliana na hilo, sasa kipi ni kipi?
 
Ukiona hivyo ni heri.

Mkuu haya maisha ya mafumbo mengi sana.

Pesa,bora afe zibaki huko au ukiona kabisa mambo huelewi kuna taratibu za kufuata ili uache mpunga kwa Watoto wasiteseke na mjane mwenye akili.

Narudia siku hizi watu hawataki NDOA ,wanataka sherehe za MC Dr.Cheni na n.k
Wanataka kupostiana kaolewa kutoka kundi lile walilomaliza Degree,Biashara ,kazini na mtaani.

Nina ushahidi wanaume wengi husukumwa kwenye Sherehe hizi wanawake baadhi wakiamini ni NDOA lakini sio.

Mambo ya kukaa pamoja yakianza unaona kabisa wewe hukuwa Mke au Mume wa aliyekuoa,picha la wazi kabisa.

Ndiko usiri na kuficha vitu huja kwa mwanaume.

Kuna namna Mungu ameumba Mwanaume, japo kwa sasa Dunia inatetea mtoto wa Kike ni sawa ila Mwanaume kuna namna huwa na asili yake daima hata awe bwege kiasi gani.

Siri kwa wanafamilia zetu pia wivu wa maendeleo ni ndugu wachache sana wenye upendo kwenye familia zetu sio wote.

Kuna wengine tuliachwa yatima ila kuna ndugu walisimama nasi kwenye mali zilibakishwa hata kidogo.Wakatunyanyua na kufikia malengo yetu kiasi chake.

NDOA batili ndio chanzo cha siri nyingi kwa wake kwa waume.
Hakika Sir.
 
Hata mimi kwenye mambo ya pesa hua siwaamini hawa viumbe mimi wife mda wote namlilia njaa kila mda nalalamika sina hela😀😀 ila akiomba kitu nampa ila always story ni sina hela. Shida ya hawa viumbe akijua una hela anaanza kukupigia hesabu hela zako akuwekee demand zake ambazo hata yeye ameshindwa kutimiza kwa hela yakr wewe ndio umtimizie😹😹
 
Kuna thread jamaa mmoja alileta, alilalamika hela yake haitoshi matumizi.

Wanaume wengi wakamshauri amfiche mweke mshahara wake, ili asiwe na mategemeo makubwa.

Watu wengi walionekana kukubaliana na hilo, sasa kipi ni kipi?
Ficha hela mzee hela yako ni yako😀😀
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom