Tundu Lisu pekee na computer magamba kalamu za risasi na karatasi

Ilihitajika hapo? Maana wengine wanaenda na laptop kama fashion hata kama haina kazi hapo!Utakuta watu mnaendelea na kikao,mwingine yuko Jf au Facebook anachat! au anafanya kazi yake nyingine tu. Hata hivo hilo laptop la tundu lisu ni kubwa kidogo mpaka linamzuia wajumbe wengine wasimuone! Kwa nini asinunue kile kidogo kabisa akawa anatembea nacho?

So low...wakati mwingine huwa najiuliza hivi hata wewe mwenyewe unaamini unachokiandika au unatumika tu? Unaiabisha nafsi yako...sijui ni shida ndio inakusuma ufanye haya unayofanya au ni uelewa mdogo (which i dont think is the case here) sasa kweli kikao cha kamati computer inakosaje umuhimu. hao wajumbe hapo wana minutes za vikao kibao, ni njia gani bora ya kutunza hizo kama sio computer? Wanajadili masuala technical ni njia gani bora ya kupata refference na rejea mbalimbali kama sio computer? kabla ya kumshauri Lissu anunue "kale kadogo kabisa" huoni ni busara uwashauri hao wenye makaratasi wajifunze matumizi ya computer!
 
pakua+(17).jpg


Tundu lisu pekee na Computer kwenye kikao cha kamati ya kudumu ya katiba, sheria na utawala ya bunge wakati Magamba bado wanatumia kalamu za risasi zenye mfuto kama za watoto wa chekechea kuandikwa kwenye makaratasi, na waliojitajidi kidogo ni kutumia nibu zile za kuchovya kwenye vidao vya wino wakati Lisu anabonyeza vitufe vya computer. Kazi kweli kweli.
...Hao magamba ndio wanaotuharibia nji mpaka sasa watoto wetu wanakaa sakafuni shuleni kwa sababu hata wao wenyewe bado akili zao zimelala na haijulikani wataamka lini. Hovyo kabisa magamba!!
 
Ukienda kwenye ofisi za ccm utakutana na malimba (type writter) kibao zinatumika. Hayo ndiyo magamba. Yana ruzuku kibao lakini inaishia kuhonga wake za watu tu.

Umenivunja mbavu leo bila kutegemea, duh makubwa haya, maana nakumbuka zile malimba za kizamani unatakiwa upate kitumbua kwanza ili kuweze kupiga type, na kelele zake zinasikika hadi njiani na wapita njia wanajua katibu muhtasi yuko kazini. Maana asipogiga kisawasawa stencil haiwezi kutoboka kwa ajili ya kurudifu nakala. Enzi hizo hakukuna na hizi photo copy, sasa Magamba bado wako kwenye era hizo.
 
Hapo alikuwa anachati kwenye facebook na mimi, ila itanisikitisha kama baadae atatoka hapo,ataanza kulalamika. hapo wenzake wanafanya mambo kwa umoja na ndiyo yaliyokuwa yakitakiwa kwenye kikao hicho, Je kuna yeyote anaushahidi wa kuthibitisha kuwa hapo alikuwa akifanya kinachotakiwa? zaidi ya kuchati na mimi kwenye facebook. Toeni kwanza ushaidi wenu halafu wangu unafuatia.
 
Ilihitajika hapo? Maana wengine wanaenda na laptop kama fashion hata kama haina kazi hapo!Utakuta watu mnaendelea na kikao,mwingine yuko Jf au Facebook anachat! au anafanya kazi yake nyingine tu. Hata hivo hilo laptop la tundu lisu ni kubwa kidogo mpaka linamzuia wajumbe wengine wasimuone! Kwa nini asinunue kile kidogo kabisa akawa anatembea nacho?

Kama ni Laptop, ndio size yake - ndogo yake inaitwa netbook.
 
Hapo alikuwa anachati kwenye facebook na mimi, ila itanisikitisha kama baadae atatoka hapo,ataanza kulalamika. hapo wenzake wanafanya mambo kwa umoja na ndiyo yaliyokuwa yakitakiwa kwenye kikao hicho, Je kuna yeyote anaushahidi wa kuthibitisha kuwa hapo alikuwa akifanya kinachotakiwa? zaidi ya kuchati na mimi kwenye facebook. Toeni kwanza ushaidi wenu halafu wangu unafuatia.

hiki kikatuni.ondoa ukatuni wako tupa kule
 
Yani vichupa vya Kilimanjaro vimekuwa ni fashion. Wangeweka vending machines kwenye hallways anaetaka akajichukulie. Unless ni lobbying ya Mengi.

Mengi kaingiaje tena hapa mkuu. Afu wewe una hasira sana na huyu mzee, vp kala kitu gani kwako mkuu tuambie, maana Masha Lawrence naye alianza kama wewe!
 
Ilihitajika hapo? Maana wengine wanaenda na laptop kama fashion hata kama haina kazi hapo!Utakuta watu mnaendelea na kikao,mwingine yuko Jf au Facebook anachat! au anafanya kazi yake nyingine tu. Hata hivo hilo laptop la tundu lisu ni kubwa kidogo mpaka linamzuia wajumbe wengine wasimuone! Kwa nini asinunue kile kidogo kabisa akawa anatembea nacho?


Kwani laptop huhitajika wapi? Size ya laptop hutegemea na mtumiaji sasa wewe unaona kabisa jamaa yuko bespectacled unataka atumie kale ka SAMSUNG ?
 
Kwani laptop huhitajika wapi? Size ya laptop hutegemea na mtumiaji sasa wewe unaona kabisa jamaa yuko bespectacled unataka atumie kale ka SAMSUNG ?

Kale ka SAMSUNG sikapendi kana screen ndogo mno. Mtu unayefanya kazi kubwa na pengine to pull out a couple of open windows unahitaji screen kubwa. Hako kadogo anakosema Rugas ni kwa kuchezea na kuchati si kwa kazi kubwa. Ni kichekesho graphic disign kutumia kakomputa kadogo au katibu huhtasi wakati ana mambo mengi ya kuanya na anatunia muda wote kazini, kwa nini kuumiza macho wakati kubwa yenye kumfaa ipo. Comment nyingine bana?

Pamoja na matumizi ya laptop, hiyo kwangu ni ya kutembea nayo niwapo kazini na safarini, lakini home natumia desktop computer ni bomba kabisa. Mambo haya hutemegea nafasi na matumizi yake.
 
Mengi kaingiaje tena hapa mkuu. Afu wewe una hasira sana na huyu mzee, vp kala kitu gani kwako mkuu tuambie, maana Masha Lawrence naye alianza kama wewe!
Hujaelewa Mengi kaingiaje? Nilisema haya maji huwa ni Kilimanjaro most of the times. Je, ni lobbying ya Mengi kuinunulisha serikali maji kwenye kila warsha na kongamano? Waweke vending machines kwenye front lobby kila mtu ajichukulie vinywaji kivyake.

Sasa usiulize maji ya Kilimanjaro yanahusiana vipi na Mengi, utakuwa mgeni mjini tutakuitia immigration police.
 
pakua+(17).jpg


Jambo moja muhimu anavyofanya Tundu Lisu kuwa na computer kwenye kikao, hapa anaweza downloard kila anachotaka kwa ajili ya reference. Vifungu vyote vya katiba, maelekezo ya kamati na sheria mbalimbali anaweza kuzipata wakati anapohitaji bila kutoka nje ya kikao au kusitisha kikao ili kusubiri kupata hard copy ilikohifadhiwa.

Kwa usahihi hapao Tundu Lisu ana reference zote na hiyo ndiyo siri moja kubwa ya mtu kuwa na hoja ambayo huwa ngumu kupingika akiijenga kutokana na dondoo alizo nazo, na wengine hapo watajibu na kutoa maelezo bila rejea ya vifungu vya sheria na kanuni ambavyo Lisu anavyo live.
 
pakua+%2817%29.jpg


Tundu lisu pekee na Computer kwenye kikao cha kamati ya kudumu ya katiba, sheria na utawala ya bunge wakati Magamba bado wanatumia kalamu za risasi zenye mfuto kama za watoto wa chekechea kuandikwa kwenye makaratasi, na waliojitajidi kidogo ni kutumia nibu zile za kuchovya kwenye vidao vya wino wakati Lisu anabonyeza vitufe vya computer. Kazi kweli kweli.
Wasipoandikia penseli unafikiri watachakachuwa vipi baadae.
 
pakua+%2817%29.jpg


Tundu lisu pekee na Computer kwenye kikao cha kamati ya kudumu ya katiba, sheria na utawala ya bunge wakati Magamba bado wanatumia kalamu za risasi zenye mfuto kama za watoto wa chekechea kuandikwa kwenye makaratasi, na waliojitajidi kidogo ni kutumia nibu zile za kuchovya kwenye vidao vya wino wakati Lisu anabonyeza vitufe vya computer. Kazi kweli kweli.

Tatizo ni hilo ji-computer alilolibeba ni ji "laptop" na hayo sasa ni "out dated" kutembea nayo kwenye mikutano, yanabaki ofisini tu, siku hizi watu mikutanoni na vi "palmtop" na "vi ipad" au vi "tablet", Unaonesha u mwanjo-mwanjo kama huyo Mheshimiwa. Unanchekesha!
 
Tatizo ni hilo ji-computer alilolibeba ni ji "laptop" na hayo sasa ni "out dated" kutembea nayo kwenye mikutano, yanabaki ofisini tu, siku hizi watu mikutanoni na vi "palmtop" na "vi ipad" au vi "tablet", Unaonesha u mwanjo-mwanjo kama huyo Mheshimiwa. Unanchekesha!
  1. Chadema walianza kufanya kampeni kwa chopper, ccm wameiga
  2. Chadema walianza kufanya mikutano kwa magari kwa kutumia truck maalum kama jukwaa, leo CCM wameiga kwa kuanza kutumia truck ya wanamuziki wa TOT kama jukwaa huko Igunga
  3. Zito wa Chadema alianza kutumia Ipad kutoa hotuba ya bajet bungeni kuna waziri mmoja akaanza naye kujifunzia kutumia bungeni hivi karibuni
  4. Tundu Lisu huyo kwenye kamati na labtop, magamba muda si mrefu wataibuka na desktop mikutanoni hata mikutano ya hadhara kama yule aliyepanda jukwaani na trigger kule Igunga.

Siyo siri Chadema wanawaendesha wanamagamba kama gari bovu vile.
 
  1. Chadema walianza kufanya kampeni kwa chopper, ccm wameiga
  2. Chadema walianza kufanya mikutano kwa magari kwa kutumia truck maalum kama jukwaa, leo CCM wameiga kwa kuanza kutumia truck ya wanamuziki wa TOT kama jukwaa huko Igunga
  3. Zito wa Chadema alianza kutumia Ipad kutoa hotuba ya bajet bungeni kuna waziri mmoja akaanza naye kujifunzia kutumia bungeni hivi karibuni
  4. Tundu Lisu huyo kwenye kamati na labtop, magamba muda si mrefu wataibuka na desktop mikutanoni hata mikutano ya hadhara kama yule aliyepanda jukwaani na trigger kule Igunga.

Siyo siri Chadema wanawaendesha wanamagamba kama gari bovu vile.


1) Lakini hawakushinda uchaguzi
2) Lakini hawakushinda uchaguzi
3) Zitto anastahili sifa kuliko huyo anaebeba ji laptop kwenye mikutano, nampa heko na huyo waziri umsemae.
4) Amepitwa na wakati, aongee na Zitto amfundishe kutumia i pad.
 
pakua+%2817%29.jpg


Tundu lisu pekee na Computer kwenye kikao cha kamati ya kudumu ya katiba, sheria na utawala ya bunge wakati Magamba bado wanatumia kalamu za risasi zenye mfuto kama za watoto wa chekechea kuandikwa kwenye makaratasi, na waliojitajidi kidogo ni kutumia nibu zile za kuchovya kwenye vidao vya wino wakati Lisu anabonyeza vitufe vya computer. Kazi kweli kweli.
Unaweza kukuta anasurf jamiiforums tehe tehe tehe tehe huku mambo mengine yakienda.
 
Back
Top Bottom