Tundu Lissu unakumbuka kitu?

Tundu Lissu unakumbuka kitu?

Kwani katiba ya sasa na sheria zetu si zinatambua demokrasia na haki ya vyama kufanya siasa?, lakini mbona hawaiheshimu? Nakuhakikishia hata kama ingekuwa katiba ya Warioba, wangeamua kutoiheshimu wasingeiheshimu tu.
Naungana nawe kwa 100%
 
Mkuu The Boss naomba nitumbukize senti sumuni katika hili bandiko

1.Historia inatufundisha vema. Kenya walipewa 'katiba ya pembeni' wakakataa, wakakomaa hadi walipopata katiba na kuipigia kura. Hadi hapo wananchi walishinda, kura iliamua tu mwelekeo.

2. Hoja ya Tanganyika ilikuwa nzito na ni nzito kuliko zote zilzokuwepo.
Hakukuwa na marufuku ingawa matumizi ya vyombo vya dola yalikuwa kwa mtu, bado katiba ya Warioba ingalitatua tatizo

3. Hoja ya Tanganyika ilitumiwa na CCM ili kuweza kuvuruga bunge.
Utumbuka k.mwenezi alisema 'Rasimu ya Warioba haikubaliki kwa vyovyote'

4. CCM walikuwa na katiba yao. Kuikubali ni kuwapa uhalali wa kuendelea kulaghai Taifa. Ilikuwa kudharau ya maoni ya watu milioni 45 kwa kukubali maoni ya CCM.
Yaani kupuuza maoni ya wengi kwasababu wachache wamekamata mpini

5. Katiba iliyopo(1977) Pamoja na ubovu wake, haina kipengele kinachozuia mikutano wala kuwaweka watu mahabusu bila sababu za kisheria.

Kwavile imewezekana kukiuka katiba iliyopo hakuna uwezekano, mpya, ingekuja na kitu ambacho kingezuia hali iliyopo.

6. Kama wameweza kuvuruga uchaguzi wa znz unaoongozwa na katiba nini kingewashinda kukiuka hiyo ya Sitta ambayo wametengeneza wao wenyewe

7. Kukubali katiba pendekezwa kungepokonya wapinzani hoja ya katiba.
ccm wanajua katiba inayopendekezwa inaweza kufutwa wakati wowote wapinzani wakiingia madarakani. Kuwapa go ahead ilikuwa kujinyima haki kwa siku za baadaye

8.Ukisoma katiba pendekezwa, mambo yote yanayo favor CCM yapo intact.
Kilichofanyika ni kubadilisha lugha. Kukubali katiba hiyo ni kukubali maoni ya 1977'

9. Kama tunakubali katiba pendekezwa ambayo si maoni ya wananchi bali ya CCM, tunaweza kukasimu madaraka ya halmashauri kuu ya CCM kutenda kwa niaba yetu

10. Tukikubali nusu glasi ya maziwa hata kama ina funza tele,tukubaliane na lolote linalofanya sasa hivi. Tumekubali unyonge, hakuna unyonge afadhali , unyonge ni unyonge

Mandela aliaambiwa na makaburu wamtoe aache siasa, akasema atafia gerezani
Nyerere wamepitia wakati mgumu kudai uhuru, hawakukubali nusu glasi ya maziwa

Huko makaburini watakuwa wanageuka kwa 'ghadhabu' na wangepata fursa ya kurudi, wangetucheka kwa kuridhia unyonge hadi mbavu zipasuke warudi kaburini.
 
Hawana hoja za kupambana na wapinzani hivyo wameamua kufanya udikteta uchwara ili kuwadhibiti wapinzani. Kinachofanyika si sawa hata kidogo na kinabidi kipigwe vita na wapenda amani wote nchini. Magufuli hana hati miliki ya nchi kuwa Rais siyo ticket ya kufanya atakavyo bila kuheshimu katiba ya nchi.

Labda majibu anayo yule mzeee wa tume ya uchaguzi,maana ni kweli amshaamsha hizi dhidi ya upinzani awamu hii zimezidi mno.Labda ni zile kura mil 6 zinawakosesha watu usingizi,au kuna cha zaidi tusichojua?!
 
Wanafiki waseme ndiooo ndiooooooooooooooooooooooooo ,wasiowanafiki waseme siyo siyo siyooo.

wanafiki ambao ni wengi kwa idadi ambao ni makada wa CCM kwenye bunge la katiba wangeshinda tu upinzani ungechemsha tu so lissu hana kosa hapo.
Hii nchi sijui tunaipeleka wapi!
 
Katika maisha siku zote ni muhimu kukumbuka makosa tunayoyafanya mara chache sana sisi binadamu tunakumbuka na kukubali makosa ambayo tumeyafanya zamani na yanakuja kutuumiza leo.

Kama ndugu Tundu Lissu atapitia hapa ni vizuri akakumbuka kitu.

'Bunge la Katiba'.....

Hakuna mtu katika bunge lile la katiba aliekuwa na nguvu kama Tundu Lissu yeye alikuwa ndo 'roho' ya kila mtu alietaka 'Rasimu ya Warioba' hata UKAWA ni kama alianzisha yeye na wengine wakamuunga mkono.

Itoshe kusema kuwa kama Tundu Lissu angeweza kuwashawishi wenzie wabaki kwenye bunge la katiba kwa 'faida' zingine hilo lingewezekana

Tusisahau original wanaUKAWA walikuwepo hadi wana CCM ambao walikuwa
wanataka 'Rasimu ya Warioba' iheshimiwe.

lakini kosa kubwa kabisa la wanaUKAWA ni 'kubeba hoja za Tanganyika' mbele ya hoja zoote muhimu za Rasimu ya Warioba.

Rasimu ya Warioba ilikuwa ina faida nyingi zaidi

1.Tume huru ya uchaguzi
2.Kufuta wakuu wa wilaya
3.kupunguza madaraka ya Rais na kadhalika na kadhalika

Leo Tundu Lissu anakamatwa na polisi kwa 'amri za wanasiasa'
Bunge la katiba lilikuwa na nafasi ya kupiga marufuku polisi kupewa amri ya kumkamata mtu.

Hata Kenya now wametuacha Rais wa Kenya hawezi kuitumia polisi kukamata wapinzani wake washalimaliza hilo kwa kupitia katiba.

Leo Rais anateua makada kuwa wakuu wa wilaya na ma DAS.
Katiba hii iliyopo ambayo Magufuli anaitumia ni mbovu kuliko ile ya Samuel Sitta

Laiti kama Tundu Lissu angetumia ushawishi wake japo kupata 'katiba nafuu'
kuliko hii anayoitumia Magufuli now huenda leo wapinzani wasingekuwa 'wanalia kupigwa marufuku siasa'.

Leo Magufuli angelazimika tu kuheshimu na kufuata baadhi ya vitu
Polisi wasingepokea amri.
Wakuu wa mikoa na wilaya labda wasingekuwepo hawa waliopo na kadhalika.

Tukubali tu kwa Wana UKAWA then kususa kushiriki katika bunge la katiba na kuipinga Katiba ya Sitta ambayo laiti wangeshiriki ingekuwa better kuliko hii ilikuwa a big mistake.

Sasa haya ndio mavuno, tumerudi nyuma miaka 50.

Some opportunities never comes twice.
Haya nimawazo ya kushindwa, na unaonekana hukufuatilia Bunge la katiba na kuona walivyo jitahidi kuongea..
 
Hawana hoja za kupambana na wapinzani hivyo wameamua kufanya udikteta uchwara ili kuwadhibiti wapinzani. Kinachofanyika si sawa hata kidogo na kinabidi kipigwe vita na wapenda amani wote nchini. Magufuli hana hati miliki ya nchi kuwa Rais siyo ticket ya kufanya atakavyo bila kuheshimu katiba ya nchi.
Aisee wanavyo tuendesha sivyo
 
Hawana hoja za kupambana na wapinzani hivyo wameamua kufanya udikteta uchwara ili kuwadhibiti wapinzani. Kinachofanyika si sawa hata kidogo na kinabidi kipigwe vita na wapenda amani wote nchini. Magufuli hana hati miliki ya nchi kuwa Rais siyo ticket ya kufanya atakavyo bila kuheshimu katiba ya nchi.
Sijui wanawaogopa wapinzani kwa lipi?
 
Mkuu the boss tunarudi kulekule nilikokuambia hata kama rasimu ya Warioba ingepita bado kwenye kutekeleza ingetegemea utashi wa kiongozi wa kisiasa aliyeko madarakani. Nina mifano hapa chini kukuonyesha ninachoamini kuhusu wanasiasa kutelekeleza ama kutotekeleza kile wanachosema ama kilichopo,
  1. Ulisikia maneno ya JK baada ya kupokea rasimu ya Warioba na maneno aliyozungumza baada ya wanaccm wenzake walichofanya kwenye katiba pendekezwa?
  2. Ulikuwa unasikia zile lugha za kejeli walizokuwa wanatoa wanaccm kwa tume ya Jaji Warioba ambayo H.Polepole alikuwa mjumbe? H.Polepole huyuhuyu aliyekuwa hakubaliani kabisa na cheo cha mkuu wa wilaya leo ni nani?
  3. Huyo Lipumba leo unaweza kujua anasimamia nini mpaka uweze kuwa na imani kwamba hata kama katiba ile ingepita ingetekelezwa na wanasiasa. Huku africa hakuna kutekeleza katiba kama inavyosema bali ni hila tu ndio zinaamua katiba ifuatwe vipi.
Umeeleza vizuri sana
 
Hoja za tume huru ya uchaguzi haikufika
walitoka kabla....
Tena walikubaliana wakati wanakunywa juice na JK kushughulikia hilo swala kwa pamoja kabla ya uchaguzi.
Lakini hadi bunge la mwisho kabla ya uchaguzi wa Oct 2015 si Tundu Lissu, Mbowe au yule jamaa wa ' Mama Tanzania' aliyelifanyia kazi.
Kosa hilo liliwafanya hata washindwe kupinga ile tume kabla ya uchaguzi.
Kwa masikitika Ukawa ya kutafuta katiba ikageuka kikundi cha kampeni cha kutafutia madaraka na vyeo.
 
1.Tume huru ya uchaguzi
2.Kufuta wakuu wa wilaya
3.kupunguza madaraka ya Rais na kadhalika na kadhalika

Naamini kabisa kuwa hayo mambo hapo juu yasingepita mbele za wana ccm!!!!!!!!!!!...........hivi tumesahau hata jinsi kura zilivyo lazimishwa na mzee 6?, mwana sheria wa zanzibar kufukuzwa!............, there was no way kuwazuia ccm kufanya watakavyo!!!!!. and by the way bado siamini kuwa huu mchakato ulisimamishwa kwa sababbu ya ratiba kubana, hasa nikikumbuka matamlo ya walio jiita viongozi wa dini, matusi ya gwajima kwa mzee Pengo,......................
 
Ahsante sana Mkuu,very well said.

Kwani katiba ya sasa na sheria zetu si zinatambua demokrasia na haki ya vyama kufanya siasa?, lakini mbona hawaiheshimu? Nakuhakikishia hata kama ingekuwa katiba ya Warioba, wangeamua kutoiheshimu wasingeiheshimu tu.
 
Back
Top Bottom