Katika maisha siku zote ni muhimu kukumbuka makosa tunayoyafanya mara chache sana sisi binadamu tunakumbuka na kukubali makosa ambayo tumeyafanya zamani na yanakuja kutuumiza leo.
Kama ndugu Tundu Lissu atapitia hapa ni vizuri akakumbuka kitu.
'Bunge la Katiba'.....
Hakuna mtu katika bunge lile la katiba aliekuwa na nguvu kama Tundu Lissu yeye alikuwa ndo 'roho' ya kila mtu alietaka 'Rasimu ya Warioba' hata UKAWA ni kama alianzisha yeye na wengine wakamuunga mkono.
Itoshe kusema kuwa kama Tundu Lissu angeweza kuwashawishi wenzie wabaki kwenye bunge la katiba kwa 'faida' zingine hilo lingewezekana
Tusisahau original wanaUKAWA walikuwepo hadi wana CCM ambao walikuwa
wanataka 'Rasimu ya Warioba' iheshimiwe.
lakini kosa kubwa kabisa la wanaUKAWA ni 'kubeba hoja za Tanganyika' mbele ya hoja zoote muhimu za Rasimu ya Warioba.
Rasimu ya Warioba ilikuwa ina faida nyingi zaidi
1.Tume huru ya uchaguzi
2.Kufuta wakuu wa wilaya
3.kupunguza madaraka ya Rais na kadhalika na kadhalika
Leo Tundu Lissu anakamatwa na polisi kwa 'amri za wanasiasa'
Bunge la katiba lilikuwa na nafasi ya kupiga marufuku polisi kupewa amri ya kumkamata mtu.
Hata Kenya now wametuacha Rais wa Kenya hawezi kuitumia polisi kukamata wapinzani wake washalimaliza hilo kwa kupitia katiba.
Leo Rais anateua makada kuwa wakuu wa wilaya na ma DAS.
Katiba hii iliyopo ambayo Magufuli anaitumia ni mbovu kuliko ile ya Samuel Sitta
Laiti kama Tundu Lissu angetumia ushawishi wake japo kupata 'katiba nafuu'
kuliko hii anayoitumia Magufuli now huenda leo wapinzani wasingekuwa 'wanalia kupigwa marufuku siasa'.
Leo Magufuli angelazimika tu kuheshimu na kufuata baadhi ya vitu
Polisi wasingepokea amri.
Wakuu wa mikoa na wilaya labda wasingekuwepo hawa waliopo na kadhalika.
Tukubali tu kwa Wana UKAWA then kususa kushiriki katika bunge la katiba na kuipinga Katiba ya Sitta ambayo laiti wangeshiriki ingekuwa better kuliko hii ilikuwa a big mistake.
Sasa haya ndio mavuno, tumerudi nyuma miaka 50.
Some opportunities never comes twice.