denoo49
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 6,113
- 6,953
Tehehehhehe, haki ya Mungu!! Huyu Mzee atabatizwa majina yote mpaka muhula uishe tutasikia mengi.Kuna watu ni wa Jinga sana!..
Kwa hiyo Tundu Lisu alaumiwe, Yohana Ulabu apongezwe?
Tehehehhehe, haki ya Mungu!! Huyu Mzee atabatizwa majina yote mpaka muhula uishe tutasikia mengi.Kuna watu ni wa Jinga sana!..
Kwa hiyo Tundu Lisu alaumiwe, Yohana Ulabu apongezwe?
katiba ni mchakato mrefu, hata kama ingepita isingeanza kutumika hapo hapoKatiba ya sasa Rais anamteua mkuu wa polisi
ni rahisi kwake kumpa amri
ingekuwa katiba hana mamlaka ya kumteua mkuu wa polisi ingekuwa rahisi kuliko sasa
Mbona hata katiba hii mbovu iliyopo nayo ameshindwa kuiheshinu?Wao walitaka kupata kila kitu
kumbe wangepata tu hata Tume huru ya uchaguzi ingewasaidia....
Walipiga kura mpaka mahujaji mpaka marehemu ungetegemea nini hapo hata wangekuwepo?
Mkuu, Wanasiasa wengi wa Tanzania hawana vision, wao wanachoangalia ni sifa za wakati uliopo. Ndo maana nakuwa mgumu sana kuamini kile wanasiasa wanachokisema, huwa nabakia kuwa mtu huru tu nisiye na upande wowote.
Hupo BAK mambo yanaenda ila Katiba hii, na Tume hii ndio iliofanya Chadema wawe na Wabunge bungeni pamoja na CUF...Bado katiba hii yenye viraka chungu nzima pamoja na ubaya wake inaruhusu maandamano na mikutano ya vyama vya upinzani ambayo hakuna yoyote mwenye ruhusa ya kuwaamulia wapinzani nini cha kuzungumza kwenye mikutano yao na wapi pa kufanyia mikutano yao bila kujali kama wana mbunge kwenye jimbo husika au la. Na yeyote anayewazuia wapinzani kufanya hivyo anakiuka katiba ya nchi.
Tatizo la Chadema wanapenda shortcut, mfano walijijenga zaidi ya miaka 20, wakiwa wenyewe na nguvu, ghafla wanamchukua Lowasa.. Hii ni shortcut iliowagharimu sana.. Ni bora wangebaki na SLAA naamin wangekua na Wabunge wengi kuliko CCM..